Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 16.2
Bible en Swahili de l’est


1 Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.
Proverbes 19.21 Proverbes 16.9 Proverbes 20.24 Matthieu 10.19-10.20 Philippiens 2.13
2 Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huzipima roho za watu.
Proverbes 21.2 1 Samuel 16.7 Proverbes 30.12 Luc 16.15 Proverbes 24.12
3 Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika.
Psaumes 37.4-37.5 Proverbes 3.6 Psaumes 55.22 Philippiens 4.6 1 Pierre 5.7
4 Bwana amefanya kila kitu kwa kusudi lake; Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.
Romains 9.22 Esaïe 43.21 1 Pierre 2.8 Esaïe 43.7 Romains 11.36
5 Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu.
Proverbes 6.16-6.17 Proverbes 11.21 Proverbes 8.13 Jacques 4.6 Romains 2.8-2.9
6 Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha Bwana watu hujiepusha na maovu.
Proverbes 14.16 Job 28.28 Daniel 4.27 Luc 11.41 Proverbes 8.13
7 Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye.
Genèse 33.4 Jérémie 15.11 2 Chroniques 17.10 1 Jean 3.22 Hébreux 13.21
8 Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
Psaumes 37.16 Proverbes 15.16 Michée 6.10 Jérémie 17.11 1 Timothée 6.6-6.9
9 Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.
Proverbes 19.21 Proverbes 16.1 Psaumes 37.23 Proverbes 20.24 Jérémie 10.23
10 Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme; Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.
Esaïe 32.1-32.2 Psaumes 99.4 Psaumes 45.6-45.7 Amos 5.7 1 Rois 3.28
11 Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya Bwana; Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.
Proverbes 11.1 Ezéchiel 45.10 Amos 8.5 Deutéronome 25.13-25.15 Proverbes 20.23
12 Wafalme wakitenda yasiyo haki ni chukizo; Maana kiti cha enzi huthibitika kwa haki.
Proverbes 25.5 Proverbes 29.14 Deutéronome 25.16 Proverbes 20.18 Luc 12.48
13 Midomo ya haki ni furaha ya wafalme; Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.
Proverbes 14.35 Proverbes 22.11 Psaumes 101.5-101.7
14 Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.
Proverbes 19.12 Proverbes 20.2 Actes 12.20 Daniel 3.13-3.25 2 Rois 6.31-6.33
15 Kuna uhai katika nuru ya uso wa mfalme, Na fadhili zake ni kama wingu la masika.
Job 29.23-29.24 Psaumes 72.6 Psaumes 30.5 Psaumes 4.6 Proverbes 19.12
16 Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu? Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.
Proverbes 8.19 Proverbes 8.10-8.11 Job 28.13-28.28 Psaumes 119.127 Proverbes 4.7
17 Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu; Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.
Apocalypse 3.10 Esaïe 35.8 Proverbes 10.9 Tite 2.10-2.14 Proverbes 19.16
18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.
Proverbes 11.2 Proverbes 18.12 Esaïe 2.11-2.12 Abdias 1.3-1.4 Proverbes 29.23
19 Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini, Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.
Esaïe 57.15 Exode 15.9 Proverbes 29.23 Matthieu 5.3 Esaïe 10.6
20 Atakayelitafakari neno atapata mema; Na kila amwaminiye Bwana ana heri.
Psaumes 2.12 Proverbes 19.8 Psaumes 34.8 Proverbes 13.15 Matthieu 10.16
21 Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara; Utamu wa maneno huongeza elimu.
Proverbes 16.23-16.24 Esaïe 50.4 Jean 7.46 Luc 4.22 Proverbes 15.7
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao; Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.
Proverbes 13.14 Proverbes 10.11 Jean 5.24 Luc 6.39-6.40 Matthieu 15.14
23 Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake; Huzidisha elimu ya midomo yake.
Proverbes 15.28 Matthieu 12.34-12.35 Colossiens 3.16 Psaumes 45.1 Psaumes 37.30-37.31
24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
Proverbes 24.13-24.14 Psaumes 19.10 Proverbes 25.11-25.12 Psaumes 119.103 Proverbes 4.22
25 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
Proverbes 14.12 Actes 26.9 Proverbes 12.15 2 Corinthiens 13.5 Proverbes 12.26
26 Nafsi yake mfanya kazi hujifanyia kazi; Maana kinywa chake humtia bidii.
Ecclésiaste 6.7 2 Thessaloniciens 3.8-3.12 Proverbes 14.23 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 Proverbes 9.12
27 Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara; Katika midomo yake mna moto uteketezao.
Jacques 3.6 Psaumes 17.14-17.15 Psaumes 52.2-52.4 Proverbes 6.14 Psaumes 57.4
28 Mtu mshupavu huondokesha fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.
Proverbes 17.9 Proverbes 15.18 Proverbes 18.8 Proverbes 30.33 Proverbes 29.22
29 Mtu mkali humshawishi mwenzake; Humwongoza katika njia isiyo njema.
Néhémie 6.13 1 Samuel 22.7-22.9 1 Samuel 19.17 Proverbes 3.31 1 Samuel 23.19-23.21
30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.
Proverbes 10.10 Proverbes 16.27 Jean 3.20 Matthieu 14.7-14.8 Esaïe 6.10
31 Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.
Proverbes 20.29 Lévitique 19.32 1 Samuel 12.2-12.5 Proverbes 3.1-3.2 Genèse 47.7-47.10
32 Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.
Proverbes 15.18 Proverbes 14.29 Proverbes 19.11 Jacques 1.19 Romains 12.21
33 Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za Bwana.
Proverbes 18.18 Jonas 1.7 Néhémie 11.1 1 Samuel 14.41-14.42 Josué 18.10

Cette Bible est dans le domaine public.