Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 6.20
Bible en Swahili de l’est


Encouragements de Dieu à Moïse

1 Bwana akamwambia Musa, Sasa utaona nitakavyomtenda Farao; maana kwa mkono hodari atawapa ruhusa kwenda zao, na kwa mkono hodari atawafukuza katika nchi yake.
Exode 12.33 Exode 12.39 Exode 3.19-3.20 Exode 12.31 Exode 11.1
2 Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA;
Malachie 3.6 Esaïe 42.8 Exode 14.18 Actes 17.24-17.25 Esaïe 43.15
3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.
Psaumes 83.18 Psaumes 68.4 Genèse 17.1 Genèse 48.3 Exode 3.14
4 Tena nimelithibitisha agano langu nao, la kuwapa nchi ya Kanaani; nchi ya kukaa kwao hali ya ugeni.
Genèse 15.18 Genèse 28.4 Genèse 17.7-17.8 Genèse 26.3 Genèse 17.13
5 Na zaidi ya hayo, nimesikia kuugua kwao wana wa Israeli, ambao Wamisri wanawatumikisha, nami nimelikumbuka agano langu.
Exode 2.24 Psaumes 106.44-106.45 Esaïe 63.9 Genèse 8.1 Genèse 9.15
6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa;
Deutéronome 26.8 1 Chroniques 17.21 Deutéronome 7.8 Néhémie 1.10 Exode 7.4
7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri.
Deutéronome 4.20 Deutéronome 29.13 Deutéronome 7.6 Exode 29.45-29.46 Apocalypse 21.7
8 Nami nitawaleta hata nchi ile ambayo naliinua mkono wangu, niwape Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; nitawapa iwe urithi wenu; Mimi ni YEHOVA.
Genèse 26.3 Genèse 15.18 Ezéchiel 20.5-20.6 Genèse 14.22 Exode 32.13
9 Musa akawaambia wana wa Israeli maneno haya; lakini hawakumsikiliza Musa kwa ajili ya uchungu wa moyo, na kwa ajili ya utumwa mgumu.
Exode 5.21 Exode 14.12 Job 21.4 Proverbes 14.19 Nombres 21.4
10 Bwana akasema na Musa, akamwambia,
11 Ingia ndani, ukaseme na Farao, mfalme wa Misri, ili awape ruhusa wana wa Israeli watoke nchi yake.
Exode 5.1 Exode 5.23 Exode 7.1 Exode 3.10 Exode 6.29
12 Musa akanena mbele ya Bwana, akasema, Tazama, hao wana wa Israeli hawakunisikiza mimi; basi huyo Farao atanisikizaje, mimi niliye na midomo isiyo tohara?
Jérémie 1.6 Exode 6.30 Exode 4.10 Exode 6.9 Jérémie 6.10
13 Bwana akanena na Musa na Haruni, akawaagiza wawaendee wana wa Israeli, na Farao, mfalme wa Misri, ili awatoe hao wana wa Israeli katika nchi ya Misri.
Psaumes 91.11 Nombres 27.23 1 Timothée 1.18 2 Timothée 2.4 Nombres 27.19

Généalogie de Moïse et d’Aaron

14 Hawa ndio vichwa vya nyumba za baba zao: wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli; ni Hanoki, na Palu, na Hesroni, na Karmi; hao ni jamaa za Reubeni.
Genèse 46.9 1 Chroniques 5.3 Nombres 26.5-26.7 Josué 13.15 Exode 6.25
15 Na wana wa Simeoni; ni Yemueli, na Yamini, na Ohadi, na Yakini, na Sohari, na Shauli mwana wa mwanamke wa Kikanaani; hao ni jamaa za Simeoni.
Genèse 46.10 1 Chroniques 4.24 Nombres 26.12-26.13
16 Na haya ndiyo majina ya wana wa Lawi, sawasawa na vizazi vyao; Gershoni, na Kohathi, na Merari; na miaka ya maisha yake Lawi ilikuwa ni miaka mia na thelathini na saba.
Nombres 3.17 Genèse 46.11 1 Chroniques 6.16 1 Chroniques 6.1 Nombres 26.57
17 Wana wa Gershoni; ni Libni, na Shimei, sawasawa na jamaa zao.
1 Chroniques 6.17 Nombres 3.18 1 Chroniques 23.7 Genèse 46.11
18 Na wana wa Kohathi; ni Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli; na miaka ya maisha ya huyo Kohathi ilikuwa ni miaka mia na thelathini na mitatu.
1 Chroniques 6.18 1 Chroniques 6.2 Nombres 3.19 Nombres 26.57
19 Na wana wa Merari; ni Mali, na Mushi. Hizi ni jamaa za hao Walawi sawasawa na vizazi vyao.
1 Chroniques 23.21 Nombres 3.20 1 Chroniques 6.19
20 Huyo Amramu akamwoa Yokebedi ndugu ya baba yake; naye akamzalia Haruni, na Musa; na miaka ya maisha yake Amramu ilikuwa ni miaka mia na thelathini na saba.
Nombres 26.59 Exode 2.1-2.2 Exode 6.18 Exode 6.16
21 Na wana wa Ishari; ni Kora, na Nefegi, na Zikri.
Nombres 16.1 1 Chroniques 6.37-6.38 Nombres 16.32 Nombres 26.10-26.11 Exode 6.24
22 Na wana wa Uzieli; ni Mishaeli, na Elisafani, na Sithri.
Lévitique 10.4 Nombres 3.30 Néhémie 3.20
23 Haruni akamwoa Elisheba, binti ya Aminadabu, umbu lake Nashoni; naye akamzalia Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
Ruth 4.19-4.20 1 Chroniques 6.3 Nombres 2.3 Nombres 1.7 Matthieu 1.4
24 Na wana wa Kora; ni Asiri, na Elkana, na Abiasafu; hizo ni jamaa za hao Wakora.
1 Chroniques 6.22-6.23 1 Chroniques 6.37-6.38 Nombres 16.1 Nombres 16.32 Nombres 26.9-26.11
25 Na Eleazari mwana wa Haruni akamwoa mmoja miongoni mwa binti za Putieli; naye akamzalia Finehasi. Hawa ndio vichwa vya nyumba za mababa ya Walawi sawasawa na jamaa zao.
Josué 24.33 Nombres 25.7-25.13 Josué 22.31-22.32 Psaumes 106.30-106.31 Josué 22.13
26 Hawa ni Haruni ye yule, na Musa ye yule, Bwana aliowaambia, akisema, Watoeni wana wa Israeli watoke nchi ya Misri sawasawa na majeshi yao.
Exode 12.17 Exode 7.4 Exode 12.51 Exode 6.13 Nombres 33.1
27 Ni hao walionena na Farao mfalme wa Misri ili wawatoe wana wa Israeli watoke Misri; hao ni Musa ye yule, na Haruni ye yule.
Exode 32.7 Exode 33.1 Exode 6.26 Exode 5.1-5.3 Exode 6.13
28 Ilikuwa siku hiyo Bwana aliponena na Musa katika nchi ya Misri,
29 Bwana akamwambia Musa, akasema, Mimi ni Bwana; mwambie Farao mfalme wa Misri maneno yote nikuambiayo.
Exode 6.11 Exode 7.2 Exode 6.2 Exode 6.8 Exode 6.6
30 Musa akanena mbele ya Bwana, Mimi ni mtu mwenye midomo isiyo tohara, Farao atanisikizaje?
Exode 6.12 Exode 4.10 1 Corinthiens 9.16-9.17

Cette Bible est dans le domaine public.