Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 34
Bible en Swahili de l’est


Le salut de l’Éternel pour le juste

1 Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Psaumes 145.1-145.2 1 Thessaloniciens 5.18 Psaumes 71.14-71.15 Actes 16.25 Colossiens 3.17
2 Katika Bwana nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie wakafurahi.
Jérémie 9.24 Psaumes 119.74 1 Corinthiens 1.31 Psaumes 44.8 1 Timothée 1.15-1.16
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Psaumes 69.30 Luc 1.46 Apocalypse 19.5-19.6 Psaumes 66.8 Psaumes 103.20-103.22
4 Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
Psaumes 18.6 Psaumes 116.1-116.6 Matthieu 7.7 Psaumes 56.3 2 Timothée 1.7
5 Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya.
Psaumes 123.1-123.2 Hébreux 12.2 Psaumes 97.11 Esaïe 45.22 Psaumes 36.9
6 Maskini huyu aliita, Bwana akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.
Psaumes 40.17 2 Samuel 22.1 Psaumes 34.17-34.19 Apocalypse 7.14-7.17 Psaumes 3.4
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Daniel 6.22 Psaumes 91.11 Hébreux 1.14 2 Rois 6.17 2 Rois 19.35
8 Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini.
Hébreux 6.4-6.5 1 Pierre 2.2-2.3 Psaumes 119.103 Jérémie 31.14 Psaumes 63.5
9 Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
Psaumes 23.1 Philippiens 4.19 Psaumes 31.23 Esaïe 8.13-8.14 Psaumes 22.23
10 Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.
Psaumes 84.11 Job 4.10-4.11 Matthieu 6.32 Psaumes 104.21 Luc 1.51-1.53
11 Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana.
Psaumes 32.8 Proverbes 1.7 Psaumes 111.10 Proverbes 8.32 Proverbes 8.17
12 Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema?
1 Pierre 3.10-3.12 Psaumes 21.4 Deutéronome 30.20 Psaumes 4.6 Ecclésiaste 3.13
13 Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.
1 Pierre 2.22 Jacques 3.2 Jacques 1.26 Psaumes 141.3 Jacques 3.5-3.10
14 Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.
Hébreux 12.14 Psaumes 37.27 Esaïe 1.16-1.17 Romains 12.18 Proverbes 16.16-16.17
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao.
Psaumes 34.17 Job 36.7 Psaumes 33.18 Psaumes 34.6 Psaumes 130.2
16 Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Jérémie 44.11 Lévitique 17.10 Proverbes 10.7 Amos 9.4 Job 18.17
17 Walilia, naye Bwana akasikia, Akawaponya na taabu zao zote.
Esaïe 65.24 Psaumes 34.6 Psaumes 91.15 Psaumes 145.18-145.20 Psaumes 34.19
18 Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.
Psaumes 147.3 Psaumes 145.18 Esaïe 57.15 Esaïe 61.1 Psaumes 51.17
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote.
Psaumes 34.17 2 Corinthiens 4.17 Psaumes 34.6 1 Pierre 4.12-4.13 Proverbes 24.16
20 Huihifadhi mifupa yake yote, Haukuvunjika hata mmoja.
Jean 19.36 Psaumes 91.12 Psaumes 35.10 Daniel 6.22-6.24
21 Uovu utamwua asiye haki, Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa.
Psaumes 94.23 Luc 19.41-19.44 Psaumes 37.12-37.15 Exode 20.7 Jean 15.18-15.23
22 Bwana huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao.
Psaumes 103.4 Psaumes 71.23 2 Samuel 4.9 1 Pierre 1.5 Apocalypse 5.9

Cette Bible est dans le domaine public.