Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 135.13
Bible en Swahili de l’est


Le Dieu véritable et les idoles

1 Haleluya. Lisifuni jina la Bwana, Enyi watumishi wa Bwana, sifuni.
Psaumes 134.1 Psaumes 107.15 Psaumes 107.8 Psaumes 113.1-113.3 Néhémie 9.5
2 Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana, Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu.
Psaumes 116.19 Psaumes 92.13 Luc 2.37 Psaumes 96.8 1 Chroniques 16.37-16.42
3 Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema, Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza.
Psaumes 147.1 Psaumes 119.68 Psaumes 118.1 Psaumes 33.1 Psaumes 92.1-92.2
4 Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo, Na Israeli, wawe watu wake hasa.
Deutéronome 10.15 1 Pierre 2.9 Deutéronome 7.6-7.7 Malachie 3.17 Tite 2.14
5 Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu, Na Bwana wetu yu juu ya miungu yote.
Psaumes 97.9 Psaumes 95.3 Psaumes 48.1 Esaïe 40.25 Psaumes 96.4-96.5
6 Bwana amefanya kila lililompendeza, Katika mbingu na katika nchi, Katika bahari na katika vilindi vyote.
Psaumes 115.3 Matthieu 8.26-8.27 Amos 4.13 Psaumes 136.13-136.15 Amos 9.6
7 Ndiye apandishaye mvuke toka miisho ya nchi; Huifanyia mvua umeme; Hutoa upepo katika hazina zake.
Jérémie 10.13 Zacharie 10.1 Jérémie 51.16 Job 28.25-28.26 Psaumes 148.8
8 Aliwapiga wazaliwa wa kwanza wa Misri, Wa wanadamu na wa wanyama.
Psaumes 78.51 Exode 12.12 Psaumes 105.36 Exode 12.29-12.30 Exode 13.15
9 Alipeleka ishara na maajabu kati yako, Ee Misri, Juu ya Farao na watumishi wake wote.
Psaumes 136.15 Deutéronome 6.22 Deutéronome 4.34 Exode 7.1-7.15 Jérémie 32.20-32.21
10 Aliwapiga mataifa mengi, Akawaua wafalme wenye nguvu;
Psaumes 136.17-136.22 Nombres 21.24 Psaumes 44.2-44.3
11 Sihoni, mfalme wa Waamori, Na Ogu, mfalme wa Bashani, Na falme zote za Kanaani.
Josué 12.7-12.24 Deutéronome 2.30-3.11 Néhémie 9.22 Deutéronome 29.7 Josué 10.1-10.12
12 Akaitoa nchi yao iwe urithi, Urithi wa Israeli watu wake.
Psaumes 78.55 Psaumes 136.21-136.22 Josué 11.23 Josué 12.7 Nombres 33.54
13 Ee Bwana, jina lako ni la milele, Bwana, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Psaumes 102.12 Exode 3.15 Matthieu 6.9 Psaumes 72.17 Psaumes 8.9
14 Kwa kuwa Bwana atawaamua watu wake, Atawahurumia watumishi wake.
Deutéronome 32.36 Psaumes 50.4 Juges 10.16 Psaumes 7.8 Jonas 4.2
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
Psaumes 115.4-115.8 Esaïe 44.9-44.20 Habakuk 2.18-2.19 Esaïe 46.6-46.7 Actes 17.29
16 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
Esaïe 6.10 Matthieu 13.14-13.16
17 Zina masikio lakini hazisikii, Wala hamna pumzi vinywani mwake.
18 Wazifanyao watafanana nazo, Na kila mmoja anayezitumainia.
Psaumes 97.7 Jérémie 10.8 2 Corinthiens 4.4 Esaïe 44.18-44.20 Psaumes 115.8
19 Enyi mlango wa Israeli, mhimidini Bwana; Enyi mlango wa Haruni, mhimidini Bwana;
Psaumes 147.19-147.20 Psaumes 145.10 Psaumes 118.1-118.4 Apocalypse 19.5 Psaumes 115.9-115.11
20 Enyi mlango wa Lawi, mhimidini Bwana; Ninyi mnaomcha Bwana, mhimidini Bwana.
21 Na ahimidiwe Bwana toka Sayuni, Akaaye Yerusalemu. Haleluya.
Psaumes 134.3 Psaumes 132.13-132.14 Psaumes 48.9 Esaïe 12.6 2 Chroniques 6.6

Cette Bible est dans le domaine public.