Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 106.42
Bible en Swahili de l’est


L’infidélité d’Israël et la bonté de Dieu

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Psaumes 105.1 Psaumes 107.1 1 Chroniques 16.34 Psaumes 136.1 1 Thessaloniciens 5.18
2 Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana, Kuzihubiri sifa zake zote?
Néhémie 9.5 Job 26.14 Psaumes 145.3-145.12 Romains 11.33 Psaumes 40.5
3 Heri washikao hukumu, Na kutenda haki sikuzote.
Psaumes 15.2 Apocalypse 22.14 Galates 6.9 Jacques 1.25 Ezéchiel 18.21-18.22
4 Ee Bwana, unikumbuke mimi, Kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako. Unijilie kwa wokovu wako,
Psaumes 119.132 Luc 23.42 Actes 15.14 Néhémie 13.22 Néhémie 13.14
5 Ili niuone wema wa wateule wako. Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako, Na kujisifu pamoja na watu wako.
Psaumes 105.6 Psaumes 105.43 2 Thessaloniciens 2.13 Jean 15.16 Psaumes 1.3
6 Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.
1 Rois 8.47 Néhémie 9.16 Lévitique 26.40 Psaumes 78.8 Esdras 9.6-9.7
7 Baba zetu katika Misri Hawakufikiri matendo yako ya ajabu; Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako; Wakaasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Exode 14.11-14.12 Psaumes 78.42 Lamentations 3.32 Psaumes 51.1 Ephésiens 2.11
8 Lakini akawaokoa kwa ajili ya jina lake, Ayadhihirishe matendo yake makuu.
Exode 9.16 Ezéchiel 20.9 Ezéchiel 20.14 Ezéchiel 20.22 Ezéchiel 20.44
9 Akaikemea bahari ya Shamu ikakauka, Akawaongoza vilindini kana kwamba ni uwanda.
Psaumes 18.15 Nahum 1.4 Esaïe 63.11-63.14 Psaumes 78.13 Psaumes 114.3-114.7
10 Akawaokoa na mkono wa mtu aliyewachukia, Na kuwakomboa na mkono wa adui zao.
Psaumes 107.2 Exode 14.30 Deutéronome 11.4 Michée 6.4 Exode 15.9-15.10
11 Maji yakawafunika watesi wao, Hakusalia hata mmoja wao.
Exode 15.5 Exode 14.27-14.28 Psaumes 78.53 Exode 14.13 Exode 15.10
12 Ndipo walipoyaamini maneno yake, Waliziimba sifa zake.
Exode 14.31-15.21 Jean 8.30-8.31 Luc 8.13
13 Wakayasahau matendo yake kwa haraka, Hawakulingojea shauri lake.
Exode 15.24 Exode 16.2 Psaumes 78.11 Proverbes 1.25 Exode 17.2
14 Bali walitamani sana jangwani, Wakamjaribu Mungu nyikani.
1 Corinthiens 10.9 Exode 17.2 Nombres 11.4 1 Corinthiens 10.6 Psaumes 78.18-78.20
15 Akawapa walichomtaka, Akawakondesha roho zao.
Esaïe 10.16 Nombres 11.31-11.34 Esaïe 24.16 Psaumes 78.29-78.31
16 Wakamhusudu Musa matuoni, Na Haruni, mtakatifu wa Bwana.
Nombres 16.1-16.50 Lévitique 21.10-21.12 Exode 28.36 Lévitique 21.6-21.8
17 Nchi ikapasuka ikammeza Dathani, Ikaufunika mkutano wa Abiramu.
Deutéronome 11.6 Nombres 16.29-16.33 Nombres 26.10
18 Moto ukawaka katika mkutano wao, Miali yake ikawateketeza wabaya.
Nombres 16.35-16.40 Nombres 16.46 Hébreux 12.29
19 Walifanya ndama huko Horebu, Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.
1 Corinthiens 10.7 Exode 32.4-32.8 Néhémie 9.18 Exode 32.35 Deutéronome 9.8
20 Wakaubadili utukufu wao Kuwa mfano wa ng’ombe mla majani.
Jérémie 2.11 Esaïe 40.18-40.25 Exode 20.4-20.5 Psaumes 89.17 Romains 1.22-1.23
21 Wakamsahau Mungu, mwokozi wao, Aliyetenda makuu katika Misri.
Psaumes 106.13 Deutéronome 10.21 Tite 3.4-3.6 Deutéronome 4.34 Psaumes 135.9
22 Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu, Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu.
Psaumes 78.51 Psaumes 105.23 Exode 14.25-14.28 Psaumes 105.27-105.36 Exode 15.10
23 Akasema ya kuwa atawaangamiza Kama Musa, mteule wake, asingalisimama, Mbele zake kama mahali palipobomoka, Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu.
Psaumes 105.6 Ezéchiel 22.30 Deutéronome 9.25 Ezéchiel 20.8 Jean 15.16
24 Wakaidharau nchi ile ya kupendeza, Wala hawakuliamini neno lake.
Deutéronome 1.32 Nombres 14.31 Ezéchiel 20.6 Hébreux 3.18-3.19 Jérémie 3.19
25 Bali wakanung’unika hemani mwao, Wala hawakuisikiliza sauti ya Bwana.
Psaumes 95.7-95.9 Hébreux 3.15 Nombres 14.22 Deutéronome 1.26-1.27 Hébreux 3.7-3.8
26 Ndipo alipowainulia mkono wake, Ya kuwa atawaangamiza jangwani,
Ezéchiel 20.15 Hébreux 3.11 Psaumes 95.11 Nombres 14.28-14.35 Exode 6.8
27 Na kuwatawanya wazao wao kati ya mataifa, Na kuwatapanya katika nchi mbali.
Psaumes 44.11 Lévitique 26.33 Deutéronome 28.37 Deutéronome 32.26-32.27 Ezéchiel 20.23
28 Wakajiambatiza na Baal-Peori, Wakazila dhabihu za wafu.
Osée 9.10 Deutéronome 4.3 Nombres 25.5 1 Corinthiens 10.19-10.20 Jérémie 10.8-10.10
29 Wakamkasirisha kwa matendo yao; Tauni ikawashambulia.
Ecclésiaste 7.29 Nombres 25.9 Deutéronome 32.16-32.21 1 Corinthiens 10.8 Romains 1.21-1.24
30 Ndipo Finehasi akasimama akafanya hukumu; Tauni ikazuiliwa.
Nombres 25.14-25.15 Josué 7.12 Nombres 25.6-25.8 Deutéronome 13.15-13.17 Jonas 1.12-1.15
31 Akahesabiwa kuwa ana haki Kizazi baada ya kizazi hata milele.
Nombres 25.11-25.13 Deutéronome 24.13 Genèse 15.6 Marc 14.3-14.9
32 Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao,
Psaumes 81.7 Deutéronome 1.37 Nombres 20.2-20.13 Nombres 20.23-20.24 Deutéronome 4.21
33 Kwa sababu waliiasi roho yake, Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.
Nombres 20.10-20.11 Psaumes 78.40 Job 2.10 Job 38.2 Jacques 3.2
34 Hawakuwaharibu watu wa nchi Kama Bwana alivyowaambia;
Juges 1.21 Deutéronome 7.16 Deutéronome 7.2 Josué 15.63 Nombres 33.52
35 Bali walijichanganya na mataifa, Wakajifunza matendo yao.
Juges 3.5-3.6 Juges 1.27-1.36 Juges 2.2-2.3 Esaïe 2.6 Josué 15.63
36 Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao.
Deutéronome 7.16 Exode 23.33 Juges 2.3 Exode 34.15-34.16 2 Rois 17.8-17.11
37 Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani.
2 Rois 16.3 Deutéronome 32.17 1 Corinthiens 10.20 2 Rois 17.17 Lévitique 17.7
38 Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; Nchi ikatiwa unajisi kwa damu.
Nombres 35.33 Jérémie 2.34 Esaïe 1.15 Esaïe 26.21 Deutéronome 21.9
39 Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao, Wakafanya uasherati kwa matendo yao.
Ezéchiel 20.18 Lévitique 17.7 Nombres 15.39 Osée 9.1 Ezéchiel 20.30-20.31
40 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya watu wake, Akauchukia urithi wake.
Juges 2.14 Deutéronome 9.29 Deutéronome 32.19 Psaumes 74.1 Juges 2.20
41 Akawatia mikononi mwa mataifa, Nao waliowachukia wakawatawala.
Juges 2.14 Deutéronome 28.25 Deutéronome 32.30 Juges 3.8 Juges 3.12
42 Adui zao wakawaonea, Wakatiishwa chini ya mkono wao.
Juges 10.12 Juges 4.3
43 Mara nyingi aliwaponya, Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao, Wakadhilika katika uovu wao.
Juges 2.16-2.18 Psaumes 81.12 1 Samuel 13.19 1 Samuel 12.9-12.11 Juges 6.5
44 Lakini aliyaangalia mateso yao, Aliposikia kilio chao.
Juges 3.9 Juges 4.3 Juges 6.6-6.10 Juges 2.18 Néhémie 9.27-9.38
45 Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;
Psaumes 105.8 Psaumes 69.16 Juges 2.18 Lamentations 3.32 Psaumes 51.1
46 Akawajalia kuhurumiwa Na watu wote waliowateka.
Esdras 9.9 Jérémie 42.12 1 Rois 8.50 Jérémie 15.11 Néhémie 1.11
47 Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe, Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, Tulishukuru jina lako takatifu, Tuzifanyie shangwe sifa zako.
2 Corinthiens 2.14 Apocalypse 7.10-7.12 Ezéchiel 36.24-36.28 Ezéchiel 37.21-37.28 1 Chroniques 16.35-16.36
48 Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, Tangu milele hata milele. Watu wote na waseme, Amina. Haleluya.
Psaumes 41.13 Psaumes 89.52 Psaumes 72.18-72.19 Psaumes 105.45-106.1 1 Chroniques 29.10

Cette Bible est dans le domaine public.