Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 41.12
Bible en Swahili de l’est


1 Je! Waweza wewe kumvua mamba kwa ndoana? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba?
Psaumes 74.14 Job 3.8 Psaumes 104.26 Esaïe 27.1
2 Je! Waweza kutia kamba puani mwake? Au kutoboa taya yake kwa kulabu?
Esaïe 37.29 Ezéchiel 29.4-29.5 Esaïe 27.1 2 Rois 19.28
3 Je! Atakusihi sana? Au, atakuambia maneno ya upole?
Proverbes 18.23 Esaïe 30.10 Proverbes 15.1 Proverbes 25.15 Psaumes 55.21
4 Je! Atafanya agano pamoja nawe, Umtwae kuwa mtumishi wako milele?
Exode 21.6 Deutéronome 15.17 Psaumes 8.5-8.6 Genèse 1.28 1 Rois 20.31-20.34
5 Je! Utamchezea kama ndege? Au, kumfunga kwa ajili ya wasichana wako?
Job 28.11 Juges 16.25-16.30
6 Je! Vikosi vya wavuvi watamfanyia biashara? Watamgawanya kati ya wafanyao biashara?
Juges 14.11
7 Je! Waweza kuijaza ngozi yake na vyuma vyenye ncha, Au kichwa chake kwa vyusa?
8 Mwekee mkono wako; Vikumbuke vile vita, wala usifanye tena.
1 Rois 20.11 Luc 14.31-14.32 2 Rois 10.4
9 Tazama, kumtamani ni bure; Je! Hatambwaga chini huyo atakayemtazama?
Esaïe 28.19 1 Samuel 3.11 Luc 21.11 Deutéronome 28.34
10 Hapana aliye mkali hata akathubutu kumwamsha; Bali ni nani awezaye kusimama mbele yangu mimi?
Job 9.4 Genèse 49.9 Job 3.8 Psaumes 2.11-2.12 Nombres 24.9
11 Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.
Psaumes 24.1 Romains 11.35 Deutéronome 10.14 Psaumes 50.12 Exode 19.5
12 Sitanyamaa kusema habari za via vyake, Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri.
Genèse 1.25
13 Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu?
Jacques 3.3 2 Rois 19.28 Psaumes 32.9
14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.
Job 38.10 Daniel 7.7 Psaumes 58.6 Proverbes 30.14 Psaumes 57.4
15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri.
Apocalypse 5.2-5.3 Apocalypse 5.5 Jérémie 9.23
16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati.
17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa.
18 Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka, Na macho yake yanafanana na makope ya alfajiri.
Job 3.9 Apocalypse 1.14
19 Mienge iwakayo hutoka kinywani mwake, Na macheche ya moto huruka nje.
Psaumes 18.8
20 Moshi hutoka katika mianzi ya pua yake, Kama nyungu ikitokota, na manyasi yawakayo.
Jérémie 1.13-1.14
21 Pumzi zake huwasha makaa, Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.
Psaumes 18.8 Habakuk 3.5 Psaumes 18.12 Esaïe 30.33
22 Katika shingo yake hukaa nguvu, Na utisho hucheza mbele yake.
Job 39.19 Osée 13.14 Job 40.16 1 Corinthiens 15.55-15.57
23 Manofu ya nyama yake hushikamana; Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.
24 Moyo wake una imara kama jiwe; Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.
Esaïe 48.4 Jérémie 5.3 Zacharie 7.12
25 Anapojiinua, mashujaa huogopa; Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.
Psaumes 107.28 Jonas 1.4-1.6
26 Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
Job 39.21-39.24
27 Yeye huona chuma kuwa kama nyasi, Na shaba kama mti uliooza.
28 Mshale hauwezi kumkimbiza; Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.
Job 39.7 Habakuk 1.10
29 Marungu huhesabiwa kama mabua; Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.
2 Chroniques 26.14
30 Pande zake za chini ni kama vigae vikali; Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.
Esaïe 41.15
31 Yeye huchemsha kilindi mfano wa nyungu; Hufanya bahari kuwa kama mafuta.
32 Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.
Job 38.16 Proverbes 20.29 Genèse 1.2 Genèse 42.38 Proverbes 16.31
33 Juu ya nchi hapana aliyefanana naye, Aliyeumbwa pasipo oga.
Job 40.19
34 Yeye hutazama kila kitu kilicho juu; Ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.
Job 28.8 Job 26.12 Esaïe 28.1 Ezéchiel 29.3 Psaumes 73.10

Cette Bible est dans le domaine public.