Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 9.35
Bible en Swahili de l’est


Premiers habitants de Jérusalem après l’exil

1 Hivyo Israeli wote walihesabiwa kwa nasaba; na tazama, hizo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli; na Yuda wakachukuliwa mateka mpaka Babeli, kwa sababu ya makosa yao.
2 Chroniques 36.9-36.10 Esdras 2.59 Esdras 2.62-2.63 1 Chroniques 5.25-5.26 Jérémie 39.9
2 Basi wenyeji wa kwanza waliokaa katika hozi zao katika miji yao walikuwa Israeli, na makuhani, na Walawi, na Wanethini.
Néhémie 7.73 Esdras 2.43 Esdras 8.20 Esdras 2.70 Esdras 2.58
3 Na huko Yerusalemu walikuwa wakikaa baadhi ya wana wa Yuda, na wana wa Benyamini, na wana wa Efraimu na Manase;
Néhémie 11.1 2 Chroniques 30.11 Néhémie 11.4-11.9 2 Chroniques 11.16
4 Uthai, mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imli, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Genèse 46.12 1 Chroniques 2.5 Nombres 26.20 Néhémie 11.6 Néhémie 8.7
5 Na wa Washiloni; Asaya, mzaliwa wa kwanza, na wanawe.
Nombres 26.20 Néhémie 11.5
6 Na wa wana wa Zera; Yeueli, na ndugu zao; watu mia sita na tisini.
1 Chroniques 2.4 1 Chroniques 2.6 Nombres 26.20 Genèse 38.30
7 Na wa wana wa Benyamini; Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Néhémie 11.7 Néhémie 10.20 Néhémie 8.4
8 na Ibneya, mwana wa Yerohamu; na Ela, mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu, mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya;
9 na ndugu zao, sawasawa na vizazi vyao; watu mia kenda na hamsini na sita. Watu hao wote ndio waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao, kwa kadiri ya mbari za baba zao.
Néhémie 11.8
10 Na katika makuhani; Yedaya, na Yehoyaribu, na Yakini;
Néhémie 12.19 Néhémie 11.10-11.24
11 na Azaria, mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu;
Néhémie 11.11 Nombres 4.15-4.16 1 Chroniques 6.8-6.15 Actes 5.24 1 Chroniques 24.5
12 na Adaya, mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; na Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yazera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri;
1 Chroniques 24.14 Néhémie 11.12-11.13 Néhémie 7.40 Esdras 2.37
13 wakuu wa mbari za baba zao; pamoja na ndugu zao; watu elfu na mia saba na sitini; watu wenye ustadi waliofaa sana kwa kazi ya huduma ya nyumba ya Mungu.
1 Chroniques 26.6 1 Chroniques 26.32 Néhémie 11.14 1 Chroniques 26.30
14 Na katika Walawi; Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari;
1 Chroniques 6.29 Néhémie 11.15-11.19 Nombres 26.57 Néhémie 12.24 1 Chroniques 6.19
15 na Bakbakari, na Hereshi, na Galali, na Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu;
Néhémie 11.22 1 Chroniques 12.25 1 Chroniques 12.35 Néhémie 10.12 1 Chroniques 25.2
16 na Obadia, mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni; na Berekia, mwana wa Asa, mwana wa Elkana; waliokaa katika vijiji vya Wanetofathi.
1 Chroniques 12.25 1 Chroniques 2.54 Néhémie 11.17 2 Chroniques 35.15 Néhémie 7.26
17 Na katika mabawabu; Shalumu, na Akubu, na Talmoni, na Ahimani, na ndugu zao; naye Shalumu alikuwa mkuu wao;
1 Chroniques 26.1-26.32 1 Chroniques 23.5 Néhémie 11.19
18 ambao tangu hapo walikuwa wakingojea penye lango la mfalme upande wa mashariki; hao ndio waliokuwa wangojezi wa rago la wana wa Lawi.
Ezéchiel 46.1-46.2 1 Rois 10.5 1 Chroniques 26.12-26.19 Ezéchiel 44.2-44.3 2 Rois 11.19
19 Naye Shalumu, mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora; pamoja na nduguze wa mbari ya babaye, Wakora; walikuwa wakiisimamia kazi hiyo ya huduma, wenye ungojezi wa malango ya maskani; na baba zao walikuwa wamesimamia matuo ya Bwana, wakiyalinda maingilio;
1 Chroniques 6.22-6.23 1 Chroniques 26.7-26.8 Nombres 26.9-26.11 1 Chroniques 26.13-26.19 Psaumes 49.1
20 naye Finehasi, mwana wa Eleazari, alikuwa mkuu wao hapo zamani, naye Bwana alikuwa pamoja naye.
Nombres 4.16 1 Samuel 16.18 Nombres 25.7-25.13 Nombres 3.32 Nombres 4.33
21 Zekaria, mwana wa Meshelemia, alikuwa bawabu mlangoni pa ile hema ya kukutania.
1 Chroniques 26.14 1 Chroniques 26.2
22 Hao wote waliochaguliwa kuwa wangojezi wa malango walikuwa watu mia mbili na kumi na wawili. Nao wakahesabiwa kwa nasaba katika vijiji vyao, ambao Daudi na Samweli, huyo mwonaji, walikuwa wamewaweka katika kazi yao waliyoamaniwa.
1 Samuel 9.9 1 Chroniques 9.25-9.26 2 Chroniques 31.18 1 Chroniques 28.21 Néhémie 12.44
23 Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu.
Néhémie 12.45 2 Chroniques 23.19 1 Chroniques 23.32 Ezéchiel 44.10-44.11 Ezéchiel 44.14
24 Hao wangojezi walikuwapo pande zote nne, kuelekea mashariki, na magharibi, na kaskazini, na kusini.
1 Chroniques 26.14-26.18
25 Na ndugu zao, katika vijiji vyao, wakaamaniwa kuingia kila siku ya saba, zamu kwa zamu, ili kuwa pamoja nao;
2 Rois 11.5 2 Chroniques 23.8 2 Rois 11.7
26 kwa maana wale wangojezi wanne, waliokuwa wakuu, nao ni Walawi, walikuwa na kazi ya kuamaniwa, tena walikuwa juu ya vyumba na juu ya hazina katika nyumba ya Mungu.
1 Chroniques 26.20-26.27 2 Chroniques 31.5-31.12 Néhémie 13.5 Néhémie 10.38-10.39
27 Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.
1 Chroniques 23.30-23.32 Malachie 1.10 Romains 12.7 1 Samuel 3.15
28 Na baadhi yao walikuwa na ulinzi wa vyombo vya huduma; kwani huingizwa kwa hesabu, na kutolewa kwa hesabu vile vile.
Nombres 23.25-23.27 Néhémie 13.4-13.5 Esdras 8.25-8.30 1 Chroniques 26.22-26.26 Néhémie 12.44
29 Na baadhi yao waliamaniwa kuviangalia vyombo vya nyumbani, na vyombo vyote vya Patakatifu; na kuwa juu ya unga safi, na divai, na mafuta, na ubani, na manukato.
1 Chroniques 23.29 Exode 30.23-30.38 Exode 27.20
30 Na baadhi ya wana wa makuhani waliweka tayari machanganyiko ya manukato.
Exode 30.23-30.25 Exode 37.29 Exode 30.33 Exode 30.35-30.38
31 Naye Matithia, Mlawi mmojawapo, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, Mkora, aliamaniwa kazi ya kuviangalia vitu vile vilivyookwa kaangoni.
1 Chroniques 9.19 1 Chroniques 9.22 1 Chroniques 9.17 1 Chroniques 9.26 Lévitique 2.5
32 Na baadhi ya ndugu zao, wa wana wa Wakohathi, walikuwa juu ya mikate ile ya Wonyesho, ili kuiandaa kila sabato.
Lévitique 24.5-24.8 1 Chroniques 6.33-6.48 Exode 25.30
33 Tena hawa ndio waimbaji, wakuu wa mbari za baba zao katika Walawi, ambao walikaa vyumbani, kisha walikuwa hawana kazi nyingine; kwa kuwa walitumika katika kazi yao mchana na usiku.
1 Chroniques 6.31-6.33 1 Chroniques 25.1-25.31 1 Chroniques 15.16-15.22 Psaumes 134.1-134.2 Néhémie 11.22-11.23
34 Hao walikuwa wakuu wa mbari za baba zao katika Walawi, katika vizazi vyao vyote, watu wakuu; nao walikuwa wakikaa huko Yerusalemu.
1 Chroniques 9.13 Néhémie 11.1-11.15

Généalogie de Saül et de Jonathan

35 Basi huko Gibea alikaa babaye Gibea, jina lake Yeieli, na jina la mkewe aliitwa Maaka;
1 Chroniques 2.23-2.24 1 Chroniques 2.50-2.52 1 Chroniques 8.29-8.40 1 Chroniques 2.45
36 na mwanawe, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa Abdoni; na Suri, na Kishi, na Baali, na Meri, na Nadabu;
1 Chroniques 9.39 1 Chroniques 8.33
37 na Gedori, na Ahio, na Zekaria, na Miklothi.
1 Chroniques 8.31
38 Na Miklothi akamzaa Shimea. Hao nao walikuwa wakikaa pamoja na ndugu zao huko Yerusalemu, kuwakabili ndugu zao.
1 Chroniques 8.32
39 Naye Neri akamzaa Kishi; na Kishi akamzaa Sauli; na Sauli akamzaa Yonathani, na Malkishua, na Abinadabu, na Eshbaali.
1 Samuel 13.22 1 Samuel 14.1 1 Chroniques 10.2 1 Samuel 14.49-14.51 1 Chroniques 8.33-8.38
40 Na mwana wa Yonathani alikuwa Meribaali; na Meribaali akamzaa Mika.
2 Samuel 4.4 1 Chroniques 8.34-8.36
41 Na wana wa Mika; Pithoni, na Meleki, na Tarea.
1 Chroniques 8.35
42 Na Ahazi akamzaa Yara; na Yara akamzaa Alemethi, na Azmawethi, na Zimri; na Zimri akamzaa Mosa;
1 Chroniques 8.36
43 na Mosa akamzaa Binea; na mwanawe huyo alikuwa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli;
1 Chroniques 8.37
44 naye Aseli alikuwa na wana sita, ambao majina yao ni haya; Azrikamu, na Bokeru, na Ishmaeli, na Shearia, na Obadia, na Hanani. Hao wote walikuwa wana wa Aseli

Cette Bible est dans le domaine public.