Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 9.6
Bible en Swahili de l’est


Nouvelle apparition de Dieu à Salomon

1 Ikawa Sulemani alipokwisha kuijenga nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme, na mambo yote yaliyoingia moyoni mwake Sulemani, naye akataka kuyafanya,
1 Rois 9.19 1 Rois 6.37-7.1 2 Chroniques 7.11-8.6 Ecclésiaste 6.9 Ecclésiaste 2.10
2 basi, Bwana akamtokea Sulemani mara ya pili kama alivyomtokea huko Gibeoni.
1 Rois 3.5 1 Rois 11.9 2 Chroniques 7.12 2 Chroniques 1.7-1.12
3 Bwana akamwambia, Nimeyasikia maombi yako na dua zako, ulizotoa mbele zangu. Nimeitakasa nyumba hii uliyoijenga ili niweke jina langu humo milele; tena macho yangu na moyo wangu utakuwapo hapo siku zote;
1 Rois 8.29 Deutéronome 11.12 2 Rois 20.5 Psaumes 10.17 2 Chroniques 6.40
4 na wewe, ukienda mbele zangu kama alivyokwenda Daudi, baba yako, kwa ukamilifu wa moyo, na kwa adili, kufanya hayo yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu,
1 Rois 11.6 1 Rois 15.5 Genèse 17.1 1 Rois 11.4 1 Rois 14.8
5 ndipo nitakapokifanya imara kiti cha ufalme wako juu ya Israeli milele; kama nilivyomwahidia Daudi, baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kukaa katika kiti cha enzi cha Israeli.
1 Rois 2.4 1 Rois 6.12 2 Samuel 7.12 2 Samuel 7.16 1 Chroniques 22.9-22.10
6 Bali mkighairi, mkaacha kunifuata, ninyi na watoto wenu, msizishike sheria zangu na amri zangu, nilizoziweka mbele yenu, tena mkienda na kuitumikia miungu mingine na kuiabudu,
2 Samuel 7.14-7.16 1 Chroniques 28.9 1 Samuel 2.30 2 Chroniques 15.2 Psaumes 89.30
7 basi nitawakatilia Israeli mbali na nchi hii niliyowapa; na nyumba hii niliyoitakasa kwa jina langu, nitaitupilia mbali na macho yangu, na Israeli watakuwa mithali na neno la tusi katika mataifa yote.
Jérémie 24.9 Psaumes 44.14 Deutéronome 4.26 Deutéronome 28.37 2 Rois 25.21
8 Na ijapokuwa nyumba hii imetukuka namna hii, lakini kila apitaye atasituka na kuizomea; nao watasema, Kwa nini Bwana ameitenda nchi hii na nyumba hii mambo haya?
Jérémie 22.8-22.9 Deutéronome 29.24-29.26 2 Chroniques 7.21 Jérémie 22.28 Jérémie 19.8
9 Na watu watajibu, Kwa sababu walimwacha Bwana, Mungu wao, aliyewatoa baba zao katika nchi ya Misri, wakashikamana na miungu mingine na kuiabudu na kuitumikia, basi ndiyo sababu Bwana ameleta mabaya haya yote juu yao.
Jérémie 2.10-2.13 Deutéronome 29.25-29.28 Jérémie 2.19 Jérémie 12.7-12.8 Jérémie 50.7

Travaux de construction de Salomon

10 Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani alizijenga zile nyumba mbili, nyumba ya Bwana na nyumba yake mfalme,
1 Rois 6.37-7.1 1 Rois 9.1 2 Chroniques 8.1-8.18
11 (basi Hiramu, mfalme wa Tiro, alikuwa amemletea Sulemani mierezi na miberoshi, na dhahabu, sawasawa na haja zake zote), ndipo mfalme Sulemani akampa Hiramu miji ishirini ya nchi ya Galilaya.
2 Chroniques 8.2 2 Chroniques 2.8-2.10 Josué 20.7 2 Chroniques 2.16 1 Rois 5.6-5.10
12 Naye Hiramu akatoka Tiro kuitazama hiyo miji Sulemani aliyompa; wala haikumpendeza.
Nombres 22.34 Juges 14.3
13 Akasema, Miji gani hii uliyonipa, ndugu yangu? Akaiita nchi ya Kabuli, hata leo.
Josué 19.27 1 Rois 5.1-5.2 Amos 1.9
14 Hiramu akamletea mfalme talanta sitini za dhahabu.
1 Rois 9.11 1 Rois 10.21 1 Rois 10.10 1 Rois 10.14 1 Rois 9.28
15 Na hii ndiyo sababu ya shokoa aliyoitoza mfalme Sulemani; ili kuijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake mwenyewe, na Milo, na ukuta wa Yerusalemu, na Hazori, na Megido, na Gezeri.
1 Rois 5.13 2 Samuel 5.9 1 Rois 9.24 Josué 17.11 Josué 11.1
16 Farao, mfalme wa Misri, alikuwa amepanda akautwaa Gezeri, na kuuteketeza kwa moto, akawaua Wakanaani waliokaa mjini, akampa zawadi binti yake, mkewe Sulemani.
1 Rois 3.1 1 Rois 9.24 1 Rois 7.8 Josué 16.10
17 Naye Sulemani akaujenga Gezeri, na Beth-horoni wa chini,
Josué 16.3 Josué 21.22 Josué 19.44 Josué 10.10 2 Chroniques 8.4-8.18
18 na Baalathi, na Tamari ulio nyikani, katika nchi;
Josué 19.44 2 Chroniques 8.4
19 na miji yote ya hazina iliyokuwa yake Sulemani; na miji ya magari yake, na miji ya watu wake wapandao farasi, na kila alichopenda kujenga Sulemani huko Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote ya mamlaka yake.
1 Rois 9.1 1 Rois 4.26-4.28 1 Rois 10.26 Ecclésiaste 6.9 Ecclésiaste 2.10
20 Kwa habari ya watu wote waliosalia, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi, wasiokuwa wa wana wa Israeli;
Deutéronome 7.1-7.3 Exode 34.11-34.12 Exode 23.28-23.33 2 Chroniques 8.7-8.18 Genèse 15.19-15.21
21 watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuweza kuwaharibu kabisa, katika hao Sulemani akawatumikisha shokoa hata leo.
Josué 17.12 Josué 15.63 Juges 1.21 Genèse 9.25-9.26 Esdras 2.55-2.58
22 Lakini wa wana wa Israeli Sulemani hakumtumikisha mtu shokoa; ila ndio watu wa vita, na wangoje wake, na wakuu wake, na akida zake, na wakuu, wa magari yake, na wa wapanda farasi wake.
Lévitique 25.39 1 Samuel 8.11-8.12 1 Rois 4.1-4.27 2 Chroniques 8.9-8.10
23 Hao maakida wakuu, waliokuwa juu ya kazi yake Sulemani, walikuwa mia tano na hamsini, waliowaamuru watu watendao kazi.
1 Rois 5.16 2 Chroniques 8.10 2 Chroniques 2.18
24 Lakini binti Farao akapanda toka mji wa Daudi, mpaka hiyo nyumba yake Sulemani, aliyomjengea; kisha, aliijenga Milo.
1 Rois 11.27 2 Samuel 5.9 2 Chroniques 32.5 1 Rois 7.8 1 Rois 3.1
25 Na mara tatu kila mwaka Sulemani alikuwa akitoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu aliyomjengea Bwana akafukiza uvumba pamoja nazo juu ya madhabahu iliyokuwako mbele za Bwana. Hivyo akaimaliza nyumba.
Deutéronome 16.16 2 Chroniques 8.16 2 Chroniques 8.12-8.13 Exode 23.14-23.17 1 Chroniques 23.13
26 Tena, mfalme Sulemani akaunda merikebu huko Ezion-geberi, ulioko karibu na Elothi, pwani ya Bahari ya Shamu, katika nchi ya Edomu.
1 Rois 22.48 Nombres 33.35 Deutéronome 2.8 2 Chroniques 8.17-8.18 2 Chroniques 8.11-8.12
27 Naye Hiramu akatuma merikebuni watumishi wake, wanamaji wenye kuijua bahari, pamoja na watumishi wake Sulemani.
1 Rois 10.11 1 Rois 5.6 1 Rois 5.9 2 Chroniques 20.36-20.37 1 Rois 22.49
28 Wakafika Ofiri, wakachukua toka huko dhahabu, talanta mia nne na ishirini, wakamletea mfalme Sulemani.
1 Chroniques 29.4 2 Chroniques 8.18 Esaïe 13.12 Job 22.24 Job 28.16

Cette Bible est dans le domaine public.