Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 6.8
Bible en Swahili de l’est


Transport de l’arche jusqu’à Jérusalem

1 Basi Daudi akakusanya tena wateule wote wa Israeli, watu thelathini elfu.
1 Chroniques 13.1-13.4 1 Chroniques 13.6-13.14 2 Samuel 5.1 1 Rois 8.1 Psaumes 132.1-132.6
2 Akaondoka Daudi akaenda pamoja na watu wote waliokuwa naye, mpaka Baala wa Yuda, ili kulipandisha kutoka huko sanduku la Mungu lililoitwa kwa jina, naam, jina la Bwana wa majeshi akaaye juu ya makerubi.
1 Samuel 7.1 1 Samuel 4.4 Psaumes 80.1 1 Chroniques 13.5-13.6 Josué 15.9-15.10
3 Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya gari jipya, wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyoko kilimani; nao Uza na Ahio wana wa Abinadabu wakaliendesha lile gari jipya.
1 Samuel 6.7 Nombres 7.4-7.9 Nombres 4.5-4.12
4 Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu iliyoko kilimani, pamoja na sanduku la Bwana; na huyo Ahio akatangulia mbele ya sanduku.
1 Chroniques 13.7 1 Samuel 7.1-7.2
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli wakacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa kayamba, na kwa matoazi.
1 Chroniques 13.8 Psaumes 150.3-150.5 1 Samuel 18.6-18.7 Daniel 3.15 Daniel 3.5
6 Hata walipofika kwa uga ya Nakoni, Uza akalinyoshea mkono sanduku la Mungu, akalikamata kwa maana wale ng’ombe walikunguwaa.
1 Chroniques 13.9 Nombres 4.15 Nombres 4.19-4.20
7 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Uza; naye Mungu akampiga huko kwa kosa lake; hata akafa pale pale penye sanduku la Mungu.
1 Samuel 6.19 1 Chroniques 15.13 1 Corinthiens 11.30-11.32 Lévitique 10.1-10.3 1 Chroniques 15.2
8 Daudi akaona uchungu kwa kuwa Bwana amemfurikia Uza; akapaita mahali pale Peres-uza hata leo.
1 Chroniques 13.11-13.12 Jonas 4.9 Jonas 4.1
9 Naye Daudi akamwogopa Bwana siku ile; akasema, Litanijiaje sanduku la Bwana?
Psaumes 119.120 1 Chroniques 13.11-13.12 1 Pierre 3.6 Luc 5.8-5.9 1 Samuel 5.10-5.11
10 Basi Daudi hakutaka kulileta sanduku la Bwana kwake mjini mwa Daudi; ila Daudi akalihamisha nyumbani kwa Obed-edomu, Mgiti.
1 Chroniques 26.4-26.8 1 Chroniques 15.18 2 Samuel 4.3 2 Samuel 18.2 2 Samuel 15.19
11 Sanduku la Bwana akalitia katika nyumba ya Obed-edomu, Mgiti, muda wa miezi mitatu; naye Bwana akambarikia Obed-edomu, na nyumba yake yote.
Genèse 30.27 Genèse 39.5 Malachie 3.10 Proverbes 3.9-3.10 Genèse 39.23
12 Kisha mfalme Daudi akaambiwa ya kwamba, Bwana ameibarikia nyumba ya Obed-edomu, na vitu vyote alivyo navyo kwa ajili ya sanduku la Mungu. Daudi akaenda, akalileta sanduku la Mungu, toka nyumba ya Obed-edomu mpaka mji wa Daudi, kwa shangwe.
1 Rois 8.1 Matthieu 10.42 Psaumes 132.6-132.8 Psaumes 24.7-24.10 1 Chroniques 15.25-16.3
13 Hata ikawa, watu waliolichukua sanduku la Bwana walipokwisha kwenda hatua sita, akachinja ng’ombe na kinono.
1 Rois 8.5 Nombres 4.15 1 Chroniques 15.2 Josué 3.3 1 Chroniques 15.15
14 Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.
1 Samuel 2.18 Psaumes 150.4 Exode 15.20 Psaumes 149.3 Psaumes 30.11
15 Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la Bwana kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.
1 Chroniques 15.25 Nombres 10.1-10.10 Esdras 3.10-3.11 Psaumes 68.24-68.27 Psaumes 132.18
16 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.
1 Chroniques 15.29 2 Samuel 3.14 Esaïe 53.3 Psaumes 69.7 1 Corinthiens 2.14
17 Wakaliingiza sanduku la Bwana, na kuliweka mahali pake, katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
1 Chroniques 15.1 2 Chroniques 1.4 Psaumes 132.8 1 Rois 8.5 1 Rois 8.62-8.65
18 Kisha Daudi alipokwisha kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani akawabarikia watu kwa jina la Bwana wa majeshi.
1 Rois 8.55 Genèse 14.19 2 Chroniques 6.3 Lévitique 9.22-9.23 2 Chroniques 30.18-30.19
19 Akawagawia watu wote, mkutano wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu. Basi watu wote wakaenda zao, kila mtu nyumbani kwake.
Néhémie 8.10 1 Chroniques 16.3 2 Chroniques 35.7-35.8 1 Rois 8.66 Actes 20.35
20 Ndipo Daudi akarudi ili awabarikie watu wa nyumbani mwake. Na Mikali, binti Sauli, akatoka nje aende kumlaki Daudi, naye akasema, Mfalme wa Israeli alikuwa mtukufu leo namna gani, akijifunua mwili wake mbele ya vijakazi vya watumishi wake, mfano wa watu baradhuli mmojawapo, ajifunuavyo mwili wake mbele ya watu, asipokuwa na haya!
2 Samuel 6.16 2 Samuel 6.14 Juges 9.4 Psaumes 101.2 Josué 24.15
21 Daudi akamwambia Mikali, Ilikuwa mbele za Bwana, aliyenichagua mimi juu ya baba yako, na juu ya nyumba yake, ili kuniweka niwe mkuu juu ya watu wa Bwana, juu ya Israeli; kwa hiyo mimi nitacheza mbele za Bwana.
1 Samuel 13.14 1 Samuel 15.28 2 Samuel 6.5 1 Corinthiens 10.31 2 Samuel 6.14
22 Kisha nitakuwa hafifu zaidi, nami nitakuwa mnyonge machoni pangu mimi mwenyewe; lakini kwa wale vijakazi uliowanena, kwao nitaheshimiwa.
1 Pierre 4.14 Job 42.6 Actes 5.41-5.42 1 Timothée 1.15 Hébreux 12.2
23 Basi Mikali, binti Sauli, hakuwa na mtoto hata siku ya kufa kwake.
Matthieu 1.25 Esaïe 22.14 Luc 1.25 1 Samuel 15.35 Esaïe 4.1

Cette Bible est dans le domaine public.