Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 24.25
Bible en Swahili de l’est


Recensement et peste

1 Tena hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, akamtia Daudi nia juu yao, akisema, Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda.
1 Chroniques 21.1 1 Chroniques 27.23-27.24 Ezéchiel 14.9 2 Samuel 16.10 2 Thessaloniciens 2.11
2 Basi mfalme akamwambia Yoabu, jemadari wa jeshi la askari, waliokuwa pamoja naye, Zunguka sasa katikati ya kabila zote za Israeli, tangu Dani mpaka Beer-sheba, mkawahesabu watu, nipate kujua jumla ya hao watu.
2 Samuel 3.10 Juges 20.1 2 Samuel 20.23 2 Corinthiens 12.7 2 Samuel 23.37
3 Naye Yoabu akamwambia mfalme, Bwana, Mungu wako, na awaongeze watu, hesabu yao ikiwa yo yote, mara mia, tena macho ya bwana wangu mfalme na yawaone; ila kwa nini neno hili limempendeza bwana wangu mfalme?
Psaumes 115.14 Deutéronome 1.11 1 Chroniques 21.3-21.4 Esaïe 60.5 Proverbes 14.28
4 Lakini neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu, na juu ya majemadari wa jeshi. Basi Yoabu akatoka na majemadari wa jeshi machoni pa mfalme, kwenda kuwahesabu watu wa Israeli.
Ecclésiaste 8.4 Exode 1.17 Actes 5.29 1 Chroniques 21.4
5 Wakavuka Yordani, wakapiga kambi huko Aroeri, upande wa kuume wa mji ulioko kati ya bonde la Gadi, na mpaka Yazeri;
Deutéronome 2.36 Josué 13.9 Josué 13.16 Nombres 32.3 Nombres 32.1
6 kisha wakaja Gileadi, na nchi ya Wahiti huko Kadeshi; kisha wakaja Dani, na kutoka Dani wakazunguka mpaka Sidoni,
Josué 19.28 Juges 18.28-18.29 Genèse 31.47-31.48 Nombres 32.1 Juges 1.31
7 wakaja ngomeni kwa Tiro, na kwa miji yote ya Wahivi, na ya Wakanaani; tena wakatoka kusini kwa Yuda huko Beer-sheba.
Josué 19.29 Josué 11.3 Juges 3.3 Genèse 21.22-21.33 2 Samuel 24.2
8 Nao walipokwisha kuzunguka nchi yote, wakaja Yerusalemu mwisho wa miezi kenda na siku ishirini.
9 Naye Yoabu akamtolea mfalme jumla ya hesabu ya watu; nao walikuwa wa Israeli mashujaa wenye kufuta panga mia nane elfu; nao wa Yuda walikuwa watu mia tano elfu.
1 Chroniques 27.23-27.24 Nombres 1.44-1.46 1 Chroniques 21.5-21.6
10 Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia Bwana, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee Bwana, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.
2 Samuel 12.13 1 Samuel 13.13 1 Samuel 24.5 2 Chroniques 16.9 Proverbes 28.13
11 Na Daudi alipoondoka asubuhi, neno la Bwana likamjia nabii Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema,
1 Samuel 9.9 1 Samuel 22.5 1 Chroniques 29.29 1 Chroniques 2.19
12 Nenda, ukanene na Daudi, Bwana asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya uchague moja, nikutendee hilo.
2 Samuel 12.14 Hébreux 12.6-12.10 1 Chroniques 21.10-21.11 Lévitique 26.43 Proverbes 3.12
13 Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, miaka saba ya njaa ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma.
1 Chroniques 21.12 Lévitique 26.25 Deutéronome 28.27 Ezéchiel 14.13 2 Samuel 21.1
14 Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na tuanguke katika mkono wa Bwana; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.
Psaumes 51.1 Psaumes 119.156 Jean 12.27 2 Chroniques 28.5-28.9 Psaumes 145.9
15 Basi Bwana akawaletea Israeli tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu toka Dani mpaka Beer-sheba sabini elfu.
1 Chroniques 21.14 1 Chroniques 27.24 Matthieu 24.7 Nombres 16.46-16.49 Esaïe 37.36
16 Lakini huyo malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili auharibu, Bwana akaghairi katika mabaya, akamwambia huyo malaika mwenye kuwaharibu watu, Yatosha, sasa ulegeze mkono wako. Naye yule malaika wa Bwana alikuwako karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.
Actes 12.23 1 Samuel 15.11 Joël 2.13-2.14 Genèse 6.6 Exode 12.23
17 Daudi, alipomwoma malaika aliyewapiga watu, akanena na Bwana, akasema, Tazama, ni mimi niliyekosa, ni mimi niliyepotoka; lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Mkono wako na uwe juu yangu, na juu ya nyumba ya baba yangu.
Psaumes 74.1 1 Chroniques 21.16-21.17 2 Samuel 24.10 Esaïe 6.5 Job 42.6
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi, akamwambia, Haya! Kwea wewe, ukamwinulie Bwana madhabahu penye kiwanja cha Arauna, Myebusi.
1 Chroniques 21.18-21.30 2 Samuel 24.11
19 Basi Daudi akakwea sawasawa na neno la Gadi, kama Bwana alivyoamuru.
1 Chroniques 21.19 2 Chroniques 36.16 Genèse 6.22 Hébreux 11.8 Néhémie 9.26
20 Huyo Arauna akatazama, akamwona mfalme na watumishi wake wakimjia; Arauna akatoka, akasujudu mbele ya mfalme kifulifuli hata nchi.
Genèse 18.2 1 Chroniques 21.20-21.21 Ruth 2.10 2 Samuel 9.8
21 Arauna akasema, Bwana wangu mfalme amemjia mtumwa wake kwa kusudi gani? Naye Daudi akasema, Makusudi ninunue kwako kiwanja hiki, ili nimjengee Bwana madhabahu, ili kwamba tauni ipate kuzuiliwa katika watu.
Psaumes 106.30 2 Samuel 24.18 Jérémie 32.6-32.14 2 Samuel 24.3 Nombres 16.44-16.50
22 Arauna akamwambia Daudi, Bwana wangu mfalme na akitwae, akatolee yaliyo mema machoni pake; tazama, ng’ombe hawa kwa sadaka ya kuteketezwa, tena vyombo vya kupuria, na vyombo vya ng’ombe, viko kwa kuni,
1 Rois 19.21 1 Samuel 6.14 Genèse 23.11 1 Chroniques 21.22
23 vitu hivi vyote, Ee mfalme, mimi Arauna nakupa wewe mfalme. Kisha Arauna akamwambia mfalme, Bwana, Mungu wako, na akukubali.
Ezéchiel 20.40-20.41 1 Pierre 2.5 Psaumes 45.16 Psaumes 20.3-20.4 1 Timothée 2.1-2.2
24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha.
1 Chroniques 21.24-21.25 Romains 12.17 1 Chroniques 22.1 Genèse 23.13 Malachie 1.12-1.14
25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.
2 Samuel 21.14 1 Samuel 7.17 Genèse 8.20 Lamentations 3.32-3.33 1 Samuel 7.9

Cette Bible est dans le domaine public.