Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 26.6
Bible en Swahili de l’est


Isaac à Guérar

1 Ikawa njaa katika nchi hiyo, mbali na njaa ile ya kwanza iliyokuwa siku za Ibrahimu. Isaka akamwendea Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, huko Gerari.
Genèse 12.10 Genèse 25.11 Genèse 21.22-21.32 Genèse 20.1-20.2
2 Bwana akamtokea, akasema, Usishuke kwenda Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia.
Genèse 12.7 Genèse 12.1 Genèse 18.1 Genèse 17.1 Psaumes 37.3
3 Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako.
Genèse 28.15 Genèse 13.15 Genèse 15.18 Genèse 12.7 Genèse 20.1
4 Nitazidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, nami nitawapa uzao wako nchi hizi zote, na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.
Genèse 15.5 Genèse 22.17-22.18 Galates 3.8 Actes 3.25 Exode 32.13
5 Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu.
Genèse 22.16 Genèse 22.18 Galates 5.6 1 Corinthiens 15.58 Jacques 2.21
6 Isaka akakaa katika Gerari.
Genèse 20.1
7 Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso.
Genèse 12.13 Genèse 20.2 Proverbes 29.25 Genèse 24.16 Genèse 20.12-20.13
8 Ikawa alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia dirishani, akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe.
Juges 5.28 Proverbes 5.18-5.19 Proverbes 7.6 Ecclésiaste 9.9 Cantique 2.9
9 Abimeleki akamwita Isaka, akasema, Yakini huyu ni mkeo, mbona ulisema, Ni ndugu yangu huyu? Isaka akamwambia, Kwa sababu nalisema, Nisife kwa ajili yake.
10 Abimeleki akasema, Ni nini hii uliyotutendea? Labda mtu mmojawapo angalilala na mkeo bila kufikiri, nawe ungalitutia hatiani.
Genèse 12.18-12.19 Genèse 20.9-20.10
11 Basi Abimeleki akawaamuru watu wote, akisema, Amgusaye mtu huyu au mkewe lazima atauawa.
Psaumes 105.15 Genèse 20.6 Proverbes 6.29 Zacharie 2.8
12 Isaka akapanda mbegu katika nchi ile, akapata mwaka ule vipimo mia kwa kimoja, Bwana akambariki.
Genèse 24.1 Genèse 26.3 Job 42.12 Genèse 24.35 Zacharie 8.12
13 Na mtu huyu akawa mkuu, akazidi kusitawi, hata akawa mkuu sana.
Proverbes 10.22 Psaumes 112.3 Genèse 24.35
14 Akawa na mali ya kondoo, na mali ya ng’ombe, na watumwa wengi. Hao Wafilisti wakamhusudu.
Ecclésiaste 4.4 Genèse 37.11 Psaumes 112.10 Psaumes 144.13-144.14 Psaumes 112.3
15 Na vile visima vyote walivyochimba watumwa wa baba yake, siku za Ibrahimu babaye, Wafilisti walikuwa wamevifukia, wakavijaza kifusi.
Genèse 21.30 Genèse 21.25
16 Abimeleki akamwambia Isaka, Utoke kwetu, maana wewe una nguvu sana kuliko sisi.
Exode 1.9
17 Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari, akakaa huko.
18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.
Genèse 21.31 Zacharie 13.2 Osée 2.17 Nombres 32.38 Psaumes 16.4
19 Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.
Jean 4.10-4.11 Jean 7.38 Cantique 4.15
20 Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
Genèse 21.25
21 Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna.
Esdras 4.6
22 Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
Genèse 17.6 Exode 1.7 Psaumes 4.1 Genèse 28.3 Psaumes 18.19
23 Akapanda kutoka hapo mpaka Beer-sheba.
Genèse 21.31 Juges 20.1 Genèse 46.1
24 Bwana akamtokea usiku uleule, akasema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu baba yako, usiogope, maana mimi ni pamoja nawe, nami nitakubarikia, na kuzidisha uzao wako kwa ajili ya Ibrahimu mtumishi wangu.
Genèse 24.12 Exode 3.6 Genèse 17.7 Genèse 15.1 Apocalypse 1.17
25 Akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema yake huko, na watumwa wa Isaka wakachimba kisima huko.
Genèse 13.18 Psaumes 116.17 Genèse 12.7-12.8 Genèse 13.4 Genèse 8.20
26 Ndipo Abimeleki akamwendea kutoka Gerari, pamoja na Ahuzathi rafiki yake, na Fikoli, jemadari wa jeshi lake.
Genèse 20.3 Genèse 21.22-21.32
27 Isaka akawauliza, Mbona mwanijia, nanyi mmenichukia, mkanifukuza kwenu?
Genèse 26.16 Juges 11.7 Genèse 26.14 Actes 7.9 Actes 7.27
28 Wakasema, Hakika tuliona ya kwamba Bwana alikuwa pamoja nawe; nasi tukasema, Na tuapiane, sisi na wewe, na kufanya mapatano nawe
Genèse 21.22-21.23 Genèse 21.31-21.32 Esaïe 45.14 Hébreux 13.5 Genèse 31.49-31.53
29 ya kuwa hutatutenda mabaya, iwapo sisi hatukukugusa wewe, wala hatukukutendea ila mema, tukakuacha uende zako kwa amani; nawe sasa u mbarikiwa wa Bwana.
Genèse 24.31 Psaumes 115.15 Genèse 12.2 Genèse 26.11-26.12 Genèse 21.22
30 Basi akawafanyia karamu, nao wakala, wakanywa.
Genèse 19.3 1 Pierre 4.9 Romains 12.18 Genèse 21.8 Genèse 31.54
31 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakaapiana wao kwa wao, kisha Isaka akawapa ruhusa, nao wakaenda zao kwa amani.
Genèse 21.31-21.32 Genèse 22.3 1 Samuel 30.15 Genèse 14.22 Genèse 31.55
32 Ikawa siku ileile, watumwa wa Isaka wakaja wakampasha habari za kile kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, Tumeona maji.
Proverbes 2.4-2.5 Proverbes 10.4 Proverbes 13.4 Genèse 26.25 Matthieu 7.7
33 Naye akakiita jina lake Shiba; kwa hiyo jina la mji huo ni Beer-sheba, hata leo.
Genèse 21.31 Genèse 26.28
34 Esau alipokuwa mwenye miaka arobaini, akamwoa Yudithi, binti Beeri, Mhiti, na Basemathi, binti Eloni, Mhiti.
Genèse 36.2 Genèse 24.3 Genèse 28.9 1 Corinthiens 7.2 Hébreux 12.16
35 Roho zao Isaka na Rebeka zikajaa uchungu kwa ajili yao.
Genèse 27.46-28.2 Genèse 28.8 Genèse 6.2

Cette Bible est dans le domaine public.