Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 19.4
Bible en Swahili de l’est


Destruction de Sodome et de Gomorrhe

1 Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi.
Genèse 18.22 Genèse 18.1-18.5 Job 31.32 Hébreux 13.2
2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha.
Genèse 18.4 Hébreux 13.2 Luc 24.28-24.29 Actes 16.15 Juges 19.17-19.21
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala.
Genèse 18.6-18.8 Juges 6.19 1 Corinthiens 5.8 1 Samuel 28.24 Genèse 21.8
4 Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote.
Genèse 13.13 Genèse 18.20 Exode 23.2 Proverbes 4.16 Romains 3.15
5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua.
Juges 19.22 Esaïe 3.9 Romains 1.26-1.27 Lévitique 18.22 Jude 1.7
6 Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake.
Juges 19.23
7 Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi.
Juges 19.23 1 Samuel 30.23-30.24 1 Corinthiens 6.9-6.11 Actes 17.26 Lévitique 18.22
8 Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu.
Juges 19.24 Genèse 19.31-19.38 Marc 9.6 Juges 9.15 Romains 3.8
9 Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango.
Exode 2.14 Genèse 13.12 Proverbes 9.7-9.8 Ecclésiaste 10.13 Matthieu 7.6
10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango.
11 Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango.
2 Rois 6.18 Actes 13.11 Deutéronome 28.28-28.29 Jérémie 2.36 Ecclésiaste 10.15
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa;
2 Pierre 2.7 Apocalypse 18.4 Genèse 7.1 Genèse 19.22 2 Pierre 2.9
13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu.
Genèse 18.20 Psaumes 11.5-11.6 Esaïe 37.36 Apocalypse 16.1-16.12 Ezéchiel 9.5-9.6
14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. Lakini akawa kama achezaye machoni pa wakweze.
Nombres 16.21 Nombres 16.45 Exode 9.21 Jérémie 51.6 Nombres 16.26
15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu.
Nombres 16.24-16.27 2 Corinthiens 6.2 Apocalypse 18.4 Proverbes 6.4-6.5 Genèse 19.22
16 Akakawia-kawia; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana alivyomhurumia, wakamtoa wakamweka nje ya mji.
Psaumes 86.15 Michée 7.18-7.19 Romains 9.18 Psaumes 111.4 Romains 9.15-9.16
17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.
Genèse 19.26 Matthieu 24.16-24.18 Luc 9.62 Philippiens 3.13-3.14 Genèse 19.22
18 Lutu akawaambia, Sivyo, bwana wangu!
2 Rois 5.11-5.12 Jean 13.6-13.8 Genèse 32.26 Esaïe 45.11 Actes 10.14
19 Tazama, mtumwa wako ameona kibali machoni pako, nawe umezidisha rehema zako ulizonifanyia kwa kuponya nafsi yangu, nami siwezi kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa.
1 Rois 9.9 Genèse 12.13 Marc 9.19 Psaumes 77.7-77.11 Psaumes 116.1-116.19
20 Basi mji huu u karibu, niukimbilie, nao ni mdogo, nijiponye sasa huko, sio mdogo huu? Na nafsi yangu itaishi.
Proverbes 3.5-3.7 Psaumes 119.175 Genèse 19.30 Genèse 12.13 Amos 3.6
21 Akamwambia, Tazama, nimekukubali hata kwa neno hili, kwamba sitauangamiza mji huo uliounena.
Psaumes 34.15 Jérémie 14.10 Psaumes 102.17 Genèse 12.2 Genèse 18.24
22 Hima, ujiponye huko, maana siwezi kufanya neno lo lote, hata uingiapo humo. Kwa hiyo jina la mji ule likaitwa Soari.
Genèse 14.2 Genèse 13.10 Psaumes 91.1-91.10 Jérémie 48.34 Deutéronome 9.14
23 Jua lilikuwa limechomoza juu ya nchi Lutu alipoingia Soari.
24 Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana.
Deutéronome 29.23 Esaïe 13.19 2 Pierre 2.6 Jérémie 50.40 Jude 1.7
25 Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile.
Psaumes 107.34 Genèse 14.3 Genèse 13.10
26 Lakini mkewe Lutu akatazama nyuma yake, akawa nguzo ya chumvi.
Genèse 19.17 Proverbes 14.14 Hébreux 10.38 Nombres 16.38 Luc 17.31-17.32
27 Ibrahimu akatoka asubuhi kwenda mahali aliposimama mbele za Bwana,
Habakuk 2.1 Psaumes 5.3 Ezéchiel 16.49-16.50 Hébreux 2.1 Genèse 18.22-18.33
28 naye akatazama upande wa Sodoma na Gomora na nchi yote ya hilo Bonde, akaona, na tazama, moshi wa nchi ukapanda, kama moshi wa tanuru.
Apocalypse 18.9 Apocalypse 18.18 Apocalypse 21.8 Apocalypse 19.3 Apocalypse 14.10-14.11
29 Ikawa Mungu alipoiharibu miji ya Bondeni, Mungu akamkumbuka Ibrahimu, akamtoa Lutu katika maangamizi alipoiangamiza miji hiyo aliyokaa Lutu.
Deutéronome 9.5 Genèse 8.1 Genèse 12.2 2 Pierre 2.7 Psaumes 106.4

Descendance de Lot

30 Lutu akapanda kutoka Soari akakaa mlimani, na binti zake wawili pamoja naye, kwa sababu aliogopa kukaa katika Soari. Akakaa katika pango, yeye na binti zake wawili.
Genèse 19.19 Jacques 1.8 Genèse 49.4 Deutéronome 34.3 Genèse 19.17
31 Yule mkubwa akamwambia mdogo, Baba yetu ni mzee, wala hakuna mtu mume katika nchi atuingilie kama ilivyo desturi ya dunia yote.
Deutéronome 25.5 Genèse 16.4 Genèse 16.2 Genèse 19.28 Genèse 6.4
32 Haya, na tumnyweshe baba yetu mvinyo, tukalale naye, ili tumhifadhie baba yetu uzao.
Lévitique 18.6-18.7 Genèse 11.3 Genèse 9.21 Habakuk 2.15-2.16 Proverbes 23.31-23.33
33 Wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka huyo mkubwa akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.
Habakuk 2.15-2.16 Lévitique 18.6-18.7 Proverbes 23.29-23.35 Proverbes 20.1
34 Ikawa siku ya pili, mkubwa akamwambia mdogo, Tazama, nimelala jana na baba yangu, tumnyweshe mvinyo tena usiku huu, ukaingie ukalale naye.
Jérémie 8.12 Jérémie 3.3 Jérémie 5.3 Esaïe 3.9 Jérémie 6.15
35 Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.
1 Pierre 4.7 Luc 21.34 Psaumes 8.4 Proverbes 24.16 1 Corinthiens 10.11-10.12
36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
1 Samuel 15.33 Habakuk 2.15 Matthieu 7.2 Juges 1.7 Genèse 19.8
37 Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo.
Deutéronome 2.9 Nombres 24.1-24.25 Juges 3.1-3.31 Nombres 22.1-22.41 Deutéronome 23.3
38 Na yule mdogo naye akazaa mwana akamwita jina lake Benami; huyo ndiye baba wa Waamoni hata leo.
Deutéronome 2.19 Néhémie 13.23-13.28 2 Samuel 10.1-10.19 Esaïe 11.14 Deutéronome 23.3

Cette Bible est dans le domaine public.