Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 7.10
Bible en Swahili de l’est


Supériorité de Melchisédek sur les Lévites

1 Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
Genèse 14.18-14.20 Marc 5.7 Psaumes 76.2 Daniel 5.21 Esaïe 41.2-41.3
2 ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;
2 Samuel 8.15 1 Rois 4.24-4.25 Psaumes 72.1-72.3 Lévitique 27.32 Psaumes 45.4-45.7
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Hébreux 7.23-7.28 Hébreux 7.6 Exode 6.18 1 Chroniques 6.1-6.3 Hébreux 7.17
4 Basi, angalieni jinsi mtu huyo alivyokuwa mkuu, ambaye Ibrahimu, baba yetu mkuu, alimpa sehemu ya kumi ya nyara.
Actes 2.29 Genèse 14.20 Actes 7.8-7.9 Romains 4.17-4.18 Genèse 17.5-17.6
5 Na katika wana wa Lawi nao, wale waupatao ukuhani, wana amri kutwaa sehemu ya kumi kwa watu wao, yaani, ndugu zao, kwa agizo la sheria, ijapokuwa wametoka katika viuno vya Ibrahimu.
Nombres 18.21-18.32 Exode 28.1 Nombres 17.3-17.10 2 Chroniques 31.4-31.6 1 Rois 8.19
6 Bali yeye, ambaye uzazi wake haukuhesabiwa kuwa umetoka kwa hao, alitwaa sehemu ya kumi kwa Ibrahimu, akambariki yeye aliye na ile ahadi.
Romains 4.13 Genèse 14.19-14.20 Hébreux 7.3-7.4 Genèse 13.14-13.17 Genèse 12.13
7 Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.
2 Chroniques 30.27 1 Rois 8.55 Genèse 48.15-48.20 Genèse 27.20-27.40 Genèse 49.28
8 Na hapa wanadamu wapatikanao na kufa hutwaa sehemu ya kumi; bali huko yeye ashuhudiwaye kwamba yu hai.
Hébreux 5.6 Hébreux 6.20 Apocalypse 1.18 Jean 14.6 Jean 11.25-11.26
9 Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi;
Romains 5.12 Genèse 14.20 Hébreux 7.4
10 kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.
1 Rois 8.19 Genèse 35.11 Hébreux 7.5 Genèse 46.26
11 Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?
Hébreux 8.7 Hébreux 5.6 Galates 2.21 Hébreux 7.17-7.19 Galates 4.9
12 Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.
Ezéchiel 16.61 Jérémie 31.31-31.34 Esaïe 66.21 Actes 6.13-6.14
13 Maana yeye aliyenenwa hayo alikuwa mshirika wa kabila nyingine, ambayo hapana mtu wa kabila hiyo aliyeihudumia madhabahu.
Hébreux 7.14 2 Chroniques 26.16-26.21 Nombres 16.40 Nombres 17.5 Hébreux 7.11
14 Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lo lote juu yake katika mambo ya ukuhani.
Esaïe 11.1 Michée 5.2 Apocalypse 5.5 Luc 3.33 Romains 1.3
15 Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa ametokea kuhani mwingine mithili ya Melkizedeki;
Psaumes 110.4 Hébreux 7.3 Hébreux 7.17-7.21 Hébreux 7.11
16 asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, bali kwa nguvu za uzima usio na ukomo;
Apocalypse 1.18 Hébreux 7.3 Hébreux 10.1 Hébreux 7.21 Hébreux 7.24-7.25
17 maana ameshuhudiwa kwamba, Wewe u kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki.
Hébreux 5.6 Psaumes 110.4 Hébreux 6.20 Hébreux 7.21 Hébreux 5.10
18 Maana, kuna kubatiliwa kwa ile amri iliyotangulia, kwa sababu ya udhaifu wake, na kutokufaa kwake;
Romains 8.3 Actes 13.39 Hébreux 7.19 Galates 4.9 Hébreux 10.1-10.9
19 (kwa maana ile sheria haikukamilisha neno); na pamoja na hayo kuliingizwa matumaini yaliyo mazuri zaidi, ambayo kwa hayo twamkaribia Mungu.
Hébreux 4.16 Actes 13.39 Hébreux 9.9 Romains 8.3 Hébreux 6.18
20 Na kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo,
21 (maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana ameapa wala hataghairi, Wewe u kuhani wa milele;)
Psaumes 110.4 Hébreux 7.17 1 Samuel 15.29 Hébreux 6.16-6.18
22 basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
Luc 22.20 Genèse 44.32 Hébreux 12.24 Hébreux 9.15-9.23 Hébreux 13.20
23 Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;
Hébreux 7.8 Néhémie 12.10-12.11 1 Chroniques 6.3-6.14
24 bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.
Hébreux 7.28 Jean 12.34 Apocalypse 1.18 Hébreux 7.8-7.25 Romains 6.9
25 Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Romains 8.34 1 Jean 2.1-2.2 Jean 14.6 Hébreux 7.19 Romains 5.2
26 Maana ilitupasa sisi tuwe na kuhani mkuu wa namna hii aliye mtakatifu, asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji, aliyekuwa juu kuliko mbingu;
Hébreux 8.1 Hébreux 4.14-4.15 2 Corinthiens 5.21 1 Pierre 2.22 1 Jean 3.5
27 ambaye hana haja kila siku, mfano wa wale makuhani wakuu wengine, kwanza kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za hao watu; maana yeye alifanya hivi mara moja, alipojitoa nafsi yake.
Hébreux 9.28 Hébreux 9.12 Hébreux 5.3 Hébreux 9.14 Esaïe 53.10-53.12
28 Maana torati yawaweka wanadamu walio na unyonge kuwa makuhani wakuu; bali hilo neno la kiapo kilichokuja baada ya torati limemweka Mwana, aliyekamilika hata milele.
Hébreux 2.10 Hébreux 1.2 Hébreux 7.21 Hébreux 5.1-5.2 Hébreux 4.14

Cette Bible est dans le domaine public.