Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 7.23
Bible en Swahili de l’est


Ordre de détruire les Cananéens et leurs idoles

1 Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang’oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe;
Deutéronome 4.38 Deutéronome 31.3 Deutéronome 9.1 Psaumes 44.2-44.3 Deutéronome 6.10
2 wakati Bwana, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao;
Deutéronome 23.14 Deutéronome 20.16-20.17 Josué 2.14 Lévitique 27.28-27.29 Juges 1.24
3 binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake.
Exode 34.15-34.16 1 Rois 11.2 Josué 23.12-23.13 2 Corinthiens 6.14-6.17 Genèse 6.2-6.3
4 Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi.
Deutéronome 6.15 Deutéronome 32.16-32.17 Juges 10.6-10.7 Juges 2.20 Deutéronome 4.26
5 Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.
Exode 34.13 Exode 23.24 Deutéronome 7.25 Deutéronome 12.2-12.3 Deutéronome 9.21
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako; Bwana Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.
Deutéronome 14.2 Exode 19.5-19.6 Tite 2.14 Deutéronome 26.19 1 Pierre 2.9
7 Bwana hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
Deutéronome 10.22 Romains 11.6 Romains 9.18 1 Jean 3.1 Romains 9.27-9.29
8 bali kwa sababu Bwana anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu, ndiyo sababu Bwana akawatoa kwa mkono wa nguvu, akawakomboa katika nyumba ya utumwa, katika mkono wa Farao, mfalme wa Misri.
Jérémie 31.3 Exode 32.13 Deutéronome 10.15 Luc 1.72-1.73 Esaïe 43.4
9 Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu;
2 Timothée 2.13 Hébreux 10.23 1 Corinthiens 1.9 Daniel 9.4 Néhémie 1.5
10 naye huwalipa wamchukiao mbele ya uso wao, kuwaangamiza. Hatakuwa mlegevu kwake yeye amchukiaye, atamlipa mbele ya uso wake.
Nahum 1.2 Esaïe 59.18 Deutéronome 32.35 Deutéronome 7.9 Deutéronome 32.25
11 Basi zishike amri, na sheria, na hukumu ninazokuamuru leo, uzitende.
Jean 14.15 Deutéronome 5.32 Deutéronome 4.1
12 Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiliza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimilizia agano na rehema aliyowaapia baba zako;
Lévitique 26.3-26.13 Deutéronome 28.1-28.14 Luc 1.55 Deutéronome 7.9 Psaumes 105.8-105.10
13 naye atakupenda na kukubarikia na kukuongeza tena ataubarikia uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, nafaka zako na divai yako, na mafuta yako, maongeo ya ng’ombe zako, na wadogo wa kondoo zako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwa atakupa.
Jean 14.21 Job 42.12 Matthieu 6.33 Psaumes 144.12-144.15 Exode 23.25
14 Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mtu mume wala mke aliye tasa kati yenu; wala kati ya wanyama wenu wa mifugo.
Psaumes 127.3 Deutéronome 28.11 Psaumes 115.15 Deutéronome 33.29 Lévitique 26.9
15 Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao.
Exode 15.26 Deutéronome 28.60 Exode 9.11 Deutéronome 28.27 Lévitique 26.3-26.4
16 Nawe angamiza mataifa yote atakayokupa Bwana, Mungu wako; jicho lako lisiwahurumie, wala usiitumikie miungu yao; kwani litakuwa ni mtego kwako jambo hilo.
Juges 8.27 Exode 23.33 Psaumes 106.36 Deutéronome 19.21 Deutéronome 25.12
17 Nawe kama ukisema moyoni mwako, Mataifa haya ni mengi kunipita mimi; nitawatoaje katika milki yao?
Nombres 33.53 Nombres 13.32 Jérémie 13.22 Esaïe 47.8 Deutéronome 15.9
18 Usiwaogope; kumbuka sana Bwana, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote;
Psaumes 105.5 Deutéronome 31.6 Deutéronome 1.29 Psaumes 77.11 Deutéronome 3.6
19 uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.
Deutéronome 4.34 Ezéchiel 20.6-20.9 Josué 3.10 Deutéronome 11.2-11.4 Jérémie 32.20-32.21
20 Tena Bwana, Mungu wako, atampeleka mavu kati yao, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.
Josué 24.12 Exode 23.28-23.30
21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho.
Deutéronome 10.17 Josué 3.10 Néhémie 9.32 Néhémie 1.5 Nombres 14.14
22 Naye Bwana, Mungu wako, atayatupia nje mataifa yale mbele yako kidogo kidogo; haikupasi kuwaangamiza kwa mara moja, wasije wakaongezeka kwako wanyama wa mwitu.
Exode 23.29-23.30 Josué 15.63
23 Ila Bwana, Mungu wako, atawatoa mbele yako, atawatia mashaka, mashaka makuu, hata waishe kuangamizwa.
Deutéronome 9.3 Esaïe 13.6 Joël 1.15 Jérémie 17.18 2 Thessaloniciens 1.9
24 Na wafalme wao atakutilia mkononi mwako, nawe utalipoteza jina lao litoke chini ya mbingu; hapana mtu atakayeweza kusimama mbele yako, hata utakapokwisha kuwaangamiza.
Josué 23.9 Josué 1.5 Josué 10.8 Deutéronome 11.25 Deutéronome 9.14
25 Sanamu za kuchonga za miungu yao mtaziteketeza kwa moto; usitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala usiitwae iwe yako usije ukanaswa nayo; kwa maana ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako;
Exode 32.20 1 Chroniques 14.12 Deutéronome 17.1 Deutéronome 12.3 Josué 7.21
26 na machukizo usitie ndani ya nyumba yako, usije wewe kuwa kitu cha haramu mfano wake; ukichukie kabisa, na kukikataa kabisa; kwa kuwa ni kitu kilichoharimishwa.
Deutéronome 13.17 Esaïe 30.22 Lévitique 27.28-27.29 Ezéchiel 11.18 Habakuk 2.9-2.11

Cette Bible est dans le domaine public.