Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 9.23
Bible en Swahili de l’est


Exemple de Paul

1 Je! Mimi si huru? Mimi si mtume? Mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Ninyi si kazi yangu katika Bwana?
Actes 9.3 Actes 9.17 1 Corinthiens 3.6 Actes 23.11 1 Corinthiens 9.19
2 Kwa maana ikiwa mimi si mtume kwa wengine, lakini ni mtume kwenu ninyi; kwa maana ninyi ndinyi muhuri ya utume wangu katika Bwana.
2 Corinthiens 3.1-3.3 Jean 6.27 2 Corinthiens 12.12
3 Hilo ndilo jawabu langu kwa wale wanaoniuliza.
Actes 25.16 2 Corinthiens 13.10 1 Corinthiens 14.37 2 Timothée 4.16 Actes 22.1
4 Je! Hatuna uwezo wa kula na kunywa?
1 Thessaloniciens 2.6 2 Thessaloniciens 3.8-3.9 Matthieu 10.10 Galates 6.6 1 Corinthiens 9.7-9.14
5 Hatuna uwezo kuchukua pamoja nasi mke aliye ndugu, kama wao mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?
Jean 1.42 Matthieu 8.14 Galates 1.19 1 Corinthiens 7.7 Actes 1.14
6 Au je! Ni mimi peke yangu na Barnaba tusio na uwezo wa kutokufanya kazi?
Actes 4.36 2 Thessaloniciens 3.7-3.9 Actes 13.1-13.2 Actes 18.3 1 Thessaloniciens 2.9
7 Ni askari gani aendaye vitani wakati wo wote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi?
Proverbes 27.18 Deutéronome 20.6 2 Timothée 2.3-2.4 1 Timothée 1.18 Cantique 8.12
8 Je! Ninanena hayo kwa kibinadamu? Au torati nayo haisemi yayo hayo?
1 Thessaloniciens 4.8 Romains 6.19 Esaïe 8.20 1 Thessaloniciens 2.13 1 Corinthiens 14.34
9 Kwa maana katika torati ya Musa imeandikwa, Usimfunge kinywa ng’ombe apurapo nafaka. Je! Hapo Mungu aangalia mambo ya ng’ombe?
Deutéronome 25.4 1 Timothée 5.18 Psaumes 104.27 Psaumes 145.15-145.16 Psaumes 147.8-147.9
10 Au yamkini anena hayo kwa ajili yetu? Naam, yaliandikwa kwa ajili yetu; kwa kuwa alimaye nafaka ni haki yake kulima kwa matumaini, naye apuraye nafaka ni haki yake kutumaini kupata sehemu yake.
2 Timothée 2.6 Romains 4.23-4.24 1 Corinthiens 3.9 2 Corinthiens 4.15 Jean 4.35-4.38
11 Ikiwa sisi tuliwapandia ninyi vitu vya rohoni, je! Ni neno kubwa tukivuna vitu vyenu vya mwilini?
Romains 15.27 Galates 6.6 2 Corinthiens 11.15 2 Rois 5.13 Matthieu 10.10
12 Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.
2 Corinthiens 11.12 1 Corinthiens 9.18 1 Corinthiens 9.15 2 Corinthiens 11.7-11.10 Romains 15.22
13 Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
Lévitique 6.26 Nombres 18.8-18.20 Nombres 5.9-5.10 Deutéronome 10.9 1 Corinthiens 10.18
14 Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.
Matthieu 10.10 1 Corinthiens 9.4 Luc 10.7 1 Timothée 5.17-5.18 Galates 6.6
15 Lakini mimi sikutumia mambo hayo hata moja. Wala siyaandiki hayo ili iwe hivyo kwangu mimi; maana ni heri nife kuliko mtu awaye yote abatilishe huku kujisifu kwangu.
Actes 18.3 1 Corinthiens 9.12 1 Corinthiens 4.12 2 Corinthiens 11.9-11.12 Philippiens 1.20-1.23
16 Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili!
Romains 1.14 Actes 9.15 Luc 9.62 Actes 4.20 Actes 9.6
17 Maana nikiitenda kazi hii kwa hiari yangu nina thawabu; ila ikiwa si kwa hiari yangu, nimeaminiwa uwakili.
Galates 2.7 Colossiens 1.25 1 Corinthiens 3.8 1 Corinthiens 4.1 1 Corinthiens 3.14
18 Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.
1 Corinthiens 7.31 1 Corinthiens 9.6-9.7 1 Thessaloniciens 2.6 1 Corinthiens 10.33 2 Thessaloniciens 3.8-3.9
19 Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi.
Matthieu 18.15 Galates 5.13 1 Pierre 3.1 Matthieu 20.26-20.28 2 Timothée 2.10
20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
Actes 16.3 Galates 5.18 Actes 21.20-21.26 Actes 17.2-17.3 Romains 11.14
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria.
Romains 2.14 Romains 2.12 Galates 3.2 Matthieu 5.17-5.20 Psaumes 119.32
22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
1 Corinthiens 10.33 Romains 15.1 Romains 11.14 2 Corinthiens 11.29 1 Corinthiens 9.19
23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.
2 Timothée 2.10 Hébreux 3.14 Marc 8.35 1 Pierre 5.1 1 Corinthiens 9.12
24 Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
1 Corinthiens 9.26 Hébreux 12.1 Philippiens 3.14 Philippiens 2.16 Galates 2.2
25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.
Apocalypse 2.10 Jacques 1.12 1 Timothée 6.12 2 Timothée 4.7-4.8 2 Pierre 1.6
26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
2 Timothée 1.12 Colossiens 1.29 2 Pierre 1.10 Philippiens 1.21 Luc 13.24
27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.
Romains 8.13 1 Corinthiens 8.13 2 Corinthiens 13.5-13.6 1 Corinthiens 9.25 Colossiens 3.5

Cette Bible est dans le domaine public.