Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 26.9
Bible en Swahili de l’est


1 Agripa akamwambia Paulo, Una ruhusa kusema maneno yako. Ndipo Paulo akanyosha mkono wake, akajitetea,
Actes 9.15 Proverbes 18.17 Actes 26.2 Proverbes 1.24 Actes 22.1
2 Najiona nafsi yangu kuwa na heri, Ee mfalme Agripa, kwa kuwa nitajitetea mbele yako leo, katika mambo yale yote niliyoshitakiwa na Wayahudi.
3 Hasa kwa sababu wewe unajua sana desturi na maswali yote waliyo nayo Wayahudi; kwa sababu hiyo nakuomba unisikilize kwa uvumilivu.
Actes 6.14 Actes 26.26 Actes 26.7 Actes 24.10 Actes 25.26
4 Kwa maana Wayahudi wote wanajua maisha yangu tangu ujana, yaliyokuwa tangu mwanzo katika taifa langu huko Yerusalemu,
Galates 1.13 Actes 22.3 2 Timothée 3.10 Philippiens 3.5
5 wakinijua sana tangu mwanzo, kama wakipenda kushuhudia, ya kwamba nalikuwa Farisayo kwa kuifuata madhehebu ya dini yetu iliyo sahihi kabisa.
Actes 23.6 Actes 24.5 Actes 22.3 Philippiens 3.5-3.6 Actes 24.14
6 Na sasa ninasimama hapa nihukumiwe kwa ajili ya tumaini la ahadi baba zetu waliyopewa na Mungu,
Actes 28.20 Actes 24.15 Michée 5.2 Romains 15.8 Actes 23.6
7 ambayo kabila zetu kumi na mbili wanataraji kuifikia, wakimwabudu Mungu kwa bidii mchana na usiku. Nami ninashitakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hilo, Ee Mfalme.
Jacques 1.1 Matthieu 19.28 1 Thessaloniciens 3.10 1 Timothée 5.5 Esdras 6.17
8 Kwa nini limedhaniwa kwenu kuwa ni neno lisilosadikika, kwamba Mungu awafufua wafu?
Actes 4.2 Actes 10.40-10.42 Actes 13.30-13.31 Actes 17.31-17.32 Actes 25.19
9 Kweli, mimi mwenyewe naliona ndani ya nafsi yangu kwamba yanipasa kutenda mambo mengi yaliyopingamana na jina lake Yesu Mnazareti;
1 Timothée 1.13 Actes 22.8 Romains 10.2 Jean 15.21 Actes 9.16
10 nami nikayafanya hayo Yerusalemu; niliwafunga wengi miongoni mwa watakatifu ndani ya magereza, nikiisha kupewa amri na wakuu wa makuhani; na walipouawa nalitoa idhini yangu.
Actes 8.3 Actes 9.21 Actes 9.13-9.14 Actes 22.4-22.5 Galates 1.13
11 Na mara nyingi katika masinagogi yote naliwaadhibu, nikawashurutisha kukufuru; nikawaonea hasira kama mwenye wazimu, nikawaudhi hata katika miji ya ugenini.
Actes 13.45 Matthieu 10.17 Actes 22.19 Luc 21.12 Jacques 2.7
12 Basi katika kazi hiyo nilipokuwa nikienda Dameski, mwenye mamlaka na maagizo ya wakuu wa makuhani;
Jean 7.45-7.48 Actes 26.10 Actes 22.5-22.11 Psaumes 94.20-94.21 Jérémie 26.8
13 Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote.
Matthieu 17.2 Esaïe 24.23 Actes 22.6 Apocalypse 1.16 Actes 9.3
14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
Actes 21.40 Actes 9.7 Actes 22.2 1 Corinthiens 10.22 Actes 9.4-9.5
15 Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.
Jean 15.20-15.21 Exode 16.8 Matthieu 25.45 Matthieu 25.40
16 Lakini inuka, usimame kwa miguu yako, maana nimekutokea kwa sababu hii, nikuweke wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako;
Actes 22.14-22.15 Ezéchiel 2.1 Daniel 10.11 2 Corinthiens 4.1 1 Thessaloniciens 3.2
17 nikikuokoa na watu wako, na watu wa Mataifa, ambao nakutuma kwao;
Actes 9.15 Jérémie 1.19 Jérémie 1.8 Romains 11.13 1 Timothée 2.7
18 uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.
1 Pierre 2.9 Actes 20.32 Ephésiens 1.18 Esaïe 42.7 2 Corinthiens 4.6
19 Kwa hiyo, Ee Mfalme Agripa, sikuyaasi yale maono ya mbinguni,
Galates 1.16 Jonas 1.3 Actes 26.2 Esaïe 50.5 Actes 26.26-26.27
20 bali kwanza niliwahubiri wale wa Dameski na Yerusalemu, na katika nchi yote ya Uyahudi, na watu wa Mataifa, kwamba watubu na kumwelekea Mungu, wakiyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao.
Actes 3.19 Matthieu 3.8 Actes 2.38 Matthieu 9.13 Actes 9.35
21 Kwa sababu ya hayo Wayahudi wakanikamata ndani ya hekalu wakajaribu kuniua.
Actes 21.30-21.31 Actes 21.27 Actes 22.22 Actes 23.12-23.15 Actes 25.3
22 Basi kwa kuwa nimeupata msaada utokao kwa Mungu nimesimama hata leo hivi nikiwashuhudia wadogo kwa wakubwa, wala sisemi neno ila yale ambayo manabii na Musa waliyasema, kwamba yatakuwa;
Actes 24.14 Jean 5.46 Luc 24.44 Actes 10.43 Luc 24.27
23 ya kwamba Kristo hana budi kuteswa na ya kwamba yeye kwanza kwa kufufuliwa katika wafu atatangaza habari za nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.
Apocalypse 1.5 Luc 2.32 Colossiens 1.18 Luc 24.26 Zacharie 13.7
24 Alipokuwa akijitetea hivi, Festo akasema kwa sauti kuu, Paulo, una wazimu, kusoma kwako kwingi kumekugeuza akili.
1 Corinthiens 4.10 Marc 3.21 2 Rois 9.11 Jérémie 29.26 2 Corinthiens 5.13
25 Lakini Paulo akasema, Sina wazimu, Ee Festo mtukufu, bali nanena maneno ya kweli na ya akili kamili.
Actes 23.26 Actes 24.3 1 Pierre 3.9 1 Pierre 2.21-2.23 1 Pierre 3.15
26 Kwa maana mfalme anajua habari za mambo haya, nami naweza kusema naye kwa ujasiri, kwa sababu najua sana ya kuwa hapana neno moja katika hayo asilolijua; kwa maana jambo hilo halikutendeka pembeni.
Actes 2.1-2.12 Actes 5.18-5.42 Matthieu 26.5 Actes 26.2-26.3 Matthieu 27.29-27.54
27 Mfalme Agripa, je! Wawaamini manabii? Najua ya kuwa wawaamini.
Actes 26.22-26.23
28 Agripa akamwambia Paulo, Kwa maneno machache wadhani kunifanya mimi kuwa Mkristo.
Actes 11.26 2 Corinthiens 4.2 Jacques 1.23-1.24 Ezéchiel 33.31 Marc 10.17-10.22
29 Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe kama mimi, isipokuwa vifungo hivi.
Actes 21.33 1 Corinthiens 7.7 Luc 19.41-19.42 2 Rois 5.3 2 Corinthiens 11.1
30 Mfalme na liwali na Bernike na wale walioketi pamoja nao wakasimama;
Actes 18.15 Actes 25.23 Actes 28.22
31 hata walipoondoka wakasemezana, wakisema, Mtu huyu hatendi neno linalostahili kifo wala kufungwa.
Actes 23.29 Actes 23.9 Actes 25.25 1 Pierre 3.16 1 Pierre 4.14-4.16
32 Agripa akamwambia Festo, Mtu huyo angeweza kufunguliwa, kama asingalitaka rufani kwa Kaisari.
Actes 28.18 Actes 25.25 Actes 25.11-25.12

Cette Bible est dans le domaine public.