Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 7.11
Bible en Swahili de l’est


Jésus à la fête des tentes

1 Na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua.
Jean 7.19 Jean 4.3 Matthieu 21.38 Matthieu 10.23 Jean 5.16-5.18
2 Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Zacharie 14.16-14.19 Nombres 29.12-29.38 Deutéronome 16.13-16.16 Exode 23.16-23.17 Esdras 3.4
3 Basi ndugu zake wakamwambia, Ondoka hapa, uende Uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama kazi zako unazozifanya.
Matthieu 12.46 Jean 7.5 Matthieu 22.16-22.17 Jérémie 12.6 Marc 3.31
4 Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu.
Jean 18.20 Proverbes 18.1-18.2 Luc 6.45 Matthieu 23.5 Matthieu 6.5
5 Maana hata nduguze hawakumwamini.
Marc 3.21 Jean 1.11-1.13 Michée 7.5-7.6 Jean 7.3 Jean 7.10
6 Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo.
Jean 7.8 Jean 2.4 Jean 7.30 Jean 17.1 Jean 13.1
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu.
Jean 15.18-15.19 Jean 3.19 Proverbes 9.7-9.8 Galates 4.16 Proverbes 15.12
8 Kweeni ninyi kwenda kula sikukuu; mimi sikwei bado kwenda kula sikukuu hii, kwa kuwa haujatimia wakati wangu.
Jean 7.6 Jean 7.30 Jean 8.20 Jean 11.6-11.7 1 Corinthiens 2.15-2.16
9 Naye alipokwisha kuwaambia hayo, alikaa vivi hivi huko Galilaya.
10 Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye alipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.
Amos 5.13 Matthieu 3.15 Psaumes 26.8 Psaumes 40.8 Galates 4.4
11 Basi Wayahudi wakamtafuta kwenye sikukuu, wakasema, Yuko wapi yule?
Jean 11.56
12 Kukawa na manung’uniko mengi katika makutano juu yake. Wengine wakasema, Ni mtu mwema. Na wengine wakasema, Sivyo; bali anawadanganya makutano.
Jean 9.16 Jean 7.40-7.43 Jean 7.47 Jean 7.32 Jean 7.52
13 Walakini hakuna mtu aliyemtaja waziwazi, kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
Jean 9.22 Jean 19.38 Jean 20.19 2 Timothée 2.9-2.13 Jean 12.42-12.43
14 Hata ikawa katikati ya sikukuu Yesu alikwea kuingia hekaluni, akafundisha.
Luc 19.47 Jean 7.28 Aggée 2.7-2.9 Jean 5.14 Nombres 29.23-29.40
15 Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?
Luc 4.22 Jean 7.46 Luc 2.47 Matthieu 13.54 Jean 1.19
16 Basi Yesu akawajibu, akasema, Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka.
Jean 14.24 Jean 3.11 Jean 5.23-5.24 Jean 5.30 Jean 6.38-6.40
17 Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.
Jean 8.31-8.32 Jean 8.43 Philippiens 3.15-3.16 Psaumes 119.10 Jean 8.47
18 Yeye anenaye kwa nafsi yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka, huyo ni wa kweli, wala ndani yake hamna udhalimu.
Jean 5.41 1 Corinthiens 10.31-10.33 Galates 6.12-6.14 Jean 8.49-8.50 Philippiens 2.3-2.5
19 Je! Musa hakuwapa torati? Wala hakuna mmoja wenu aitendaye torati. Mbona mnatafuta kuniua?
Jean 1.17 Matthieu 12.14 Jean 7.1 Galates 3.19 Galates 6.13
20 Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua?
Jean 10.20 Jean 8.48 Jean 8.52 Marc 3.21-3.22 Matthieu 11.18-11.19
21 Yesu akajibu, akawaambia, Mimi nalitenda kazi moja, nanyi nyote mnaistaajabia.
Jean 5.2-5.11 Jean 7.23
22 Musa aliwapa tohara; lakini si kwamba yatoka kwa Musa, bali kwa mababa; nanyi siku ya sabato humtahiri mtu.
Lévitique 12.3 Genèse 17.10-17.14 Romains 4.9-4.11 Galates 3.17
23 Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato?
Matthieu 12.5 Jean 5.14-5.16 Jean 5.8-5.9 Matthieu 12.2
24 Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki.
Esaïe 11.3-11.4 Jean 8.15 Deutéronome 1.16-1.17 Proverbes 17.15 Jacques 2.9
25 Basi baadhi ya watu wa Yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue?
Jean 7.10-7.11
26 Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu wanajua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo?
Jean 7.48 Psaumes 40.9-40.10 Esaïe 42.4 Luc 7.30 Proverbes 28.1
27 Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.
Jean 6.42 Michée 5.2 Matthieu 13.54-13.57 Jean 9.29 Jean 7.41-7.42
28 Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi.
Jean 8.42 Jean 8.19 Jean 7.14 Jean 8.26 Jean 5.43
29 Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.
Jean 8.55 Matthieu 11.27 Jean 13.3 Jean 16.27-16.28 Jean 3.16-3.17
30 Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.
Jean 8.20 Jean 10.39 Jean 7.6 Jean 7.32 Esaïe 46.10
31 Na watu wengi katika mkutano wakamwamini; wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu?
Jean 12.42 Matthieu 12.23 Jean 2.23-2.24 Jean 9.16 Matthieu 11.3-11.6
32 Mafarisayo wakawasikia mkutano wakinung’unika hivi juu yake; basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma watumishi ili wamkamate.
Matthieu 12.23-12.24 Jean 11.47-11.48 Luc 22.52-22.53 Jean 18.3 Actes 5.26
33 Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.
Jean 16.5 Jean 13.33 Jean 16.16-16.22 Jean 17.11 Jean 14.19
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja.
Osée 5.6 Proverbes 1.24-1.31 Jean 17.24 Luc 17.22-17.23 Jean 8.21-8.24
35 Basi Wayahudi wakasemezana, Huyu atakwenda wapi hata sisi tusimwone? Ati! Atakwenda kwa Utawanyiko wa Wayunani, na kuwafundisha Wayunani?
Jacques 1.1 1 Pierre 1.1 Esaïe 11.12 Sophonie 3.10 Jean 12.20
36 Ni neno gani hilo alilolisema, Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja?
Jean 7.34 Jean 6.41 Jean 3.4 Jean 3.9 1 Corinthiens 2.14
37 Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
Esaïe 55.1 Jean 4.10 Psaumes 42.2 Psaumes 63.1 Apocalypse 22.17
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
Esaïe 58.11 Jean 4.14 Esaïe 44.3 Esaïe 12.3 Jean 4.10
39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Joël 2.28 Actes 2.17 Esaïe 32.15 Actes 2.33 Actes 2.4
40 Basi wengine katika mkutano walipoyasikia maneno hayo, walisema, Hakika huyu ndiye nabii yule.
Matthieu 21.11 Jean 1.21 Jean 6.14
41 Wengine walisema, Huyu ndiye Kristo. Wengine wakasema, Je! Kristo atoka Galilaya?
Jean 7.52 Jean 1.46 Jean 1.41 Jean 4.42 Jean 4.25
42 Andiko halikusema ya kwamba Kristo atoka katika uzao wa Daudi, na kutoka Bethlehemu, mji ule alioukaa Daudi?
Michée 5.2 Matthieu 2.5 Luc 2.4 Luc 2.11 Matthieu 1.1
43 Basi kukaingia matengano katika mkutano kwa ajili yake.
Jean 10.19 Jean 9.16 Jean 7.12 Actes 14.4 Actes 23.7-23.10
44 Baadhi yao wakataka kumkamata, lakini hakuna mtu aliyenyosha mikono yake ili kumshika.
Jean 7.30 Actes 23.11 Jean 8.20 Jean 18.5-18.6 Actes 18.10
45 Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta?
Jean 7.32 Actes 5.21-5.27
46 Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena.
Luc 4.22 Matthieu 7.28-7.29 Jean 7.26
47 Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika?
Jean 7.12 2 Rois 18.32 Matthieu 27.63 2 Rois 18.29 2 Chroniques 32.15
48 Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo?
Jean 12.42 1 Corinthiens 2.8 Jean 7.26 1 Corinthiens 1.20 Jean 7.50
49 Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa.
Jacques 3.13-3.18 Esaïe 65.5 Esaïe 5.21 Esaïe 28.14 1 Corinthiens 1.20-1.21
50 Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao),
Jean 19.39 Jean 3.1-3.2
51 Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo?
Proverbes 18.13 Deutéronome 1.17 Actes 23.3 Deutéronome 17.6 Deutéronome 19.15-19.19
52 Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya!
Jean 7.41 Jean 1.46 Jean 9.34 Esaïe 9.1-9.2 1 Rois 22.24
53 Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.
Psaumes 76.5 Psaumes 76.10 Job 5.12-5.13 Psaumes 33.10

Cette Bible est dans le domaine public.