Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 19.6
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ndipo Pilato alipomtwaa Yesu, akampiga mijeledi.
Esaïe 53.5 Esaïe 50.6 Luc 23.16 Matthieu 20.19 Marc 15.15-15.20
2 Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau.
Esaïe 53.3 Jean 19.5 Luc 23.11 Marc 15.16-15.20 Matthieu 27.27-27.31
3 Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi.
Matthieu 27.29 Jean 18.33 Jean 18.22 Luc 1.28 Matthieu 26.49
4 Kisha Pilato akatokea tena nje, akawaambia, Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake.
Jean 18.38 Jean 19.6 Luc 23.4 Matthieu 27.54 1 Pierre 3.18
5 Ndipo Yesu alipotoka nje, naye amevaa ile taji ya miiba, na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, Tazama, mtu huyu!
Jean 19.2 Esaïe 43.1 Esaïe 40.9 Hébreux 12.2 Lamentations 1.12
6 Basi wale wakuu wa makuhani na watumishi wao walipomwona, walipiga kelele wakisema, Msulibishe! Msulibishe! Pilato akawaambia, Mtwaeni ninyi basi, mkamsulibishe; kwa maana mimi sioni hatia kwake.
Jean 18.31 Jean 19.4 Actes 3.13-3.15 Actes 7.52 Matthieu 27.24
7 Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu.
Jean 5.18 Lévitique 24.16 Romains 1.4 Matthieu 26.63-26.66 Jean 10.36-10.38
8 Basi Pilato aliposikia neno hilo, akazidi kuogopa.
Jean 19.13 Actes 14.11-14.19
9 Akaingia tena ndani ya ile Praitorio, akamwambia Yesu, Wewe umetokapi? Lakini Yesu hakumpa jibu lo lote.
Jean 18.33 Jean 8.14 Juges 13.6 Esaïe 53.7 Psaumes 38.13-38.15
10 Basi Pilato akamwambia, Husemi nami? Hujui ya kuwa mimi nina mamlaka ya kukufungua, nami nina mamlaka ya kukusulibisha?
Jean 18.39 Daniel 5.19 Daniel 3.14-3.15
11 Yesu akamjibu, Wewe hungekuwa na mamlaka yo yote juu yangu, kama usingepewa kutoka juu; kwa hiyo yeye aliyenitia mikononi mwako yuna dhambi iliyo kubwa zaidi.
Romains 13.1 Genèse 45.7-45.8 Jean 3.27 Actes 2.23 Matthieu 27.2
12 Na tangu hapo Pilato akatafuta kumfungua; lakini Wayahudi wakapiga makelele wakisema, Ukimfungua huyu, wewe si rafiki yake Kaisari; kila mtu ajifanyaye kuwa mfalme humfitini Kaisari.
Jean 18.33-18.36 Actes 24.24-24.27 Marc 6.16-6.26 Actes 17.6-17.7 Luc 23.2-23.5
13 Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha.
Matthieu 27.19 Esaïe 57.11 Psaumes 94.20-94.21 Psaumes 58.1-58.2 Actes 4.19
14 Nayo ilikuwa Maandalio ya pasaka, yapata saa sita. Akawaambia Wayahudi, Tazama, Mfalme wenu!
Matthieu 27.62 Marc 15.25 Jean 19.42 Jean 19.5 Jean 19.31-19.32
15 Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulibishe! Pilato akawaambia, Je! Nimsulibishe mfalme wenu! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.
Luc 23.18 Actes 21.36 Ezéchiel 21.26-21.27 Genèse 49.10 Actes 22.22
16 Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.
Matthieu 27.26-27.31 Marc 15.15-15.20 Luc 23.24-23.25

Crucifixion et mort de Jésus

17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.
Luc 23.33 Luc 14.27 Luc 23.26 Marc 15.26 Luc 9.23
18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.
Esaïe 53.12 Marc 15.24-15.27 Galates 3.13 Matthieu 27.35-27.38 Luc 23.32-23.34
19 Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
Luc 23.38 Matthieu 27.37 Marc 15.26 Jean 19.14 Jean 1.45-1.46
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani.
Jean 19.13 Hébreux 13.12 Apocalypse 16.16 Actes 26.14 Apocalypse 9.11
21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.
Jean 19.14 Jean 19.19
22 Pilato akajibu, Niliyoandika nimeyaandika.
Esther 4.16 Proverbes 8.29 Jean 19.12 Psaumes 76.10 Genèse 43.14
23 Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.
Luc 23.34 Marc 15.24 Matthieu 27.35 Exode 39.22-39.23
24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari.
Psaumes 22.18 Jean 19.28 Jean 19.36-19.37 Jean 10.35 Esaïe 10.7
25 Na penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, Mariamu wa Klopa, na Mariamu Magdalene.
Luc 23.49 Matthieu 27.55-27.56 Marc 15.40-15.41 Luc 8.2 Luc 24.18
26 Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao.
Jean 13.23 Jean 2.4 Jean 21.7 Jean 20.2 Jean 21.24
27 Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.
1 Timothée 5.2-5.4 Matthieu 12.48-12.50 Jean 16.32 Jean 1.11 Marc 3.34
28 Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.
Psaumes 69.21 Psaumes 22.15 Jean 19.30 Luc 22.37 Jean 13.1
29 Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani.
Nombres 19.18 Luc 23.36 Matthieu 27.48 Marc 15.36 Exode 12.22
30 Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.
Jean 17.4 Philippiens 2.8 Marc 15.37 Colossiens 2.14-2.17 Luc 23.46
31 Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba siku ya sabato, (maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe, wakaondolewe.
Jean 19.14 Jean 19.42 Marc 15.42 Deutéronome 21.22-21.23 Josué 8.29
32 Basi askari wakaenda, wakamvunja miguu wa kwanza, na wa pili, aliyesulibiwa pamoja naye.
Jean 19.18 Luc 23.39-23.43
33 Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;
34 lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji.
1 Jean 5.8 1 Jean 5.6 Zacharie 13.1 Zacharie 12.10 Ezéchiel 36.25
35 Naye aliyeona ameshuhudia, na ushuhuda wake ni kweli; naye anajua ya kuwa anasema kweli ili ninyi nanyi mpate kusadiki.
Jean 21.24 Jean 15.27 1 Jean 1.1-1.3 Actes 10.39 Jean 20.31
36 Kwa maana hayo yalitukia ili andiko litimie, Hapana mfupa wake utakaovunjwa.
Psaumes 34.20 Nombres 9.12 Exode 12.46 Jean 19.28 Psaumes 35.10
37 Na tena andiko lingine lanena, Watamtazama yeye waliyemchoma.
Zacharie 12.10 Apocalypse 1.7 Psaumes 22.16-22.17

Mise au tombeau du corps de Jésus

38 Hata baada ya hayo Yusufu wa Arimathaya, naye ni mwanafunzi wa Yesu, (lakini kwa siri, kwa hofu ya Wayahudi), alimwomba Pilato ruhusa ili auondoe mwili wake Yesu. Na Pilato akampa ruhusa. Basi akaenda, akauondoa mwili wake.
Marc 15.42-15.47 Jean 7.13 Jean 12.42 Luc 23.50-23.56 Matthieu 27.57-27.61
39 Akaenda Nikodemo naye, (yule aliyemwendea usiku hapo kwanza), akaleta machanganyiko ya manemane na uudi, yapata ratli mia.
Cantique 4.14 Jean 7.50-7.52 2 Chroniques 16.14 Matthieu 19.30 Proverbes 7.17
40 Basi wakautwaa mwili wake Yesu, wakaufunga sanda ya kitani pamoja na yale manukato, kama ilivyo desturi ya Wayahudi katika kuzika.
Jean 11.44 Luc 24.12 Actes 5.6 Jean 20.5-20.7 Matthieu 26.12
41 Na pale pale aliposulibiwa palikuwa na bustani; na ndani ya bustani mna kaburi jipya, ambalo hajatiwa bado mtu ye yote ndani yake.
Luc 23.53 Jean 20.15 Matthieu 27.60 Matthieu 27.64-27.66 Esaïe 22.16
42 Humo basi, kwa sababu ya Maandalio ya Wayahudi, wakamweka Yesu; maana lile kaburi lilikuwa karibu.
Jean 19.31 Jean 19.14 Jean 19.41 Actes 13.29 Jean 19.20

Cette Bible est dans le domaine public.