Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 3.21
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jean-Baptiste

1 Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa liwali wa Uyahudi, na Herode mfalme wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania mfalme wa Abilene,
Matthieu 27.2 Luc 2.1 Luc 3.19 Matthieu 14.1 Actes 4.27
2 wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani.
Actes 4.6 Jean 18.24 Sophonie 1.1 Matthieu 26.3 Michée 1.1
3 Akafika nchi yote iliyo karibu na Yordani, akihubiri ubatizo wa toba liletalo ondoleo la dhambi,
Luc 1.77 Jean 1.28 Matthieu 3.11 Matthieu 3.5-3.6 Actes 22.16
4 kama ilivyoandikwa katika chuo cha maneno ya nabii Isaya; Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.
Esaïe 40.3-40.5 Jean 1.23 Jean 1.26-1.36 Matthieu 3.3 Jean 1.7
5 Kila bonde litajazwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patalainishwa;
Esaïe 42.16 Esaïe 49.11 Esaïe 40.4 Esaïe 45.2 Luc 1.51-1.53
6 Na wote wenye mwili watauona wokovu wa Mungu.
Esaïe 52.10 Esaïe 40.5 Psaumes 98.2-98.3 Romains 10.12 Marc 16.15
7 Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
Matthieu 23.33 1 Thessaloniciens 1.10 Matthieu 12.34 Actes 13.10 Hébreux 6.18
8 Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto.
Actes 26.20 Jean 8.33 Ezéchiel 18.27-18.31 Esaïe 1.16-1.18 Matthieu 21.43
9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Luc 13.9 Matthieu 7.19 Luc 13.7 Jean 15.6 Matthieu 3.10
10 Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?
Actes 2.37 Actes 16.30 Actes 9.6 Luc 3.12 Luc 3.8
11 Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo.
1 Timothée 6.18 Daniel 4.27 1 Jean 3.17 Luc 18.22 Jean 13.29
12 Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi?
Luc 7.29 Matthieu 21.31-21.32 Luc 15.1-15.2 Luc 18.13
13 Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa.
Luc 19.8 Esaïe 1.16-1.17 Psaumes 18.23 Matthieu 7.12 Proverbes 28.13
14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.
Philippiens 4.11 Exode 23.1 Exode 20.16 1 Timothée 6.8-6.10 Lévitique 19.11
15 Basi, watu walipokuwa wakingoja yatakayotokea, wote wakiwaza-waza mioyoni mwao habari za Yohana, kama labda yeye ndiye Kristo,
Jean 1.19-1.28 Jean 10.24 Jean 3.28-3.29
16 Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto;
Actes 1.5 Jean 1.26 Jean 1.33 Matthieu 3.11 Actes 19.4-19.5
17 ambaye pepeo lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake, na kuikusanya ngano ghalani mwake, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.
Matthieu 13.30 Esaïe 30.24 Psaumes 21.9-21.10 Matthieu 3.12 Michée 4.12
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi aliwahubiri watu.
Jean 1.15 Actes 2.40 Jean 1.34 Jean 3.29-3.36 Jean 1.29
19 Lakini mfalme Herode alipokaripiwa na yeye kwa ajili ya Herodia, mke wa nduguye, na maovu yote aliyoyafanya Herode,
Luc 3.1 Marc 6.17-6.18 Proverbes 15.12 Matthieu 14.3-14.4 Matthieu 11.2
20 aliongeza na hili juu ya yote, alimfunga Yohana gerezani.
Luc 13.31-13.34 Matthieu 23.31-23.33 Jean 3.24 Néhémie 9.26 2 Chroniques 24.17-24.22
21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;
Jean 1.32-1.34 Matthieu 3.13-3.17 Matthieu 14.23 Luc 5.16 Luc 9.18
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.
2 Pierre 1.17-1.18 Jean 1.32 Matthieu 17.5 Psaumes 2.7 Luc 9.34-9.35

Généalogie de Jésus

23 Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,
Matthieu 13.55 Actes 1.1 Matthieu 4.17 Jean 6.42 Luc 4.22
24 wa Mathati, wa Lawi, wa Melki, wa Yana, wa Yusufu,
25 wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
26 wa Maathi, wa Matathia, wa Semei, wa Yusufu, wa Yuda,
27 wa Yoana, wa Resa, wa Zerubabeli, wa Shealtieli, wa Neri,
Matthieu 1.12
28 wa Melki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
29 wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Mathati, wa Lawi,
30 wa Simeoni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliakimu,
31 wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa Nathani, wa Daudi,
1 Chroniques 3.5 2 Samuel 5.14 1 Chroniques 14.4 Zacharie 12.12
32 wa Yese, wa Obedi, wa Boazi, wa Salmoni, wa Nashoni,
Ruth 4.18-4.22 Matthieu 1.3-1.6 1 Chroniques 2.10-2.15 Actes 13.22-13.23 1 Samuel 20.31
33 wa Aminadabu, wa Aramu, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
Ruth 4.19-4.20 1 Chroniques 9.4 Nombres 26.20-26.21 Genèse 29.35 Genèse 38.29
34 wa Yakobo, wa Isaka, wa Ibrahimu, wa Tera, wa Nahori,
Genèse 25.26 Genèse 21.3 Josué 24.2 Matthieu 1.2 Actes 7.8
35 wa Serugi, wa Ragau, wa Pelegi, wa Eberi, wa Sala,
Genèse 11.12-11.21 Genèse 10.24-10.25
36 wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
Luc 17.27 2 Pierre 2.5 Genèse 9.18 Genèse 6.22-7.1 Genèse 11.10-11.26
37 wa Methusela, wa Henoko, wa Yaredi, wa Mahalaleli, wa Kenani,
Genèse 5.6-5.28 1 Chroniques 1.1-1.3
38 wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa Mungu.
Genèse 4.25-5.3 1 Corinthiens 15.45 Genèse 1.26-1.27 1 Corinthiens 15.47 Esaïe 64.8

Cette Bible est dans le domaine public.