Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 3.11
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jean-Baptiste

1 Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa liwali wa Uyahudi, na Herode mfalme wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania mfalme wa Abilene,
Matthieu 27.2 Actes 4.27 Luc 9.7 Luc 2.1 Luc 3.19
2 wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani.
Actes 4.6 Jean 18.24 Luc 1.80 Sophonie 1.1 Matthieu 26.3
3 Akafika nchi yote iliyo karibu na Yordani, akihubiri ubatizo wa toba liletalo ondoleo la dhambi,
Luc 1.77 Actes 19.4 Jean 3.26 Marc 1.4-1.5 Jean 1.31-1.33
4 kama ilivyoandikwa katika chuo cha maneno ya nabii Isaya; Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.
Jean 1.23 Esaïe 40.3-40.5 Malachie 4.6 Marc 1.3 Esaïe 57.14
5 Kila bonde litajazwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patalainishwa;
Esaïe 42.16 Esaïe 49.11 Esaïe 40.4 Esaïe 45.2 Ezéchiel 17.24
6 Na wote wenye mwili watauona wokovu wa Mungu.
Esaïe 52.10 Esaïe 40.5 Psaumes 98.2-98.3 Luc 2.30-2.32 Luc 2.10-2.11
7 Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
Matthieu 23.33 1 Thessaloniciens 1.10 Matthieu 12.34 Genèse 3.15 Jean 8.44
8 Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto.
Actes 26.20 Esaïe 1.16-1.18 Jean 8.33 Ezéchiel 18.27-18.31 Romains 4.16
9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Luc 13.9 Matthieu 7.19 Matthieu 3.10 Luc 13.7 Jean 15.6
10 Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?
Actes 2.37 Actes 16.30 Actes 9.6 Luc 3.12 Luc 3.8
11 Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo.
1 Jean 3.17 Luc 18.22 1 Timothée 6.18 Daniel 4.27 Actes 10.4
12 Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi?
Luc 7.29 Matthieu 21.31-21.32 Luc 15.1-15.2 Luc 18.13
13 Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa.
Luc 19.8 1 Corinthiens 6.10 Tite 2.11-2.12 Esaïe 55.6-55.7 Ephésiens 4.28
14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.
Exode 23.1 Philippiens 4.11 Hébreux 13.5-13.6 Exode 20.16 1 Timothée 6.8-6.10
15 Basi, watu walipokuwa wakingoja yatakayotokea, wote wakiwaza-waza mioyoni mwao habari za Yohana, kama labda yeye ndiye Kristo,
Jean 1.19-1.28 Jean 10.24 Jean 3.28-3.29
16 Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto;
Actes 1.5 Jean 1.26 Jean 1.33 Matthieu 3.11 1 Corinthiens 12.13
17 ambaye pepeo lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake, na kuikusanya ngano ghalani mwake, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.
Matthieu 13.30 Esaïe 30.24 Marc 9.43-9.49 Jérémie 15.7 Psaumes 21.9-21.10
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi aliwahubiri watu.
Jean 1.15 Actes 2.40 Jean 1.34 Jean 3.29-3.36 Jean 1.29
19 Lakini mfalme Herode alipokaripiwa na yeye kwa ajili ya Herodia, mke wa nduguye, na maovu yote aliyoyafanya Herode,
Luc 3.1 Marc 6.17-6.18 Proverbes 9.7-9.8 Proverbes 15.12 Matthieu 14.3-14.4
20 aliongeza na hili juu ya yote, alimfunga Yohana gerezani.
1 Thessaloniciens 2.15-2.16 2 Rois 24.4 Matthieu 21.35-21.41 Jérémie 2.30 Matthieu 22.6-22.7
21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;
Jean 1.32-1.34 Matthieu 3.13-3.17 Jean 12.27-12.28 Marc 1.9-1.11 Matthieu 14.23
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.
2 Pierre 1.17-1.18 Jean 1.32 Matthieu 17.5 Psaumes 2.7 Luc 9.34-9.35

Généalogie de Jésus

23 Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,
Matthieu 13.55 Nombres 4.3 Matthieu 1.16 Marc 6.3 Actes 1.1
24 wa Mathati, wa Lawi, wa Melki, wa Yana, wa Yusufu,
25 wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
26 wa Maathi, wa Matathia, wa Semei, wa Yusufu, wa Yuda,
27 wa Yoana, wa Resa, wa Zerubabeli, wa Shealtieli, wa Neri,
Matthieu 1.12
28 wa Melki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
29 wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Mathati, wa Lawi,
30 wa Simeoni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliakimu,
31 wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa Nathani, wa Daudi,
1 Chroniques 3.5 2 Samuel 5.14 1 Chroniques 14.4 Zacharie 12.12
32 wa Yese, wa Obedi, wa Boazi, wa Salmoni, wa Nashoni,
Matthieu 1.3-1.6 1 Chroniques 2.10-2.15 Ruth 4.18-4.22 1 Rois 12.16 Nombres 2.3
33 wa Aminadabu, wa Aramu, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
Ruth 4.19-4.20 Matthieu 1.2-1.4 Genèse 46.12 1 Chroniques 2.9-2.10 Ruth 4.12
34 wa Yakobo, wa Isaka, wa Ibrahimu, wa Tera, wa Nahori,
Genèse 21.3 Genèse 25.26 1 Chroniques 1.24-1.28 1 Chroniques 1.34 Josué 24.2
35 wa Serugi, wa Ragau, wa Pelegi, wa Eberi, wa Sala,
Genèse 11.12-11.21 Genèse 10.24-10.25
36 wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
Genèse 8.1 Genèse 9.1 Genèse 9.26-9.27 1 Pierre 3.20 Genèse 5.28-5.32
37 wa Methusela, wa Henoko, wa Yaredi, wa Mahalaleli, wa Kenani,
Genèse 5.6-5.28 1 Chroniques 1.1-1.3
38 wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa Mungu.
Genèse 4.25-5.3 Genèse 2.7 1 Corinthiens 15.45 Genèse 1.26-1.27 1 Corinthiens 15.47

Cette Bible est dans le domaine public.