Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 20.26
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa siku moja, alipokuwa akiwafundisha watu hekaluni, na kuihubiri habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wazee walimtokea ghafula;
Actes 4.1 Actes 6.12 Matthieu 21.23-21.27 Luc 8.1 Matthieu 26.55
2 wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?
Jean 2.18 Exode 2.14 Marc 11.28-11.33 Matthieu 21.23-21.27 Actes 7.27
3 Akajibu akawaambia, Nami nitawauliza ninyi neno moja; niambieni,
Matthieu 15.2-15.3 Colossiens 4.6 Luc 22.68
4 Ubatizo wa Yohana, je! Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?
Luc 15.18 Jean 1.19-1.28 Matthieu 21.25-21.32 Matthieu 11.7-11.19 Jean 1.6
5 Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema ulitoka mbinguni, atasema, Basi, mbona hamkumwamini?
Jean 1.30 Jean 3.36 Jean 5.33-5.35 Jean 1.15-1.18 Jean 1.34
6 Na tukisema ulitoka kwa wanadamu, watu wote watatupiga kwa mawe, kwa kuwa wamemkubali Yohana kuwa ni nabii.
Matthieu 21.26 Matthieu 11.9 Luc 7.26-7.29 Jean 10.41 Marc 12.12
7 Wakajibu, kwamba, Hatujui ulikotoka.
2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Esaïe 29.14 2 Timothée 3.8-3.9 Jean 9.39 Malachie 2.7-2.9
8 Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.
Luc 22.68 Matthieu 16.4 Proverbes 26.4-26.5 Marc 11.33 Matthieu 15.14

Parabole des vignerons

9 Akaanza kuwaambia watu mfano huu; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu; akapangisha wakulima, akaenda akakaa katika nchi nyingine muda mrefu.
Matthieu 21.33-21.46 Marc 12.1-12.12 Cantique 8.11-8.12 Esaïe 5.1-5.7 Psaumes 80.8-80.14
10 Na wakati wa mavuno alituma mtumwa kwa wale wakulima ili wampe baadhi ya matunda ya mizabibu; wakulima wakampiga wakamfukuza mikono mitupu.
2 Chroniques 36.15-36.16 Matthieu 21.34-21.36 Néhémie 9.26 Romains 7.4 Jérémie 20.2
11 Akatuma na mtumwa mwingine. Wakampiga huyu naye, wakamwaibisha wakamfukuza mikono mitupu.
1 Thessaloniciens 2.2 Hébreux 11.36-11.37 Matthieu 23.30-23.37 Actes 7.52 Osée 10.1
12 Akamtuma na wa tatu; huyu naye wakamtia jeraha, wakamtupa nje.
13 Basi, bwana wa shamba la mizabibu alisema, Nifanyeje? Nitamtuma mwanangu, mpendwa wangu; yamkini watamheshimu yeye.
Matthieu 3.17 Jean 3.16-3.17 Jérémie 36.3 Jérémie 36.7 Luc 9.35
14 Lakini, wale wakulima walipomwona, walishauriana wao kwa wao, wakisema, Huyu ndiye mrithi; haya, na tumwue, ili urithi uwe wetu.
Romains 8.17 Hébreux 1.2 Actes 2.23 Luc 19.47 Matthieu 27.21-27.25
15 Wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi, bwana wa shamba la mizabibu atawatendeje?
Hébreux 13.12 Matthieu 21.37-21.40 Marc 12.6-12.9
16 Atakuja na kuwaangamiza wakulima wale, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. Waliposikia hayo walisema, Hasha! Yasitukie haya!
Luc 19.27 Matthieu 21.41 Actes 13.46 Psaumes 21.8-21.10 Psaumes 2.8-2.9
17 Akawakazia macho akasema, Maana yake nini basi neno hili lililoandikwa, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni?
Psaumes 118.22 Actes 4.11 Esaïe 28.16 Marc 3.5 Luc 22.37
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; na ye yote ambaye litamwangukia litamsaga kabisa.
Esaïe 8.14-8.15 Daniel 2.34-2.35 Daniel 2.44-2.45 Matthieu 21.44 1 Thessaloniciens 2.16
19 Nao waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta kumkamata saa iyo hiyo, wakawaogopa watu, maana walitambua ya kwamba mfano huu amewanenea wao.
Luc 19.47-19.48 Marc 12.12 Luc 20.14 Matthieu 21.45-21.46 Matthieu 26.3-26.4

Tentatives de piéger Jésus

20 Wakamvizia-vizia, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wamnase katika maneno yake, wapate kumtia katika enzi na mamlaka ya liwali.
Matthieu 27.2 Luc 20.26 Jérémie 20.10 Psaumes 81.15 2 Samuel 14.2
21 Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli.
Matthieu 22.16 1 Thessaloniciens 2.4-2.5 Marc 12.14 Galates 2.6 Galates 1.10
22 Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?
Esdras 4.19-4.22 Actes 5.37 Néhémie 5.4 Esdras 4.13 Néhémie 9.37
23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,
1 Corinthiens 3.19 Luc 6.8 Psaumes 95.9 1 Corinthiens 10.9 Luc 20.20
24 Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.
Matthieu 18.28 Luc 23.2 Actes 11.28 Actes 26.32 Luc 20.22
25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.
Matthieu 22.21 Romains 13.6-13.7 Proverbes 24.21 Matthieu 17.27 Actes 4.19-4.20
26 Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa.
Luc 20.20 Matthieu 22.12 Matthieu 22.34 Tite 1.10 Proverbes 26.4-26.5
27 Kisha baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale wasemao ya kwamba hakuna ufufuo, wakamwuliza,
Matthieu 22.23-22.33 Marc 12.18-12.27 1 Corinthiens 15.12 Actes 4.1-4.2 Actes 5.17
28 wakisema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kuwa, mtu akifiwa na ndugu yake mwenye mke, lakini hana mtoto na amtwae huyu mke, ampatie ndugu yake mzao.
Deutéronome 25.5-25.10 Genèse 38.26 Genèse 38.11 Ruth 1.11-1.12 Genèse 38.8
29 Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mke, akafa hana mtoto;
Jérémie 22.30 Lévitique 20.20
30 na wa pili [akamtwaa yule mke, akafa hana mtoto;]
31 hata wa tatu akamwoa, na kadhalika wote saba, wakafa, wasiache watoto.
32 Mwisho akafa yule mke naye.
Hébreux 9.27 Juges 2.10 Ecclésiaste 9.5 Ecclésiaste 1.4
33 Basi, katika ufufuo atakuwa mke wa yupi? Maana aliolewa na wote saba.
Matthieu 22.24-22.28 Marc 12.19-12.23
34 Yesu akawaambia, Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa;
Luc 16.8 Luc 17.27 Ephésiens 5.31 1 Corinthiens 7.2-7.16 Hébreux 13.4
35 lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi;
Daniel 12.2-12.3 2 Thessaloniciens 1.5 Actes 5.41 Jean 5.29 Actes 24.15
36 wala hawawezi kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile walivyo wana wa ufufuo.
Matthieu 22.30 Apocalypse 21.4 Apocalypse 7.9-7.12 Apocalypse 22.9 1 Corinthiens 15.26
37 Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.
Exode 3.2-3.6 Genèse 28.21 Actes 7.30-7.32 Exode 3.15 Marc 12.26-12.27
38 Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.
Jean 11.25-11.26 Colossiens 3.3-3.4 Romains 6.10-6.11 Hébreux 11.16 Apocalypse 7.15-7.17
39 Waandishi wengine wakajibu wakamwambia, Mwalimu, umesema vema;
Actes 23.9 Matthieu 22.34-22.40 Marc 12.28-12.34
40 wala hawakuthubutu kumwuliza neno baada ya hayo.
Matthieu 22.46 Marc 12.34 Proverbes 26.5

Reproches de Jésus aux chefs religieux

41 Akawaambia, Wasemaje watu kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?
Marc 12.35-12.37 Matthieu 1.1 Jean 7.42 Matthieu 22.41-22.45 Jérémie 23.5-23.6
42 Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume,
Psaumes 110.1 1 Corinthiens 15.25 Actes 2.34-2.35 Hébreux 1.13 Actes 13.33-13.35
43 Hata niwaweke adui zako Kuwa kiti cha kuwekea miguu yako.
Psaumes 110.1 Psaumes 21.8-21.12 Apocalypse 19.14-19.21 Luc 19.27 Psaumes 72.9
44 Basi Daudi amwita Bwana; amekuwaje mwana wake?
Apocalypse 22.16 Galates 4.4 Romains 9.5 Luc 2.11 Luc 1.31-1.35
45 Na watu wote walipokuwa wakimsikiliza, aliwaambia wanafunzi wake,
Matthieu 23.5-23.7 Matthieu 15.10 Marc 8.34 1 Timothée 5.20 Marc 12.38-12.39
46 Jilindeni na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele karamuni.
Luc 11.43 Luc 14.7 Marc 8.15 2 Timothée 4.15 Luc 12.1
47 Wanakula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu. Hao watapata hukumu iliyo kuu.
Marc 12.40 Ezéchiel 33.31 Jacques 3.1 Luc 10.12-10.14 Michée 2.2

Cette Bible est dans le domaine public.