Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 4.20
Bible en Swahili de l’est


Tentation de Jésus-Christ

1 Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
Hébreux 2.18 Marc 1.12-1.15 Luc 4.1-4.13 Ezéchiel 43.5 Jean 14.30
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
Exode 34.28 1 Rois 19.8 Deutéronome 9.18 Jean 4.6 Deutéronome 9.9
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
1 Thessaloniciens 3.5 Luc 22.31-22.32 Job 1.9-1.12 Nombres 11.4-11.6 Genèse 3.1-3.5
4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
Deutéronome 8.3 Luc 4.4 Romains 15.4 Jean 6.31-6.59 Jean 6.63
5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,
Matthieu 27.53 Néhémie 11.1 Luc 4.9 Esaïe 48.2 Esaïe 52.1
6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
Psaumes 91.11-91.12 Hébreux 1.14 2 Corinthiens 11.14 Job 1.10 Job 5.23
7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Deutéronome 6.16 1 Corinthiens 10.9 Psaumes 78.18 Psaumes 78.41 Hébreux 3.9
8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
1 Jean 2.15-2.16 Matthieu 16.26 Apocalypse 11.15 Luc 4.5-4.7 1 Pierre 1.24
9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
Daniel 5.18-5.19 Apocalypse 19.10 2 Corinthiens 4.4 Daniel 2.37-2.38 Jean 16.11
10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Deutéronome 10.20 Deutéronome 6.13-6.14 Zacharie 3.1-3.2 Job 2.1 Josué 24.14
11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.
Matthieu 26.53 Luc 22.43 Hébreux 1.14 Apocalypse 5.11-5.12 Matthieu 4.6

Début du ministère de Jésus

12 Basi Yesu aliposikia ya kwamba Yohana amefungwa, alikwenda zake mpaka Galilaya;
Marc 1.14 Luc 4.14 Luc 3.20 Matthieu 14.3 Luc 4.31
13 akatoka Nazareti, akaja akakaa Kapernaumu, mji ulioko pwani, mipakani mwa Zabuloni na Naftali;
Marc 1.21 Jean 4.46 Matthieu 11.23 Josué 19.10-19.16 Jean 2.12
14 ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,
Matthieu 1.22 Jean 19.36-19.37 Matthieu 8.17 Jean 15.25 Esaïe 9.1-9.2
15 Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, Njia ya bahari, ng’ambo ya Yordani, Galilaya ya mataifa,
Esaïe 9.1 Josué 21.32 2 Rois 15.29 1 Rois 9.11 Josué 20.7
16 Watu wale waliokaa katika giza Wameona mwanga mkuu, Nao waliokaa katika nchi na uvuli wa mauti Mwanga umewazukia.
Esaïe 9.2 Luc 2.32 Amos 5.8 Job 3.5 Esaïe 60.1-60.3
17 Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
Actes 2.38 Matthieu 3.2 Marc 1.14-1.15 Luc 24.47 Actes 17.30
18 Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.
Jean 1.40-1.42 Matthieu 10.2 Matthieu 15.29 Luc 6.14 Matthieu 1.16-1.18
19 Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Marc 1.17-1.18 Jean 12.26 Matthieu 16.24 Luc 9.59 Luc 5.27
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Marc 10.28-10.31 1 Rois 19.21 Matthieu 10.37 Psaumes 119.60 Luc 18.28-18.30
21 Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita.
Matthieu 10.2 Actes 12.2 Marc 1.19-1.20 Matthieu 26.37 Marc 3.17
22 Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata.
Matthieu 10.37 Luc 14.26 Deutéronome 33.9-33.10 Luc 9.59-9.60 Luc 14.33
23 Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu.
Matthieu 9.35 Marc 1.21 Matthieu 13.54 Marc 1.39 Marc 1.14
24 Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa hawawezi, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya.
Matthieu 17.15 Matthieu 8.6 Luc 2.2 Matthieu 15.22 Actes 15.23
25 Na makutano mengi wakamfuata, kutoka Galilaya, na Dekapoli, na Yerusalemu, na Uyahudi, na ng’ambo ya Yordani
Luc 6.17 Marc 5.20 Marc 7.31 Marc 3.7-3.8 Luc 6.19

Cette Bible est dans le domaine public.