Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 19.8
Bible en Swahili de l’est


La vache rousse et l’eau de purification

1 Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
2 Hii ndiyo amri ya sheria Bwana aliyoagiza, akisema, Waambie wana wa Israeli wakuletee ng’ombe mke mwekundu asiye na kipaku, mkamilifu, ambaye hajatiwa nira bado;
Deutéronome 21.3 1 Samuel 6.7 Lévitique 22.20-22.25 Lamentations 1.14 Philippiens 2.6-2.8
3 nanyi mtamleta kwa Eleazari kuhani, naye atakwenda naye nje ya kambi, na mtu mmoja atamchinja mbele yake;
Lévitique 4.12 Lévitique 4.21 Lévitique 13.45-13.46 Nombres 3.4 Nombres 15.36
4 kisha Eleazari kuhani atatwaa katika damu yake kwa kidole chake, na kuinyunyiza damu yake kuelekea upande wa mbele wa hema ya kukutania mara saba;
Lévitique 4.17 Lévitique 4.6 Lévitique 16.14 Lévitique 16.19 Hébreux 9.13-9.14
5 kisha mtu mmoja atamchoma moto huyo ng’ombe mbele yake; ngozi yake, na nyama yake, na damu yake, pamoja na mavi yake pia atachoma moto;
Exode 29.14 Lévitique 4.11-4.12 Psaumes 22.14 Lévitique 4.21 Esaïe 53.10
6 kisha kuhani atatwaa mti wa mwerezi, na hisopo, na sufu nyekundu, na kuvitupa katika huo moto unaomchoma ng’ombe.
Lévitique 14.4 Lévitique 14.49 Lévitique 14.6 Psaumes 51.7 Hébreux 9.19-9.23
7 Ndipo kuhani atazifua nguo zake, na kuoga mwili wake majini, kisha baadaye ataingia kambini, naye kuhani atakuwa najisi hata jioni.
Lévitique 11.25 Lévitique 11.40 Lévitique 16.26-16.28 Nombres 19.19 Lévitique 14.8-14.9
8 Na huyo aliyemchoma moto ng’ombe atazifua nguo zake majini, na kuoga mwili wake majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
9 Kisha mtu mmoja aliye safi atayazoa majivu ya huyo ng’ombe, na kuyaweka yawe akiba katika mahali safi nje ya kambi, nayo yatatunzwa kwa ajili ya mkutano wa wana wa israeli, kuwa ndiyo maji ya farakano; ni sadaka ya dhambi.
Hébreux 9.13 Nombres 19.13 Nombres 19.20-19.21 Hébreux 7.26 Nombres 8.7
10 Na yeye ayazoaye majivu ya huyo ng’ombe atazifua nguo zake, naye atakuwa najisi hata jioni; na jambo hili litakuwa amri ya milele, kwa wana wa Israeli, na wa mgeni akaaye kati yao.
Colossiens 3.11 Nombres 15.15-15.16 Romains 3.29-3.30 Nombres 19.19 Nombres 19.7-19.8
11 Mtu agusaye maiti ye yote atakuwa najisi muda wa siku saba;
Nombres 5.2 Nombres 31.19 Lévitique 21.1 Nombres 9.6 Lévitique 21.11
12 naye atajitakasa kwa yale maji siku ya tatu, na siku ya saba atakuwa safi; lakini kama hajitakasi siku ya tatu, ndipo na siku ya saba hatakuwa safi.
Nombres 31.19 Exode 19.15 Actes 15.9 Apocalypse 7.14 1 Corinthiens 15.3-15.4
13 Mtu awaye yote agusaye maiti wa mtu aliyekufa, asijitakase, yuatia unajisi maskani ya Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na Israeli; maana, hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake, atakuwa najisi; unajisi wake ukali juu yake bado.
Lévitique 15.31 Lévitique 22.3 Lévitique 7.20 Nombres 19.20 Nombres 8.7
14 Hii ndiyo amri, mtu afapo ndani ya hema; kila mtu aingiaye ndani ya hema hiyo, na kila mtu aliye humo hemani, atakuwa najisi muda wa siku saba.
15 Na kila chombo kilicho wazi, kisichofungwa na kifuniko, ni najisi.
Nombres 31.20 Lévitique 11.32 Lévitique 14.36
16 Kisha mtu ye yote huko nje shambani atakayemgusa mtu aliyeuawa kwa upanga, au mzoga, au mfupa wa mtu, au kaburi, atakuwa najisi muda wa siku saba.
Matthieu 23.27 Nombres 31.19 Luc 11.44 Nombres 19.11 Ezéchiel 39.11-39.16
17 Na kwa huyo aliye najisi watatwaa katika majivu ya kuchomwa kwake hiyo sadaka ya dhambi, na maji ya mtoni yatachanganywa na majivu katika chombo;
Jean 7.38 Apocalypse 7.17 Nombres 19.9 Cantique 4.15 Jean 4.10-4.11
18 kisha mtu mmoja aliye safi atatwaa hisopo, na kuitia katika hayo maji naye atayanyunyiza juu ya hema, na juu ya vyombo vyote, na juu ya watu waliokuwapo, na juu yake yeye aliyeugusa mfupa, au mtu aliyeuawa, au mzoga, au kaburi;
Hébreux 9.14 Psaumes 51.7 Jean 17.19 Jean 17.17 Jean 15.2-15.3
19 na yule aliye safi atamnyunyiza huyo aliye najisi siku ya tatu, na siku ya saba; na katika siku ya saba atamtakasa; naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa safi jioni.
Nombres 19.12 Lévitique 14.9 Nombres 31.19 Hébreux 10.22 Genèse 2.2
20 Lakini mtu atakayekuwa najisi, naye hataki kujitakasa, mtu huyo atakatiliwa mbali katika mkutano, kwa sababu amepatia unajisi mahali patakatifu pa Bwana; hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake; yeye yu najisi.
Genèse 17.14 Nombres 19.13 Nombres 15.30 Actes 13.39-13.41 2 Pierre 3.14
21 Nayo itakuwa amri ya sikuzote kwao; na yeye anyunyizaye maji ya farakano atazifua nguo zake; naye ayagusaye hayo maji ya farakano atakuwa najisi hata jioni.
Hébreux 7.19 Hébreux 9.10 Hébreux 10.4 Lévitique 11.40 Lévitique 16.26-16.28
22 Na kitu cho chote atakachokigusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi; na mtu atakayekigusa kitu hicho atakuwa najisi hata jioni.
Aggée 2.13 Marc 7.21-7.23 Matthieu 15.19-15.20 Lévitique 15.5 Lévitique 7.19

Cette Bible est dans le domaine public.