Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 8.18
Bible en Swahili de l’est


Entrée en fonction des prêtres

Consécration d’Aaron et de ses fils

1 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Mtwae Haruni, na wanawe pamoja naye, na yale mavazi, na mafuta ya kutia, na ng’ombe mume wa sadaka ya dhambi, na kondoo waume wawili, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu;
Exode 28.2-28.4 Exode 39.1-39.31 Exode 30.23-30.37 Hébreux 7.27 Exode 28.40-29.4
3 kisha ukutanishe mkutano wote hapo mlangoni pa hema ya kukutania.
Nombres 21.16 Actes 2.1 2 Chroniques 5.6 1 Chroniques 15.3 1 Chroniques 13.5
4 Basi Musa akafanya kama alivyoambiwa na Bwana; na huo mkutano ulikutanishwa mlangoni pa hema ya kukutania.
Matthieu 28.20 Exode 39.7 1 Corinthiens 11.23 Lévitique 8.17 Exode 39.5
5 Musa akawaambia mkutano, Neno aliloliagiza Bwana kwamba lifanywe, ni hili.
Exode 29.4-29.37
6 Basi Musa akawaleta Haruni na wanawe, akawaosha kwa maji.
1 Corinthiens 6.11 Ephésiens 5.26 Exode 29.4 Hébreux 10.22 Psaumes 51.7
7 Kisha akamvika Haruni ile kanzu, na kumfunga mshipi, na kumvika joho, na kumvika naivera, na kumfunga huo mshipi wa kazi ya mstadi wa naivera na kumfunga naivera kwa huo mshipi.
Exode 28.4 Esaïe 61.3 Romains 3.22 Exode 39.1-39.7 Romains 13.14
8 Kisha akamtia kile kifuko cha kifuani; akatia hizo Urimu na Thumimu katika hicho kifuko cha kifuani.
Esdras 2.63 Exode 39.8-39.21 Esaïe 59.17 Exode 28.15-28.30 Cantique 8.6
9 Akamvika na kile kilemba kichwani mwake; na juu ya kilemba, upande wa mbele, akakitia kile kipande cha dhahabu, hiyo taji takatifu; kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Philippiens 2.9-2.11 Zacharie 3.5 Exode 28.4 Exode 39.28-39.30 Exode 28.36-28.38
10 Kisha Musa akatwaa hayo mafuta matakatifu ya kutia, akatia mafuta maskani, na vyote vilivyokuwamo, na kuvitakasa.
Exode 30.23-30.29 Lévitique 8.2 Exode 40.9-40.11
11 Kisha akanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kuitia mafuta madhabahu na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake, ili kuvitakasa.
Exode 4.17 Exode 30.29 Exode 4.6 Ezéchiel 36.25 Exode 16.19
12 Kisha akamimina mafuta hayo ya kutia kichwani mwake Haruni, na kumtia mafuta, ili amtakase.
Exode 30.30 Psaumes 133.2 Exode 29.7 Exode 28.41 Lévitique 4.3
13 Kisha Musa akawaleta wana wa Haruni, na kuwavika kanzu, na kuwafunga mishipi, na kuwavika vilemba; kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Exode 29.8-29.9 Apocalypse 1.6 Psaumes 132.9 Esaïe 61.10 Exode 40.14-40.15
14 Kisha akamleta yule ng’ombe mume wa sadaka ya dhambi; na Haruni na wanawe wakaweka mikono yao katika kichwa cha huyo ng’ombe wa sadaka ya dhambi.
Ezéchiel 43.19 1 Pierre 3.18 Lévitique 8.2 Esaïe 53.10 Hébreux 7.26-7.28
15 Kisha akamchinja; na Musa akaitwaa damu yake, akaitia katika pembe za madhabahu pande zote kwa kidole chake, akaitakasa madhabahu, kisha akaimwaga hiyo damu hapo chini ya madhabahu, na kuitakasa, ili afanye upatanisho kwa ajili yake.
Lévitique 4.7 2 Corinthiens 5.18-5.21 Daniel 9.24 2 Chroniques 29.24 Lévitique 4.30
16 Kisha akayatwaa mafuta yote yaliyokuwa katika matumbo yake, na kitambi kilichokuwa katika ini, na figo zake mbili, na mafuta yake, na Musa akayateketeza juu ya madhabahu.
Exode 29.13 Lévitique 4.8-4.9 Lévitique 3.3-3.5
17 Lakini huyo ng’ombe mwenyewe, na ngozi yake, na nyama yake, na mavi yake, akayachoma moto nje ya marago; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Lévitique 4.11-4.12 Exode 29.14 Lévitique 16.27 Hébreux 13.11-13.13 Lévitique 6.30
18 Kisha akamsongeza yule kondoo mume wa sadaka ya kuteketezwa; na Haruni na wanawe wakaweka mikono yao kichwani mwa huyo kondoo.
Lévitique 8.2 Lévitique 1.4-1.13 Exode 29.15-29.18
19 Kisha akamchinja; na Musa akainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote.
20 Kisha akamkata kondoo vipande vyake; na Musa akateketeza kichwa, na vile vipande, na mafuta.
Lévitique 1.8
21 Kisha akayaosha matumbo na miguu yake kwa maji; na Musa akamteketeza huyo kondoo wote juu ya madhabahu; ilikuwa ni sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu ya kupendeza; ilikuwa ni sadaka iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto; kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Exode 29.18 Lévitique 1.17 Lévitique 2.9 Ephésiens 5.2 Genèse 8.21
22 Kisha akamsongeza kondoo mume wa pili, huyo kondoo wa kuwaweka wakfu; na Haruni na wanawe wakaweka mikono yao kichwani mwa huyo kondoo.
Lévitique 8.2 Jean 17.19 Ephésiens 5.27 Lévitique 8.29 Apocalypse 1.5-1.6
23 Kisha akamchinja; na Musa akatwaa katika damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la kuume la Haruni, na katika chanda chake cha gumba cha mkono wake wa kuume, na katika kidole cha gumba cha guu lake la kuume.
Exode 29.20 Lévitique 14.14 Lévitique 14.17 Lévitique 14.28 Philippiens 1.20
24 Kisha akawaleta wana wa Haruni, na Musa akaitia hiyo damu katika ncha za masikio ya kuume, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vya gumba vya maguu yao ya kuume; kisha Musa akainyunyiza hiyo damu katika madhabahu pande zote.
Hébreux 9.18-9.22
25 Kisha akayatwaa hayo mafuta, na mkia wenye mafuta, na mafuta yote yaliyokuwa katika matumbo, na kitambi cha ini, na figo mbili, na mafuta yake, na mguu wa nyuma wa upande wa kuume;
Proverbes 23.26 Exode 29.22-29.25 Lévitique 3.3-3.5 Lévitique 3.9 Esaïe 53.10
26 kisha katika kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichokuwa pale mbele za Bwana, akatwaa mkate mmoja usiochachwa, na mkate mmoja ulioandaliwa na mafuta na kaki moja nyembamba, akaiweka juu ya mafuta, na juu ya huo mguu wa nyuma wa upande wa kuume;
Exode 29.23 Actes 5.12 1 Timothée 2.5 Jean 1.14
27 kisha akaweka vyote katika mikono ya Haruni, na katika mikono ya wanawe, na kuvitikisa huku na huku viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana.
Jérémie 30.21 Hébreux 9.14 Lévitique 7.30-7.31 Exode 29.24-29.37
28 Kisha Musa akavitwaa tena mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya hiyo sadaka ya kuteketezwa vilikuwa vya kuwaweka wakfu, ni harufu nzuri; ilikuwa dhabihu iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto.
Exode 29.25 Psaumes 22.13-22.14 Zacharie 13.7 Hébreux 10.14-10.22
29 Kisha Musa akakitwaa kile kidari, akakitikisa huku na huku, kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana; ni sehemu ya Musa katika huyo kondoo mume wa kuwaweka wakfu; kama Bwana alivyomwagiza Musa.
1 Pierre 4.11 Lévitique 7.30-7.34 Esaïe 66.20 1 Corinthiens 10.31 Exode 29.26-29.27
30 Kisha Musa akatwaa baadhi ya mafuta ya kutia, na ya damu iliyokuwa pale juu ya madhabahu, na kumnyunyizia Haruni, katika mavazi yake, na wanawe, katika mavazi yao, pamoja naye; akamtakasa Haruni, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
Nombres 3.3 Exode 30.30 Exode 29.21 1 Pierre 1.2 1 Jean 2.27
31 Kisha Musa akawaambia huyo Haruni na wanawe, Tokoseni hiyo nyama mlangoni pa hema ya kukutania; mkaile pale pale, na hiyo mikate iliyo katika kile kikapu cha kuwaweka wakfu, kama nilivyoagizwa kusema, Haruni na wanawe wataila.
Exode 29.31-29.32 Jean 6.53-6.56 Lévitique 7.15 Lévitique 6.28 1 Samuel 2.13-2.17
32 Nacho kitakachosalia katika hiyo nyama na mikate mtakichoma moto.
Exode 29.34 Proverbes 27.1 2 Corinthiens 6.2 Ecclésiaste 9.10 Lévitique 7.17
33 Wala msitoke nje mlangoni pa hema ya kukutania muda wa siku saba, hata siku za kuwekwa wakfu kwenu zitakapotimia; kwa kuwa atawaweka muda wa siku saba.
Exode 29.35 Exode 29.30 Nombres 19.12 Lévitique 14.8 Ezéchiel 43.25-43.27
34 Vile vile kama vilivyotendeka siku ya leo, ni vivyo Bwana alivyoagiza kufanywa, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Hébreux 7.16 Hébreux 7.27 Hébreux 10.11-10.12
35 Nanyi mtakaa mlangoni pa hema ya kukutania muda wa siku saba mchana na usiku, na kuulinda ulinzi wa Bwana ili kwamba msife; kwani ndivyo nilivyoagizwa.
Nombres 3.7 1 Rois 2.3 Deutéronome 11.1 Nombres 9.19 2 Corinthiens 7.1
36 Basi Haruni na wanawe wakafanya mambo hayo yote Bwana aliyoyaagiza kwa mkono wa Musa.
Deutéronome 12.32 Deutéronome 4.2 1 Samuel 15.22 Exode 40.16 Exode 39.43

Cette Bible est dans le domaine public.