Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 22.23
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Nena na Haruni na wanawe, ili wajitenge wenyewe na vitu vitakatifu vya wana wa Israeli ambavyo wanitakasia mimi, tena kwamba wasilinajisi jina langu takatifu; mimi ndimi Bwana.
Deutéronome 15.19 Lévitique 18.21 Exode 28.38 Lévitique 22.32 Lévitique 19.12
3 Waambie, Mtu ye yote wa kizazi chenu chote katika vizazi vyenu, atakayevikaribia vile vitu vitakatifu, ambavyo wana wa Israeli wamtakasia Bwana, naye ana unajisi, mtu huyo atakatiliwa mbali asiwe mbele zangu; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 7.20-7.21 Psaumes 51.11 Psaumes 16.11 Matthieu 25.41 2 Thessaloniciens 1.9
4 Mtu ye yote wa kizazi cha Haruni aliye mwenye ukoma, au mwenye kisonono; yeye asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena mtu awaye yote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu ambaye shahawa humtoka;
Lévitique 11.39 Lévitique 15.2-15.3 Lévitique 15.13-15.16 Lévitique 21.1 Nombres 18.19
5 au mtu amgusaye mnyama atambaaye, wa kumpatia unajisi, au kwamba amgusa mtu wa kumpatia unajisi, kwa unajisi wo wote alio nao;
Lévitique 15.7 Lévitique 11.43-11.44 Lévitique 15.19 Lévitique 11.24-11.28
6 huyo mtu atakayegusa kitu cho chote namna hiyo atakuwa najisi hata jioni, naye hatakula katika vitu vitakatifu, asipooga mwili wake majini.
Lévitique 15.5 Hébreux 10.22 Nombres 19.7-19.10 Aggée 2.13 Lévitique 16.24-16.28
7 Jua likiisha kuchwa atakuwa safi; kisha baadaye atakula katika vitu vitakatifu, maana ni chakula chake.
Lévitique 21.22 Deutéronome 18.3-18.4 Nombres 18.11-18.19 1 Corinthiens 9.4 1 Corinthiens 9.13-9.14
8 Nyamafu au mnyama aliyeraruliwa na wanyama asile, asijitie unajisi kwa hiyo nyama; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 17.15 Exode 22.31 Deutéronome 14.21 Lévitique 7.24 Ezéchiel 44.31
9 Basi kwa hiyo watayashika mausia yangu, wasije wakachukua dhambi kwa hayo, nao wakafa humo, wakiyanajisi; mimi ndimi Bwana niwatakasaye.
Exode 28.43 Nombres 18.22 Lévitique 16.2 Nombres 18.32 Lévitique 10.1-10.2
10 Mgeni awaye yote asile katika kitu kitakatifu; mgeni wa kuhani akaaye kwake, au mtumishi aliyeajiriwa, asile katika kitu kitakatifu.
1 Samuel 21.6 Matthieu 12.4 Exode 29.33
11 Lakini kwamba kuhani akinunua mtu ye yote, kwa kumnunua kwa fedha zake, yeye atakula katika hicho; na hao waliozaliwa nyumbani mwake watakula katika chakula chake.
Genèse 17.13 Exode 12.44 Nombres 18.11-18.13
12 Na binti ya kuhani kwamba ameolewa na mgeni, asile katika sadaka ya kuinuliwa katika vitu vile vitakatifu.
Lévitique 21.3 Esaïe 40.13
13 Lakini kwamba binti ya kuhani ni mjane, au kwamba ameachwa na mumewe, wala hana mtoto, kisha amerudi na kuketi katika nyumba ya baba yake, kama vile katika ujana wake, yeye atakula katika chakula cha baba yake; lakini mgeni awaye yote asile katika chakula hicho.
Lévitique 10.14 Genèse 38.11 Nombres 18.11-18.19
14 Tena kama mtu ye yote akila katika kitu kilicho kitakatifu pasipo kukijua, ndipo ataongeza sehemu ya tano juu ya kitu hicho, na kumpa kuhani kitu hicho kitakatifu.
Lévitique 27.15 Lévitique 27.13 Lévitique 5.15-5.19
15 Wala wasivinajisi vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, wavisongezavyo kwa Bwana;
Nombres 18.32 Lévitique 19.8 Ezéchiel 22.26 Lévitique 22.9
16 hata wakawatwika ule uovu uletao hatia, hapo walapo vitu vyao vitakatifu; kwa kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye.
Lévitique 22.9 1 Pierre 2.24 Psaumes 38.4 Lévitique 20.8 Lévitique 7.18

Règlements concernant les victimes

17 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
18 Nena na Haruni na wanawe, na wana wa israeli wote, uwaambie, Mtu ye yote wa nyumba ya Israeli, au wa wageni walio katika Israeli, atakayetoa matoleo yake, kama ni nadhiri zao mojawapo, au kama ni sadaka yo yote ya hiari, watakayomtolea Bwana kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Lévitique 1.2 Deutéronome 12.6 Nombres 15.3 Lévitique 1.10 Psaumes 116.14
19 ili mpate kukubaliwa, mtaleta mume mkamilifu, katika ng’ombe, au katika kondoo, au katika mbuzi.
Lévitique 1.3 Lévitique 1.10 Exode 12.5 1 Pierre 3.18 Lévitique 4.32
20 Lakini mnyama ye yote aliye na kilema msimtoe; kwa kuwa hatakubaliwa kwa ajili yenu.
Deutéronome 17.1 Malachie 1.8 Deutéronome 15.21 Hébreux 9.14 Lévitique 22.25
21 Na mtu awaye yote atakayemtolea Bwana dhabihu katika sadaka za amani, ili kuondoa nadhiri, au sadaka ya moyo wa kupenda, katika ng’ombe, au katika kondoo, atakuwa mkamilifu, apate kukubaliwa; pasiwe na kilema ndani yake cho chote.
Nombres 15.8 Nombres 15.3 Lévitique 3.6 Deutéronome 23.21-23.23 Ecclésiaste 5.4-5.5
22 Kipofu, au aliyevunjika mahali, au kiwete au aliye na vidonda, au aliye na upele, au aliye na kikoko, hamtamtolea Bwana wanyama hao, wala msiwasongeze kwa Bwana kwa njia ya moto juu ya madhabahu.
Lévitique 22.20 Lévitique 3.3 Lévitique 1.13 Lévitique 3.5 Malachie 1.8
23 Ng’ombe, au mwana-kondoo aliye na kitu kilichozidi, au aliyepungukiwa na kitu katika vitu vya mwilini mwake, mna ruhusa kutoa kuwa sadaka ya moyo wa kupenda; lakini kwa ajili ya nadhiri hatakubaliwa.
Lévitique 21.18
24 Mnyama aliyeumia mapumbu yake, au kusetwa, au kuvunjwa, au kukatwa, msimtolee Bwana; wala msifanye hivi katika nchi yenu.
Lévitique 22.20 Lévitique 21.20 Deutéronome 23.1
25 Wala msisongeze chakula cha Mungu wenu katika wanyama hao mmojawapo kitokacho mkononi mwa mgeni; kwa sababu uharibifu wao u ndani yao, wana kilema ndani yao; hawatakubaliwa kwa ajili yenu.
Lévitique 21.8 Lévitique 21.6 Nombres 15.14-15.16 Esdras 6.8-6.10 Nombres 16.40
26 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
27 Hapo ng’ombe, au kondoo, au mbuzi, akizaliwa, atakuwa pamoja na mamaye muda wa siku saba; na siku ya nane na baadaye atakubaliwa kuwa ni sadaka ya kutolewa kwa Bwana kwa njia ya moto.
Exode 22.30 Lévitique 22.25 Lévitique 19.23-19.24 Lévitique 12.2-12.3
28 Tena kama ni ng’ombe, au kama ni kondoo, msimchinje huyo na mwanawe wote wawili kwa siku moja.
Deutéronome 22.6-22.7 Deutéronome 14.21 Exode 34.26 Exode 23.19
29 Tena mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa.
Psaumes 107.22 Amos 4.5 Psaumes 116.17 Hébreux 13.15 Lévitique 7.12-7.15
30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi Bwana.
Exode 16.19-16.20 Lévitique 19.7 Lévitique 7.15-7.18
31 Kwa hiyo mtayashika maagizo yangu, na kuyafanya; mimi ndimi Bwana.
Deutéronome 4.40 Lévitique 19.37 Nombres 15.40 1 Thessaloniciens 4.1-4.2 Lévitique 18.4-18.5
32 Wala msilinajisi jina langu takatifu; lakini nitatakaswa mimi katika wana wa Israeli; mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi,
Lévitique 18.21 Lévitique 10.3 Lévitique 22.2 Lévitique 20.8 Lévitique 21.15
33 niliyewaleta mtoke nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 11.45 Exode 6.7 Lévitique 19.36 Nombres 15.41 Exode 20.2

Cette Bible est dans le domaine public.