Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 8.21
Bible en Swahili de l’est


Vision du bélier et du bouc

1 Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza maono yalinitokea mimi, naam, mimi Danielii, baada ya hayo yaliyonitokea hapo kwanza.
Daniel 7.1 Daniel 7.28 Daniel 10.7 Daniel 11.4 Daniel 7.15
2 Nami naliona katika maono; ilitukia, nilipoona, nalikuwako huko Shushani ngomeni, katika wilaya ya Elamu; nikaona katika maono, nami nalikuwa karibu na mto Ulai.
Esther 1.2 Néhémie 1.1 Jérémie 25.25 Ezéchiel 32.24 Genèse 14.1
3 Ndipo nikainua macho yangu nikaona, na tazama, mbele ya mto alisimama kondoo mume, mwenye pembe mbili; na pembe zile mbili zilikuwa ndefu; lakini moja ilikuwa ndefu kuliko ya pili, na ile iliyokuwa ndefu zaidi ilizuka mwisho.
Daniel 8.20 Daniel 10.5 Esther 1.3 Zacharie 1.18 Esaïe 44.28
4 Nikamwona huyo kondoo mume akisukuma upande wa magharibi, na upande wa kaskazini, na upande wa kusini; wala hakuna mnyama ye yote awezaye kusimama mbele yake, wala hakuna mnyama ye yote awezaye kupokonya mkononi mwake; lakini alitenda kama alivyopenda mwenyewe, akajitukuza nafsi yake.
Daniel 11.16 Daniel 8.7 Daniel 11.36 Michée 5.8 Daniel 5.19
5 Nami nilipokuwa nikifikiri, tazama, beberu akatoka upande wa magharibi, juu ya uso wa dunia nzima, bila kuigusa nchi; na beberu yule alikuwa na pembe mashuhuri kati ya macho yake.
Daniel 8.21 Daniel 8.8 Daniel 11.3 Daniel 2.32 Daniel 7.6
6 Naye akamwendea huyo kondoo mume mwenye pembe mbili, niliyemwona akisimama karibu na mto, akamshambulia kwa ghadhabu za nguvu zake.
7 Nikamwona akimkaribia kondoo mume, akamwonea hasira kali, akampiga kondoo mume, akazivunja pembe zake mbili; na huyo kondoo mume alikuwa hana nguvu kusimama mbele yake; bali akamwangusha chini, akamkanyaga-kanyaga; wala hapakuwapo awezaye kumwokoa kondoo mume katika mkono wake.
Daniel 11.11 Daniel 7.7 Josué 8.20 Lévitique 26.37
8 Na yule beberu akajitukuza sana; na alipokuwa na nguvu, pembe ile kubwa ilivunjika; na badala yake zikazuka pembe nne mashuhuri zilizoelekea pepo nne za mbinguni.
Daniel 7.2 Apocalypse 7.1 Daniel 5.20 Daniel 8.22 2 Chroniques 26.16
9 Na katika moja ya pembe hizo ilitokea pembe ndogo, iliyokua sana, upande wa kusini, na upande wa magharibi, na upande wa nchi ya uzuri.
Daniel 11.16 Psaumes 48.2 Ezéchiel 20.6 Daniel 7.8 Ezéchiel 20.15
10 Nayo ikakua, kiasi cha kulifikilia jeshi la mbinguni; ikaangusha chini baadhi ya jeshi lile, na ya nyota, ikazikanyaga.
Esaïe 14.13 Apocalypse 12.4 Daniel 7.7 Daniel 8.7 Daniel 11.28
11 Naam, ikajitukuza hata juu yake aliye mkuu wa jeshi hilo, ikamwondolea sadaka ya kuteketezwa ya daima, na mahali pa patakatifu pake pakaangushwa chini.
Daniel 11.31 Daniel 12.11 Daniel 8.25 Ezéchiel 46.14 Esaïe 37.23
12 Na jeshi likatolewa kwake pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya daima, kwa sababu ya makosa; nayo ikaiangusha kweli hata chini; ikatenda ilivyopenda, na kufanikiwa.
Daniel 11.28 Esaïe 59.14 Daniel 8.4 1 Samuel 23.9 Psaumes 119.43
13 Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi?
Luc 21.24 Daniel 9.27 Apocalypse 11.2 Apocalypse 6.10 Daniel 4.13
14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa.
Apocalypse 11.2-11.3 Daniel 7.25 Daniel 12.7 Daniel 8.26 Esaïe 1.27
15 Ikawa mimi, naam, mimi Danielii, nilipoyaona maono hayo, nalitafuta kuyafahamu, na tazama, alisimama mbele yangu mmoja mfano wa mwanadamu.
Daniel 10.16 Daniel 10.18 Apocalypse 1.13 1 Pierre 1.10-1.11 Matthieu 13.36
16 Nikasikia sauti ya mwanadamu katikati ya mto Ulai, iliyoita na kusema, Gabrieli, mfahamishe mtu huyu maono haya.
Luc 1.19 Luc 1.26 Daniel 12.5-12.7 Daniel 8.2 Daniel 10.11-10.12
17 Basi alipakaribia mahali niliposimama; nami naliogopa alipokaribia, nikaanguka kifudifudi; lakini aliniambia, Fahamu, Ee mwanadamu, kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.
Daniel 8.19 Apocalypse 1.17 Daniel 12.4 Habakuk 2.3 Ezéchiel 1.28-2.1
18 Basi alipokuwa akisema nami, nalishikwa na usingizi mzito na uso wangu uliielekea nchi; lakini alinigusa, akanisimamisha wima.
Daniel 10.18 Ezéchiel 2.2 Daniel 10.16 Luc 9.32 Daniel 8.27
19 Akaniambia, Tazama, nitakujulisha yatakayokuwa wakati wa mwisho wa ghadhabu; maana, ni ya wakati wa mwisho ulioamriwa.
Daniel 8.15-8.17 Habakuk 2.3 Apocalypse 11.18 Apocalypse 1.1 Daniel 11.27
20 Yule kondoo mume uliyemwona, mwenye pembe mbili, hizo ndizo wafalme wa Umedi na Uajemi.
Daniel 8.3 Daniel 11.1-11.2
21 Na yule beberu, mwenye manyoya mengi, ni mfalme wa Uyunani; na ile pembe kubwa iliyo kati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
Daniel 11.3 Daniel 10.20 Daniel 8.5-8.8
22 Tena katika habari ya pembe ile iliyovunjika, ambayo badala yake zilisimama pembe nne, falme nne zitasimama kutoka katika taifa lile, lakini si kwa nguvu kama zake.
Daniel 8.3 Daniel 11.4 Daniel 8.8
23 Na wakati wa mwisho wa ufalme wao, wakosao watakapotimia, mfalme mwenye uso mkali, afahamuye mafumbo, atasimama.
Apocalypse 13.11-13.14 2 Thessaloniciens 2.9-2.11 Daniel 8.9-8.12 1 Timothée 4.1 Daniel 7.25
24 Na nguvu zake zitakuwa nyingi mno, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe; naye ataharibu kiasi cha kustaajabisha watu, na kufanikiwa, na kutenda apendavyo; naye atawaangamiza hao walio hodari na watu watakatifu.
Daniel 8.12 Apocalypse 17.17 Apocalypse 13.3-13.10 Daniel 7.25 Apocalypse 17.6
25 Na kwa mashauri yake atafanikisha hila mkononi mwake; naye atajitukuza nafsi yake moyoni mwake; naye atawaangamiza wengi katika hali yao ya salama; naye atasimama kushindana naye aliye Mkuu wa wakuu; lakini atavunjika, bila kazi ya mikono.
Daniel 8.11 Job 34.20 Apocalypse 19.19-19.21 Daniel 7.8 Daniel 11.45
26 Na maono ya hizo nyakati za jioni na asubuhi yaliyosemwa ni kweli; lakini wewe yafunike maono hayo; maana ni ya wakati ujao baada ya siku nyingi.
Daniel 10.1 Daniel 12.4 Daniel 12.9 Daniel 10.14 Apocalypse 22.10
27 Na mimi, Danielii, nikazimia, nikaugua siku kadha wa kadha; kisha nikaondoka, nikatenda shughuli za mfalme; nami naliyastajabia yale maono, ila hakuna aliyeyafahamu.
Daniel 7.28 Habakuk 3.16 Daniel 10.8 Daniel 10.16 Daniel 8.7

Cette Bible est dans le domaine public.