Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 32.27
Bible en Swahili de l’est


Complainte sur le pharaon et l’Égypte

1 Ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 32.17 Ezéchiel 30.20 Ezéchiel 1.2 Ezéchiel 29.1 Ezéchiel 33.21
2 Mwanadamu, mfanyie Farao, mfalme wa Misri, maombolezo, umwambie, Ulifananishwa na mwana-simba wa mataifa; lakini umekuwa kama joka katika bahari; nawe watoka kwa nguvu pamoja na mito yako, na kuyachafua maji kwa miguu yako, na kuitia uchafu mito yao.
Ezéchiel 29.3 Nahum 2.11-2.13 Ezéchiel 27.2 Ezéchiel 28.12 Ezéchiel 34.18
3 Bwana MUNGU asema hivi; Nitautanda wavu wangu juu yako, kwa kusanyiko la watu wa kabila nyingi; nao watakuvua katika jarife langu.
Ezéchiel 12.13 Jérémie 16.16 Lamentations 1.13 Ezéchiel 17.20 Ecclésiaste 9.12
4 Nami nitakuacha juu ya nchi kavu, nitakutupa juu ya uso wa uwanda, nami nitawaleta ndege wote wa angani watue juu yako, nami nitawashibisha wanyama wa dunia yote kwako wewe.
Esaïe 18.6 Ezéchiel 29.5 Ezéchiel 31.12-31.13 Esaïe 66.24 1 Samuel 17.44-17.46
5 Nami nitaweka nyama yako juu ya milima, na kuyajaza mabonde kwa urefu wako.
Ezéchiel 31.12
6 Tena kwa damu yako nitainywesha nchi, ambayo waogelea juu yake, hata milimani; na mifereji ya maji itajawa nawe.
Esaïe 34.3 Apocalypse 14.20 Exode 7.17 Esaïe 34.7 Apocalypse 16.6
7 Nami nitakapokuzimisha, nitazifunikiza mbingu, na kuzifanya nyota zake kuwa giza; nami nitalifunika jua kwa wingu, wala mwezi hautatoa nuru yake.
Matthieu 24.29 Esaïe 13.10 Joël 2.31 Joël 2.2 Joël 3.15
8 Mianga yote ya mbinguni iangazayo nitaifanya kuwa giza juu yako, nami nitatia giza katika nchi yako, asema Bwana MUNGU.
Genèse 1.14 Proverbes 20.20
9 Tena nitawakasirisha watu wengi mioyo yao, nitakapoleta uangamivu wako kati ya mataifa, uingie katika nchi ambazo hukuzijua.
Apocalypse 18.10-18.15 Ezéchiel 30.23 Ezéchiel 29.12 Apocalypse 11.18 Jérémie 25.15-25.25
10 Nami nitawashangaza watu wa kabila nyingi kwa habari zako, na wafalme wao wataogopa sana kwa ajili yako, nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao; nao watatetemeka kila dakika, kila mtu kwa ajili ya uhai wake, katika siku ya kuanguka kwako.
Ezéchiel 27.35 Ezéchiel 26.16 Exode 15.14-15.16 Apocalypse 18.10 Deutéronome 29.24
11 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Upanga wa mfalme wa Babeli utakujilia.
Ezéchiel 26.7 Jérémie 43.10 Ezéchiel 30.22-30.25 Ezéchiel 30.4 Jérémie 46.13
12 Kwa panga za mashujaa nitawaangusha watu wako wote jamii; hao wote ni watu wa mataifa watishao, nao watakiharibu kiburi cha Misri, na jamii ya watu wake wengi wataangamia.
Ezéchiel 28.7 Ezéchiel 31.11 Ezéchiel 29.19 Esaïe 25.2-25.3 Ezéchiel 30.11
13 Tena nitawaharibu wanyama wake wote, toka kando ya maji mengi; na mguu wa mwanadamu hautayatibua tena, wala kwato za mnyama hazitayatibua.
Ezéchiel 29.11 Ezéchiel 29.8 Ezéchiel 34.18 Ezéchiel 32.2 Ezéchiel 30.12
14 Ndipo nitakapoyafanya maji yao kuwa safi, na kuiendesha mito yao kama mafuta, asema Bwana MUNGU.
15 Nitakapoifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa na jangwa, nchi iliyopungukiwa na vitu vilivyoijaza, nitakapowapiga watu wote wakaao ndani yake, ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 6.7 Exode 7.5 Exode 14.4 Exode 14.18 Ezéchiel 29.19-29.20
16 Hayo ndiyo maombolezo watakayoomboleza; binti za mataifa wataomboleza kwa hayo; kwa hayo wataomboleza kwa ajili ya Misri, na kwa ajili ya watu wake wote jamii, asema Bwana MUNGU.
2 Samuel 1.17 Ezéchiel 26.17 2 Chroniques 35.25 Ezéchiel 32.2 2 Samuel 3.33-3.34
17 Ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema,
Ezéchiel 32.1 Ezéchiel 1.2 Ezéchiel 31.1 Ezéchiel 33.21
18 Mwanadamu, walilie watu wa Misri. Wote jamii ukawabwage, naam, yeye, na binti za mataifa mashuhuri, hata pande za chini za nchi, pamoja na watu washukao shimoni.
Ezéchiel 31.14 Ezéchiel 32.2 Michée 1.8 Jérémie 1.10 Ezéchiel 32.16
19 Umemshinda nani kwa uzuri? Shuka, ukalazwe pamoja na wasiotahiriwa.
Ezéchiel 32.29-32.30 Ezéchiel 31.18 Ezéchiel 31.2 Jérémie 9.25-9.26 Ezéchiel 32.24
20 Wataanguka kati ya watu waliouawa kwa upanga; ametokwa apigwe na upanga; mvuteni aende mbali pamoja na watu wake wote jamii.
Psaumes 28.3 Ezéchiel 32.23-32.26 Ezéchiel 32.29-32.30 Proverbes 24.11 Jérémie 22.19
21 Walio hodari watasema naye, toka kati ya kuzimu pamoja nao wamsaidiao; wameshuka wamelala kimya, hata wasiotahiriwa, hali wameuawa kwa upanga.
Esaïe 14.9-14.10 Ezéchiel 32.27 Luc 16.23-16.24 Proverbes 14.32 Ezéchiel 32.24-32.25
22 Ashuru yuko huko, na watu wake wote jamii; makaburi yake yamzunguka; wote pia wameuawa, wameanguka kwa upanga,
Ezéchiel 32.26 Ezéchiel 32.29-32.30 Ezéchiel 32.24 Nahum 1.7-1.12 Nahum 3.1-3.19
23 ambao makaburi yao yamewekwa pande za shimo zilizo mbali sana, wote jamii wamezunguka kaburi lake; wote pia wameuawa, wameanguka kwa upanga, waliofanya utisho katika nchi yao walio hai.
Ezéchiel 26.20 Ezéchiel 32.24-32.27 Ezéchiel 26.17 Psaumes 27.13 Esaïe 38.11
24 Elamu yuko huko, na watu wake wote jamii, pande zote za kaburi lake; wote pia wameuawa, wameanguka kwa upanga, walioshuka hali hawana tohara hata pande za chini ya nchi; ambao waliwatia watu hofu katika nchi ya walio hai, nao wamechukua aibu yao, pamoja nao washukao shimoni.
Ezéchiel 26.20 Ezéchiel 16.54 Ezéchiel 16.52 Ezéchiel 32.18 Jérémie 49.34-49.39
25 Wamemwekea kitanda kati ya hao waliouawa, pamoja na watu wake wote jamii; makaburi yake yamzunguka; wote pia hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga; maana maogofyo yao yalifanyika katika nchi ya walio hai, nao wamechukua aibu yao, pamoja nao washukao shimoni; amewekwa kati ya hao waliouawa.
Psaumes 139.8 Ezéchiel 32.19 Ezéchiel 32.21 Ezéchiel 44.7 Luc 12.4-12.5
26 Mesheki yuko huko, na Tubali, na watu wake wote jamii; makaburi yake yamzunguka; wote pia hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga; maana walifanya utisho wao katika nchi ya walio hai.
Ezéchiel 27.13 Genèse 10.2 Ezéchiel 39.1 Ezéchiel 38.2-38.3 Ezéchiel 32.27
27 Je! Wasilale pamoja na mashujaa wao wasiotahiriwa, walioanguka, walioshuka kuzimu pamoja na silaha zao za vita, ambao wameweka panga zao chini ya vichwa vyao, na maovu yao mifupani mwao? Maana waliwatisha mashujaa katika nchi ya walio hai.
Esaïe 14.18-14.19 Psaumes 109.18 Ezéchiel 32.21 Job 3.13-3.15 Job 20.11
28 Lakini utavunjika kati ya hao wasiotahiriwa, nawe utalala pamoja nao waliouawa kwa upanga.
Daniel 2.34-2.35
29 Edomu yuko huko, wafalme wake, na wakuu wake wote, ambao katika uwezo wao wamelazwa pamoja nao waliouawa kwa upanga; watalala pamoja na hao wasiotahiriwa, na pamoja na hao washukao shimoni.
Jérémie 49.7-49.22 Esaïe 63.1-63.6 Esaïe 34.1-34.17 Ezéchiel 35.1-35.15 Amos 1.11-1.12
30 Wakuu wa kaskazini wako huko, wote pia, na Wasidoni, wote walioshuka pamoja na hao waliouawa; kwa sababu ya utisho walioufanya katika uwezo wao wamefedheheka, nao wamelala hali hawana tohara, pamoja nao waliouawa kwa upanga, nao wanachukua aibu yao, pamoja nao washukao shimoni.
Ezéchiel 38.6 Ezéchiel 39.2 Ezéchiel 28.21 Ezéchiel 38.15 Jérémie 25.26
31 Farao atawaona, naye atapata faraja juu ya watu wake wote jamii; naam, Farao, jeshi lake lote waliouawa kwa upanga, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 31.16 Ezéchiel 14.22 Lamentations 2.13
32 Kwa maana nimeweka utisho wake katika nchi ya walio hai; naye atalazwa kati yao wasiotahiriwa, pamoja na hao waliouawa kwa upanga; yeye Farao na watu wake wote jamii, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 32.27 Sophonie 3.6-3.8 Hébreux 10.31 Genèse 35.5 Job 31.23

Cette Bible est dans le domaine public.