Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 22.3
Bible en Swahili de l’est


Crimes et jugement de Jérusalem

1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Na wewe, mwanadamu, je! Utauhukumu, utauhukumu mji huu wa damu? Basi uujulishe machukizo yake yote.
Nahum 3.1 Ezéchiel 24.6 Ezéchiel 24.9 2 Rois 21.16 Actes 7.52
3 Nawe utasema, Bwana MUNGU asema hivi; Mji umwagao damu ndani yake, ili wakati wake upate kuja; mji ufanyao vinyago juu ya nafsi yake, ili ujitie unajisi!
Ezéchiel 22.27 Ezéchiel 22.4 Ezéchiel 24.6-24.9 Romains 2.5 Ezéchiel 23.45
4 Umekuwa na hatia katika damu yako uliyomwaga, nawe umekuwa na unajisi kwa vinyago vyako ulivyovifanya; nawe umezileta karibu siku zako, nawe umefika karibu na miaka yako; basi, kwa sababu ya hayo, nimekufanya kuwa lawama kwa mataifa, na kuwa dhihaka katika nchi zote.
2 Rois 21.16 Psaumes 44.13-44.14 Ezéchiel 5.14-5.15 Ezéchiel 16.57 Ezéchiel 22.2
5 Zilizo karibu, na zilizo mbali nawe, zitakudhihaki, Ewe mchafu, uliyejaa fujo.
Esaïe 22.2 Jérémie 15.2-15.3
6 Tazama, wakuu wa Israeli, kila mmoja kwa kadiri ya nguvu zake, wamekuwamo ndani yako, ili kumwaga damu.
Esaïe 1.23 Ezéchiel 22.27 Michée 2.1 Jérémie 5.5 Jérémie 2.26-2.27
7 Ndani yako wamedharau baba na mama; kati yako wamewatenda wageni udhalimu; ndani yako wamewaonea yatima na mjane.
Exode 22.21-22.22 Deutéronome 27.16 Zacharie 7.10 Jérémie 7.6 Lévitique 20.9
8 Umevidharau vitu vyangu vitakatifu, umezitia unajisi sabato zangu.
Ezéchiel 22.26 Ezéchiel 23.38-23.39 Ezéchiel 20.13 Ezéchiel 20.21 Ezéchiel 20.24
9 Wasingiziaji wamekuwamo ndani yako, ili kumwaga damu; na ndani yako wamekula juu ya milima; kati yako wamefanya uasherati.
Osée 4.14 Osée 4.10 Lévitique 19.16 Osée 4.2 Ezéchiel 18.11
10 Ndani yako wamefunua uchi wa baba zao; ndani yako wamemfanyia nguvu mwanamke asiye safi wakati wa kutengwa kwake.
Lévitique 18.19 Lévitique 18.7-18.8 Lévitique 20.11 Ezéchiel 18.6 2 Samuel 16.21-16.22
11 Na mtu mmoja amefanya chukizo pamoja na mke wa jirani yake; na mtu mwingine amemharibu mke wa mwanawe kwa uasherati; na mtu mwingine ndani yako amemfanyia nguvu umbu lake, binti ya babaye.
Lévitique 18.15 Lévitique 20.17 Lévitique 18.9 2 Samuel 13.14 Lévitique 18.20
12 Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.
Deutéronome 27.25 Ezéchiel 23.35 Deutéronome 16.19 Lévitique 25.35-25.36 Psaumes 106.21
13 Basi, tazama, nimeipigia kofi hiyo faida uliyopata kwa njia isiyo haki, na hiyo damu yako iliyokuwa kati yako.
Ezéchiel 21.17 Esaïe 33.15 Ezéchiel 21.14 Ezéchiel 22.27 Amos 2.6-2.8
14 Je! Moyo wako waweza kuvumilia, au mkono wako waweza kuwa hodari, katika siku zile nitakapokutenda mambo? Mimi, Bwana, nimenena neno hili, tena nitalitenda.
Ezéchiel 17.24 Ezéchiel 21.7 Ezéchiel 24.14 1 Corinthiens 10.22 Ezéchiel 28.9
15 Nami nitakutawanya kati ya mataifa, na kukutapanya kati ya nchi mbalimbali; nami nitauteketeza uchafu wako, ili ukutoke.
Zacharie 7.14 Deutéronome 4.27 Ezéchiel 22.22 Néhémie 1.8 Matthieu 3.12
16 Nawe utatiwa unajisi ndani ya nafsi yako, mbele ya macho ya mataifa; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 6.7 Ezéchiel 7.24 Psaumes 83.18 Esaïe 37.20 Exode 8.22
17 Neno la Bwana likanijia, kusema,
18 Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa taka za fedha kwangu; wote wamekuwa shaba, na bati, na chuma, na risasi, kati ya tanuu; wamekuwa taka za fedha.
Esaïe 1.22 Psaumes 119.119 Esaïe 48.10 Jérémie 6.28-6.30 Proverbes 17.3
19 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa taka za fedha, tazama, nitawakusanya kati ya Yerusalemu.
Matthieu 13.40-13.42 Matthieu 13.30 Michée 4.12 Ezéchiel 11.7 Ezéchiel 24.3-24.6
20 Kama vile watu wakusanyavyo fedha, na shaba, na chuma, na risasi, na bati, kati ya tanuu, ili kuvifukutia moto na kuviyeyusha; ndivyo nitakavyowakusanya ninyi katika hasira yangu, na ghadhabu yangu, nami nitawalaza huko, na kuwayeyusha.
Ezéchiel 22.21 Jérémie 4.11-4.12 Jérémie 4.20 Ezéchiel 21.31-21.32 Esaïe 54.16
21 Naam, nitawakusanya, na kuwafukutia moto wa ghadhabu yangu, nanyi mtayeyushwa kati yake.
Deutéronome 29.20 Esaïe 30.33 Psaumes 112.10 Jérémie 21.12 Nahum 1.6
22 Kama fedha iyeyushwavyo kati ya tanuu, ndivyo mtakavyoyeyushwa kati yake; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimemwaga ghadhabu yangu juu yenu.
Ezéchiel 20.8 Ezéchiel 20.33 Osée 5.10 Ezéchiel 22.16 Ezéchiel 22.31

Péchés des chefs et du peuple d’Israël

23 Neno la Bwana likanijia, kusema,
24 Mwanadamu, uiambie nchi, Wewe u nchi isiyosafika, wala kunyeshewa mvua siku ya ghadhabu.
Jérémie 2.30 Sophonie 3.2 Esaïe 9.13 Jérémie 6.29 Jérémie 5.3
25 Fitina ya manabii wake imo ndani yake, kama simba angurumaye akirarua mawindo; wamekula roho za watu; hutwaa kwa nguvu hazina na vitu vya thamani; wameongeza hesabu ya wajane wake ndani yake.
Osée 6.9 Ezéchiel 13.19 Jérémie 11.9 Jérémie 2.34 Esaïe 56.11
26 Makuhani wake wameihalifu sheria yangu, wametia unajisi vitu vyangu vitakatifu; hawakuweka tofauti ya vitu vitakatifu na vitu vya kutumiwa sikuzote; wala hawakuwafundisha watu kupambanua vitu vichafu na vitu vilivyo safi, nao wamefumba macho yao, wasiziangalie sabato zangu, nami nimetiwa unajisi kati yao.
Lévitique 10.10 1 Samuel 2.12-2.17 Ezéchiel 44.23 Jérémie 2.8 Ezéchiel 22.8
27 Wakuu wake kati yake wamekuwa kama mbwa-mwitu wakirarua mawindo; ili kumwaga damu, na kuharibu roho za watu, wapate faida kwa njia isiyo halali.
Ezéchiel 22.13 Sophonie 3.3 Esaïe 1.23 Ezéchiel 22.6 Michée 3.9-3.11
28 Na manabii wake wamewapakia chokaa isiyokorogwa vema, wakiona ubatili, na kuwatabiria maneno ya uongo, wakisema, Bwana MUNGU asema hivi; iwapo Bwana hakusema neno.
Jérémie 23.25-23.32 Ezéchiel 13.6-13.7 Lamentations 2.14 Jérémie 28.2 Ezéchiel 22.25
29 Watu wa nchi wametumia udhalimu, wamenyang’anya kwa nguvu; naam, wamewatenda jeuri maskini na wahitaji, nao wamewaonea wageni bila haki.
Ezéchiel 22.7 Esaïe 5.7 Exode 23.9 Exode 22.21 Amos 3.10
30 Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.
Esaïe 59.16 Jérémie 5.1 Ezéchiel 13.5 Psaumes 106.23 Esaïe 63.5
31 Kwa sababu hiyo nimemwaga ghadhabu yangu juu yao; nimewateketeza kwa moto wa hasira yangu; nami nimeileta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 16.43 Ezéchiel 9.10 Ezéchiel 7.8-7.9 Romains 2.8-2.9 Ezéchiel 7.3

Cette Bible est dans le domaine public.