Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 19.6
Bible en Swahili de l’est


Complainte sur les princes d’Israël

1 Tena uwaombolezee wakuu wa Israeli,
2 Rois 24.6 Ezéchiel 26.17 Ezéchiel 27.2 Ezéchiel 19.14 2 Rois 25.5-25.7
2 useme, Mama yako alikuwa nini? Simba mke; alijilaza kati ya simba, kati ya wana-simba aliwalisha watoto wake.
Job 4.11 Esaïe 5.29 Psaumes 58.6 Esaïe 11.6-11.9 Nahum 2.11-2.12
3 Akamlea mtoto mmoja katika watoto wake, akawa mwana-simba, akajifunza kuwinda mawindo, akala watu.
Ezéchiel 19.6 Ezéchiel 22.25 2 Rois 23.31-23.32 2 Chroniques 36.1-36.2
4 Mataifa nao wakapata habari zake, akanaswa katika rima lao, wakamchukua kwa kulabu mpaka nchi ya Misri.
2 Rois 23.33-23.34 2 Chroniques 36.4 Jérémie 22.11-22.12 2 Chroniques 36.6 2 Rois 23.31
5 Basi mamaye alipoona kwamba amemngoja, na tumaini lake limepotea, akatwaa mtoto mwingine katika watoto wake, akamfanya mwana-simba.
Ezéchiel 19.3 2 Rois 23.34-23.37
6 Naye akaenda huko na huko kati ya simba, akawa mwana-simba, akajifunza kuwinda mawindo, akala watu.
Jérémie 36.1-36.32 2 Chroniques 36.9 2 Rois 24.9 2 Chroniques 36.5 2 Rois 24.1-24.7
7 Akayajua majumba yao, akaiharibu miji yao; nchi ikawa ukiwa, navyo vitu vilivyoijaza, kwa sababu ya mshindo wa kunguruma kwake.
Ezéchiel 30.12 Amos 6.8 Michée 1.2 Proverbes 28.3 Ezéchiel 12.19
8 Ndipo mataifa wakajipanga juu yake pande zote toka nchi zote; wakaunda wavu wao juu yake; akanaswa katika rima lao.
Ezéchiel 19.4 Ezéchiel 12.13 Ezéchiel 17.20 2 Rois 24.11 Lamentations 4.20
9 Wakamtia katika tundu kwa kulabu, wakamleta kwa mfalme wa Babeli wakamtia ndani ya ngome, sauti yake isisikiwe tena juu ya milima ya Israeli.
2 Chroniques 36.6 Ezéchiel 6.2 2 Rois 24.15 Jérémie 22.18-22.19 Ezéchiel 19.7
10 Mama yako alikuwa kama mzabibu, katika damu yako, uliopandwa karibu na maji; akazaa sana na kujaa matawi, kwa sababu ya maji mengi.
Psaumes 80.8-80.11 Deutéronome 8.7 Esaïe 5.1-5.4 Ezéchiel 19.2 Ezéchiel 15.2-15.8
11 Naye alikuwa na vijiti vya nguvu, kwa fimbo za enzi zao watawalao, na kimo chao kiliinuka kati ya matawi manene, wakaonekana kwa urefu wao, pamoja na wingi wa matawi yao.
Ezéchiel 31.3 Daniel 4.11 Psaumes 80.15 Daniel 4.20-4.21 Ezéchiel 19.14
12 Lakini aling’olewa kwa ghadhabu, akaangushwa chini, upepo wa mashariki ukakausha matunda yake; vijiti vyake vya nguvu vikavunjika, vikakauka; moto ulivila.
Ezéchiel 17.10 Osée 13.15 Esaïe 27.11 Jérémie 31.28 Ezéchiel 19.11
13 Na sasa umepandwa jangwani, katika nchi kavu, ya ukame.
Osée 2.3 Ezéchiel 19.10 2 Rois 24.12-24.16 Deutéronome 28.47-28.48 Ezéchiel 20.35
14 Na moto umetoka katika vijiti vya matawi yake, umekula matunda yake, hata hana tena kijiti cha nguvu kifaacho kwa fimbo ya enzi ya kutawala. Na hayo ni maombolezo, nayo yatakuwa maombolezo.
Ezéchiel 19.1 2 Rois 24.20 Ezéchiel 19.11 Néhémie 9.37 Psaumes 79.7

Cette Bible est dans le domaine public.