Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 41.7
Bible en Swahili de l’est


Puissance de Dieu et inconsistance des idoles

1 Nyamazeni mbele zangu, enyi visiwa, na mataifa wajipatie nguvu mpya; na waje karibu wakanene; na tukaribiane pamoja kwa hukumu.
Esaïe 1.18 Habakuk 2.20 Zacharie 2.13 Joël 3.10-3.11 Esaïe 41.6-41.7
2 Ni nani aliyemwinua mmoja atokaye mashariki, ambaye katika haki amemwita mguuni pake? Ampa mataifa mbele yake, na kumtawaza juu ya wafalme; awatoa wawe kama mavumbi kwa upanga wake, kama makapi yaliyopeperushwa kwa upinde wake.
Esaïe 45.1 Esaïe 40.24 Esaïe 46.11 2 Samuel 22.43 Esdras 1.2
3 Awafuatia, apita salama hata kwa njia asiyoikanyaga kamwe kwa miguu yake.
Esaïe 57.2 Job 5.24
4 Ni nani aliyetenda na kufanya jambo hilo, aviitaye vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, wa kwanza na wa mwisho, mimi ndiye.
Apocalypse 22.13 Apocalypse 1.17 Esaïe 41.26 Esaïe 46.10 Esaïe 48.12
5 Visiwa vimeona, vikaogopa; ncha za dunia zilitetemeka; walikaribia, walikuja.
Ezéchiel 26.15-26.16 Psaumes 67.7 Josué 5.1 Psaumes 65.8 Josué 2.10
6 Wakasaidiana, kila mtu na mwenzake, kila mtu akamwambia ndugu yake; Uwe na moyo mkuu.
Esaïe 40.19 Esaïe 44.12 Esaïe 35.4 Actes 19.24-19.28 Daniel 3.1-3.7
7 Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo akamhimiza yule apigaye fuawe, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, Ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike.
Esaïe 40.19-40.20 Jérémie 10.9 Esaïe 44.12-44.15 Daniel 3.1-3.7 Juges 18.24
8 Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;
Jacques 2.23 2 Chroniques 20.7 Esaïe 44.1-44.2 Esaïe 44.21 Esaïe 29.22
9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;
1 Corinthiens 1.26-1.29 Esaïe 41.8 Psaumes 94.14 Luc 13.29 Psaumes 107.2-107.3
10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Josué 1.9 Esaïe 43.1-43.2 Romains 8.31 Philippiens 4.13 Deutéronome 31.6-31.8
11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.
Esaïe 45.24 Exode 23.22 Daniel 4.35 Zacharie 12.3 Actes 16.39
12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.
Psaumes 37.35-37.36 Job 20.7-20.9 Esaïe 17.14
13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.
Esaïe 41.10 Esaïe 45.1 Esaïe 42.6 Psaumes 63.8 Psaumes 73.23
14 Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.
Psaumes 19.14 Psaumes 22.6 Esaïe 54.5 Esaïe 43.14 Jérémie 50.34
15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.
Michée 4.13 Habakuk 3.12 Esaïe 28.27 2 Corinthiens 10.4-10.5 Zacharie 4.7
16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.
Jérémie 51.2 Philippiens 3.3 Esaïe 12.6 Luc 1.46-1.47 Psaumes 1.4
17 Maskini na wahitaji wanatafuta maji, wala hapana; ndimi zao zimekauka kwa kiu; mimi, Bwana, nitawasikia, mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
Esaïe 30.19 Esaïe 55.1 Esaïe 61.1 Esaïe 42.16 Esaïe 66.2
18 Nitafunua vijito vya maji juu ya vilima, na chemchemi katikati ya mabonde; nitageuza jangwa kuwa ziwa la maji, na mahali pakavu kuwa vijito vya maji.
Esaïe 35.6-35.7 Psaumes 107.35 Esaïe 30.25 Ezéchiel 47.1-47.8 Esaïe 58.11
19 Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja;
Esaïe 55.13 Esaïe 37.31-37.32 Esaïe 60.13 Esaïe 35.1 Esaïe 60.21
20 ili waone, na kujua, wakafikiri, na kufahamu pamoja, ya kuwa mkono wa Bwana ndio uliofanya jambo hilo. Mtakatifu wa Israeli ndiye aliyeliumba.
Job 12.9 Esaïe 44.23 Exode 9.16 Psaumes 109.27 Esaïe 43.7-43.13
21 Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.
Job 23.3-23.4 Job 38.3 Michée 6.1-6.2 Job 40.7-40.9
22 Wayatangaze na kutujulisha yatakayokuwa; watuonyeshe mambo ya zamani, ni mambo gani, tukapate kuyatia moyoni, tukajue mwisho wake; au wamdhihirishie yatakayotokea baadaye.
Esaïe 45.21 Esaïe 46.10 Jean 13.19 Jean 16.14 Esaïe 42.9
23 Tujulisheni yatakayokuwa baadaye, nasi tutakiri ya kuwa ninyi ni miungu; naam, tendeni mema au tendeni mabaya, ili tujipime, tukaone pamoja.
Esaïe 44.7-44.8 Esaïe 42.9 Jérémie 10.5 Jean 13.19 Actes 15.18
24 Tazameni, ninyi si kitu, tena kazi yenu si kitu; awachaguaye ninyi ni chukizo.
Psaumes 115.8 1 Corinthiens 8.4 Esaïe 41.29 Jérémie 10.8 Esaïe 37.19
25 Nimemwinua mtu toka kaskazini, naye amekuja; toka maawio ya jua amekuja anitajaye jina langu; naye atawajilia maliwali kama akanyagaye matope, na kama mfinyanzi afinyangaye udongo.
Esaïe 41.2 2 Samuel 22.43 Zacharie 10.5 Michée 7.10 Esaïe 10.6
26 Ni nani aliyeihubiri habari tokea mwanzo, tupate kuijua? Na tokea zamani, tupate kusema, Yeye ni mwenye haki? Naam, hapana hata mmoja aliyetujulisha; naam, hapana hata mmoja aliyetuonyesha; naam, hapana hata mmoja aliyesikia maneno yenu.
Esaïe 41.22 Esaïe 45.21 Esaïe 44.7 Habakuk 2.18-2.20 Esaïe 43.9
27 Mimi kwanza nitauambia Sayuni, Tazama; hawa ndio; nami nitampa Yerusalemu mletaji wa habari njema.
Esaïe 40.9 Esaïe 52.7 Nahum 1.15 Esaïe 44.28 Esaïe 48.12
28 Na nitazamapo, hapana mtu, hata katika watu hao hapana mshauri mmoja, ambaye, nikimwuliza, aweza kunijibu neno.
Esaïe 63.5 Esaïe 40.13-40.14 Esaïe 59.16 Daniel 2.10-2.11 Daniel 4.7-4.8
29 Tazama, hao wote ni ubatili; kazi zao si kitu; sanamu zao ni upepo na fujo.
Esaïe 41.24 Jérémie 5.13 Jérémie 10.2-10.16 Psaumes 115.4-115.8 Esaïe 44.9-44.20

Cette Bible est dans le domaine public.