Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 22.18
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Jérusalem

1 Ufunuo juu ya bonde la maono. Sasa una nini, wewe, Hata umepanda pia juu ya dari za nyumba?
Jérémie 21.13 Psaumes 125.2 Esaïe 15.3 Joël 3.12 Joël 3.14
2 Ewe uliyejaa makelele, Mji wa ghasia, mji wenye furaha; Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga, Wala hawakufa vitani.
Esaïe 32.13 Jérémie 14.18 Lamentations 2.20 Esaïe 23.7 Esaïe 37.33
3 Wakuu wako wote wamekimbia pamoja, Wamefungwa wasiutumie upinde. Wote walioonekana wamefungwa pamoja, Wamekimbia mbali sana.
Jérémie 52.24-52.27 Esaïe 3.1-3.8 2 Rois 25.4-25.7 Jérémie 39.4-39.7 2 Rois 25.18-25.21
4 Kwa sababu hiyo nasema, Geuza uso wako usinitazame, nipate kulia kwa uchungu; usijishughulishe kunifariji, kwa ajili ya kuharibika kwake binti ya watu wangu.
Jérémie 9.1 Michée 1.8 Jérémie 13.17 Ruth 1.20-1.21 Jérémie 6.26
5 Kwa maana siku ya kutaabika, siku ya kukanyagwa, siku ya fujo inakuja, itokayo kwa Bwana, Bwana wa majeshi, katika bonde la Maono; inabomoa kuta; na kuililia milima.
Esaïe 10.6 Michée 7.4 Esaïe 37.3 Lamentations 1.5 Lamentations 2.2
6 Na Elamu wameshika podo, pamoja na magari ya vita, na watu wenye kupanda farasi; na Kiri wameifunua ngao.
2 Rois 16.9 Esaïe 21.2 Amos 9.7 Amos 1.5 Jérémie 49.35-49.39
7 Hata ikawa mabonde yako mateule yamejaa magari ya vita, nao wapandao farasi wamejipanga wakielekea malango.
Esaïe 37.34 Esaïe 10.28-10.32 Esaïe 8.7-8.8 Jérémie 39.1-39.3
8 Kisha alikiondoa kifuniko cha Yuda, nawe siku hiyo ulivitazama vyombo vya vita katika nyumba ya mwituni.
1 Rois 7.2 1 Rois 10.17 Esaïe 36.1-36.3 Cantique 4.4 1 Rois 14.27-14.28
9 Nanyi mlipaona mahali palipobomoka katika mji wa Daudi ya kuwa ni pengi, nanyi mliyakusanya maji ya birika la chini.
2 Rois 20.20 Néhémie 3.16 2 Chroniques 32.1-32.6 2 Chroniques 32.30
10 Nanyi mlizihesabu nyumba za Yerusalemu, mkazibomoa nyumba ili kuutia nguvu ukuta.
11 Nanyi mlifanya birika la maji katikati ya kuta mbili, la kuwekea maji ya birika la kale; lakini hamkumwangalia yeye aliyeyafanya hayo, wala kumjali yeye aliyeyatengeneza zamani.
2 Rois 25.4 Jérémie 33.2-33.3 Esaïe 37.26 Esaïe 17.7 Néhémie 3.16
12 Siku hiyo Bwana, Bwana wa majeshi, akawaita watu walie na kuomboleza, na kung’oa nywele zao, na kuvaa nguo za magunia;
Joël 2.17 Joël 1.13 Michée 1.16 Jacques 4.8-4.10 Ecclésiaste 3.4
13 na kumbe! Furaha, na kuchekelea, na kuchinja ng’ombe, na kuchinja kondoo, na kula nyama, na kunywa mvinyo; tule, tunywe, kwa maana kesho tutakufa.
Esaïe 56.12 1 Corinthiens 15.32 Luc 17.26-17.29 Esaïe 28.7-28.8 Esaïe 21.4-21.5
14 Na yeye Bwana wa majeshi akafunua haya masikioni mwangu, Ni kweli, uovu huu hautatakaswa wala kuwatokeni hata mfe; asema Bwana, Bwana wa majeshi.
Esaïe 5.9 1 Samuel 3.14 Ezéchiel 24.13 Esaïe 13.11 Nombres 15.25-15.31
15 Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi, Haya! Enenda kwa huyu mtunza hazina, yaani, Shebna, aliye juu ya nyumba, ukamwambie,
2 Rois 18.18 Esaïe 36.3 2 Rois 18.37 Esaïe 37.2 2 Rois 19.2
16 Unafanyaje hapa? Nawe una nani hapa? Hata ukachimba kaburi hapa; ukamchimbia kaburi huko juu, na kumchongea makao katika jabali!
Matthieu 27.60 2 Samuel 18.18 2 Chroniques 16.14 Job 3.14 Michée 2.10
17 Tazama, Bwana atakutupa kwa nguvu, kama mtu mwenye nguvu; naam, atakuzonga-zonga.
Esther 7.8 Jérémie 14.3 Job 9.24
18 Hakika atakukunja na kukutupa kama mpira, mpaka nchi iliyo mbali; huko utakufa, na magari ya utukufu wako yatakuwa kuko huko, ewe uliye aibu ya nyumba ya bwana wako.
Esaïe 17.13 Amos 7.17
19 Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo.
Job 40.11-40.12 Ezéchiel 17.24 Luc 1.52 Psaumes 75.6-75.7
20 Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia;
2 Rois 18.18 Esaïe 36.3 Esaïe 37.2 Esaïe 36.22 2 Rois 18.37
21 nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nyumba ya Yuda.
Genèse 45.8 Esther 8.15 Genèse 41.42-41.43 1 Samuel 18.4 Esther 8.2
22 Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.
Apocalypse 3.7 Job 12.14 Apocalypse 1.18 Matthieu 18.18-18.19 Matthieu 16.18-16.19
23 Nami nitamkaza kama msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.
Job 36.7 Zacharie 10.4 Esdras 9.8 1 Samuel 2.8 Apocalypse 3.21
24 Nao wataangika juu yake utukufu wote wa nyumba ya baba yake; wazao wake na watoto wao, kila chombo kidogo tangu vyombo vya vikombe hata vyombo vya makopo vyote pia.
2 Timothée 2.20-2.21 Daniel 6.1-6.3 Romains 9.22-9.23 Jean 5.22-5.27 Jean 20.21-20.23
25 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, ule msumari uliokazwa katika mahali palipo imara utalegea; nao utakatwa na kuanguka chini, na ule mzigo uliokuwa juu yake utakatiliwa mbali; maana Bwana amesema haya.
Michée 4.4 Esaïe 46.11 Esther 9.24-9.25 Esaïe 22.23 Psaumes 146.3

Cette Bible est dans le domaine public.