Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 2.13
Bible en Swahili de l’est


Gloire future de Jérusalem

1 Hili ni neno aliloliona Isaya mwana wa Amozi katika habari za Yuda na Yerusalemu.
Esaïe 1.1 Michée 6.9 Esaïe 13.1 Habakuk 1.1 Michée 1.1
2 Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi.
Michée 4.1-4.3 Esaïe 56.7 Esaïe 27.13 Hébreux 1.2 Zacharie 8.3
3 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu.
Luc 24.47 Zacharie 8.20-8.23 Esaïe 51.4-51.5 Jean 7.17 Psaumes 110.2
4 Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.
Joël 3.10 Osée 2.18 Zacharie 9.10 Esaïe 9.7 Esaïe 11.6-11.9
5 Enyi wa nyumba ya Israeli, njoni, twende katika nuru ya Bwana.
Ephésiens 5.8 1 Jean 1.7 Esaïe 50.10-50.11 Esaïe 60.19-60.20 Luc 1.79

Jugement des idolâtres et des orgueilleux

6 Maana wewe umewaacha watu wako, nyumba ya Israeli, kwa sababu wamejaa kawaida za mashariki, nao ni wapiga ramli kama Wafilisti, na wanapana mikono na wana wa wageni.
2 Rois 1.2 Romains 11.20 1 Chroniques 10.13 Nombres 23.7 Lamentations 5.20
7 Tena nchi yao imejaa fedha na dhahabu, wala hapana mwisho wa hazina zao; tena nchi yao imejaa farasi, wala hapana mwisho wa magari yao.
Esaïe 30.16 Esaïe 31.1 Deutéronome 17.16-17.17 Michée 5.10 Jacques 5.1-5.3
8 Tena nchi yao imejaa sanamu; huabudu kazi ya mikono yao, vitu vilivyofanywa kwa vidole vyao wenyewe.
Jérémie 2.28 Psaumes 115.4-115.8 Esaïe 37.19 2 Chroniques 33.3-33.7 Esaïe 10.10-10.11
9 Mtu mnyonge huinama, na mtu mkubwa hujidhili; kwa hiyo usiwasamehe.
Esaïe 5.15 Psaumes 49.2 Esaïe 57.9 Colossiens 2.23 Néhémie 4.5
10 Ingia ndani ya jabali; ukajifiche mavumbini mbele za utisho wa Bwana, mbele za utukufu wa enzi yake.
Apocalypse 6.15-6.16 Luc 12.5 Luc 23.30 Psaumes 90.11 Osée 10.8
11 Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye Bwana, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.
Psaumes 18.27 Esaïe 5.15-5.16 Esaïe 24.21 Esaïe 12.4 Esaïe 13.11
12 Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.
Malachie 4.1 Jérémie 46.10 Luc 14.11 1 Thessaloniciens 5.2 Esaïe 24.4
13 Na juu ya mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu na kuinuka, na juu ya mialoni yote ya Bashani;
Esaïe 14.8 Zacharie 11.1-11.2 Esaïe 10.33-10.34 Amos 2.5 Esaïe 37.24
14 na juu ya milima mirefu yote, na juu ya vilima vyote vilivyoinuka;
Esaïe 30.25 Esaïe 40.4 Psaumes 110.5-110.6 2 Corinthiens 10.5 Psaumes 68.16
15 na juu ya kila mnara mrefu, na juu ya kila ukuta ulio na boma;
Esaïe 25.12
16 na juu ya merikebu zote za Tarshishi, na juu ya kila taswira ipendezayo.
1 Rois 10.22 Esaïe 23.1 Psaumes 47.7 Nombres 33.52 Apocalypse 18.17-18.19
17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye Bwana, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.
Esaïe 2.11 Esaïe 13.11 Ezéchiel 28.2-28.7 Jérémie 48.29-48.30
18 Nazo sanamu zitatoweka kabisa.
Zacharie 13.2 Esaïe 27.9 Sophonie 1.3 Ezéchiel 37.23 Ezéchiel 36.25
19 Na watu wataingia ndani ya pango za majabali, na ndani ya mashimo ya nchi, mbele za utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.
Esaïe 2.10 Hébreux 12.26 Esaïe 2.21 Luc 23.30 Aggée 2.6
20 Siku hiyo kila mtu atazitupilia mbali sanamu zake za fedha, na sanamu zake za dhahabu, walizojifanyia ili kuziabudu, kwa fuko na popo;
Esaïe 31.7 Esaïe 30.22 Lévitique 11.19 Esaïe 46.6 Osée 14.8
21 ili aingie ndani ya pango za majabali, na ndani ya tundu za miamba iliyopasuka, mbele za utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.
Esaïe 2.19 Exode 33.22 Esaïe 2.10 Cantique 2.14 Job 30.6
22 Mwacheni mwanadamu ambaye pumzi yake i katika mianzi ya pua yake; kwa maana hudhaniwaje kuwa ni kitu?
Psaumes 146.3 Jérémie 17.5 Psaumes 144.3-144.4 Jacques 4.14 Psaumes 8.4

Cette Bible est dans le domaine public.