Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 73.19
Bible en Swahili de l’est


Troisième livre

Perplexité face au bonheur des impies

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.
Matthieu 5.8 Luc 12.32 Psaumes 84.11 Jean 1.47 Psaumes 51.10
2 Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.
Psaumes 94.18 1 Samuel 2.9 Psaumes 116.8 Psaumes 38.16 Psaumes 17.15
3 Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna, Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki.
Job 21.7 Jérémie 12.1 Psaumes 37.1 Psaumes 37.7 Proverbes 23.17
4 Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu.
Psaumes 17.10 Job 24.20 Ecclésiaste 2.16 Psaumes 17.14 Ecclésiaste 7.15
5 Katika taabu ya watu hawamo, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu.
Psaumes 73.12 Jérémie 12.1-12.2 Job 21.9 Hébreux 12.8 Job 21.6
6 Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo.
Psaumes 109.18 Juges 8.26 Proverbes 1.9 Deutéronome 8.13-8.14 Jérémie 48.11
7 Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.
Psaumes 17.10 Job 15.27 Jérémie 5.28 Psaumes 119.70 Luc 12.16-12.19
8 Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.
Jude 1.16 Psaumes 17.10 Exode 1.9-1.10 1 Samuel 13.19 1 Rois 21.7-21.29
9 Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.
Apocalypse 13.6 Psaumes 52.4 Job 21.14 Daniel 7.25 Jacques 3.6
10 Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao.
Psaumes 75.8
11 Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?
Osée 7.2 Psaumes 139.1-139.6 Sophonie 1.12 Ezéchiel 8.12 Job 22.13-22.14
12 Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.
Psaumes 52.7 Jérémie 5.17 Psaumes 37.35 Jérémie 12.1-12.2 Psaumes 62.10
13 Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa.
Job 34.9 Psaumes 26.6 Job 21.15 Job 35.3 Malachie 3.14
14 Maana mchana kutwa nimepigwa, Na kuadhibiwa kila asubuhi.
Psaumes 34.19 Job 10.3 Jérémie 15.18 Job 7.3-7.4 Hébreux 12.5
15 Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.
Romains 14.15 1 Samuel 2.24 1 Corinthiens 8.11-8.13 1 Pierre 2.9 Matthieu 18.6-18.7
16 Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; Ikawa taabu machoni pangu;
Ecclésiaste 8.17 Psaumes 36.6 Psaumes 97.2 Romains 11.33 Jean 16.18-16.19
17 Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, Nikautafakari mwisho wao.
Psaumes 77.13 Psaumes 27.4 Job 27.8 Jérémie 5.31 Psaumes 119.24
18 Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika.
Psaumes 35.6 Psaumes 55.23 2 Thessaloniciens 1.9 Psaumes 37.20 Deutéronome 32.35
19 Namna gani wamekuwa ukiwa mara! Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.
Apocalypse 18.10 Esaïe 21.3-21.4 1 Thessaloniciens 5.3 Nombres 17.12-17.13 Job 15.21
20 Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka, Uondokapo utaidharau sanamu yao.
Psaumes 78.65 Job 20.8 Psaumes 7.6 Psaumes 39.6 Esaïe 29.7-29.8
21 Moyo wangu ulipoona uchungu, Viuno vyangu viliponichoma,
Psaumes 73.3 Psaumes 37.1 Job 16.13 Psaumes 37.7 Lamentations 3.13
22 Nalikuwa kama mjinga, sijui neno; Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako.
Ecclésiaste 3.18 Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Psaumes 69.5 Esaïe 1.3
23 Walakini mimi ni pamoja nawe daima, Umenishika mkono wa kuume.
Esaïe 41.13 Psaumes 63.8 Psaumes 23.4 Psaumes 16.8 Psaumes 139.1-139.12
24 Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.
Psaumes 32.8 Psaumes 49.15 Esaïe 58.11 Psaumes 48.14 Jean 17.5
25 Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.
Philippiens 3.8 Psaumes 63.3 Matthieu 5.8 Psaumes 16.2 Psaumes 17.15
26 Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.
Psaumes 18.2 Psaumes 84.2 Psaumes 16.5-16.6 Esaïe 40.29-40.31 Psaumes 40.12
27 Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe.
Psaumes 119.155 Exode 34.15 Nombres 15.39 Jacques 4.4 Jérémie 12.2
28 Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, Niyahubiri matendo yako yote.
Jacques 4.8 Psaumes 65.4 Psaumes 118.17 Psaumes 84.10 1 Pierre 3.18

Cette Bible est dans le domaine public.