Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 73.10
Bible en Swahili de l’est


Troisième livre

Perplexité face au bonheur des impies

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.
Matthieu 5.8 Psaumes 84.11 Luc 12.32 Jean 1.47 Psaumes 51.10
2 Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.
Psaumes 94.18 1 Samuel 2.9 Psaumes 17.15 Psaumes 17.5 Psaumes 116.8
3 Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna, Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki.
Job 21.7 Jérémie 12.1 Psaumes 37.1 Psaumes 37.7 Proverbes 23.17
4 Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu.
Ecclésiaste 7.15 Luc 16.22 Job 21.23-21.24 Psaumes 17.10 Job 24.20
5 Katika taabu ya watu hawamo, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu.
Psaumes 73.12 Jérémie 12.1-12.2 Job 21.9 1 Corinthiens 11.32 Proverbes 3.11-3.12
6 Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo.
Psaumes 109.18 Juges 8.26 Proverbes 1.9 Michée 2.1-2.2 Cantique 4.9
7 Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.
Job 15.27 Psaumes 17.10 Jérémie 5.28 1 Samuel 25.36 Esaïe 3.9
8 Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.
Jude 1.16 Psaumes 12.4-12.5 Proverbes 30.13-30.14 Psaumes 17.10 Exode 1.9-1.10
9 Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.
Apocalypse 13.6 Luc 18.4 Exode 5.2 Daniel 3.15 Psaumes 52.4
10 Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao.
Psaumes 75.8
11 Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?
Psaumes 73.9 Psaumes 44.21 Psaumes 10.11 Osée 7.2 Psaumes 139.1-139.6
12 Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.
Psaumes 52.7 Jérémie 5.28 Psaumes 17.14 Luc 16.19 Jérémie 5.17
13 Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa.
Job 34.9 Psaumes 26.6 Job 21.15 Job 35.3 Jacques 4.8
14 Maana mchana kutwa nimepigwa, Na kuadhibiwa kila asubuhi.
1 Pierre 1.6 Amos 3.2 Psaumes 94.12 Psaumes 34.19 Job 10.3
15 Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.
Psaumes 22.30 Psaumes 24.6 Romains 14.21 Romains 14.15 1 Samuel 2.24
16 Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; Ikawa taabu machoni pangu;
Ecclésiaste 8.17 Luc 18.32-18.34 Psaumes 39.6 Psaumes 36.6 Psaumes 97.2
17 Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, Nikautafakari mwisho wao.
Psaumes 77.13 Psaumes 27.4 Ecclésiaste 8.12-8.13 Luc 16.22-16.23 Job 27.8
18 Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika.
Psaumes 35.6 Psaumes 92.7 Psaumes 37.35-37.38 Jérémie 23.12 Psaumes 55.23
19 Namna gani wamekuwa ukiwa mara! Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.
1 Samuel 28.20 Esaïe 47.11 Job 20.23-20.25 Apocalypse 18.10 Esaïe 21.3-21.4
20 Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka, Uondokapo utaidharau sanamu yao.
Job 20.8 Psaumes 78.65 Psaumes 90.5 Psaumes 7.6 Psaumes 39.6
21 Moyo wangu ulipoona uchungu, Viuno vyangu viliponichoma,
Lamentations 3.13 Psaumes 73.3 Psaumes 37.1 Job 16.13 Psaumes 37.7
22 Nalikuwa kama mjinga, sijui neno; Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako.
Ecclésiaste 3.18 Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Job 18.3 Psaumes 69.5
23 Walakini mimi ni pamoja nawe daima, Umenishika mkono wa kuume.
Esaïe 41.13 Psaumes 63.8 Psaumes 23.4 Psaumes 16.8 Psaumes 139.1-139.12
24 Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.
Psaumes 32.8 Psaumes 49.15 Esaïe 58.11 Psaumes 48.14 Jean 17.5
25 Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.
Philippiens 3.8 Psaumes 63.3 Matthieu 5.8 Psaumes 16.2 Psaumes 17.15
26 Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.
Psaumes 84.2 Psaumes 18.2 Psaumes 16.5-16.6 Esaïe 40.29-40.31 Psaumes 40.12
27 Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe.
Psaumes 119.155 Nombres 15.39 Exode 34.15 Jacques 4.4 Ephésiens 2.17
28 Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, Niyahubiri matendo yako yote.
Jacques 4.8 Psaumes 65.4 Psaumes 118.17 Lamentations 3.25-3.26 Psaumes 84.10

Cette Bible est dans le domaine public.