Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 44.7
Bible en Swahili de l’est


Prière d’Israël opprimé

1 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu Baba zetu wametuambia, Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale.
Exode 13.14-13.15 Psaumes 78.3-78.6 Psaumes 42.1 Esaïe 38.19 Job 15.17-15.19
2 Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa, Ukawakalisha wao. Wewe uliwatesa watu wa nchi, Ukawaeneza wao.
Psaumes 78.55 Exode 15.17 Psaumes 135.10-135.12 Nombres 13.32 Exode 34.11
3 Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi, Wala si mkono wao uliowaokoa; Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako, Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.
Deutéronome 7.7-7.8 Josué 24.12 Deutéronome 8.17-8.18 1 Samuel 12.22 Esaïe 63.12
4 Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu, Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo.
Psaumes 74.12 Psaumes 42.8 Marc 9.25 Marc 1.25-1.26 Marc 1.41
5 Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu; Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao.
Psaumes 108.13 Psaumes 60.12 Deutéronome 33.17 Psaumes 118.10-118.13 Esaïe 41.14-41.16
6 Maana sitautumainia upinde wangu, Wala upanga wangu hautaniokoa.
Osée 1.7 Psaumes 33.16-33.17 Psaumes 20.7 1 Samuel 17.47
7 Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu; Na watuchukiao umewaaibisha.
Josué 11.6 Josué 10.8-10.10 Juges 7.4-7.7 Juges 2.18 Psaumes 53.5
8 Tumejisifia Mungu mchana kutwa, Na jina lako tutalishukuru milele.
Psaumes 34.2 1 Corinthiens 1.29-1.31 Jérémie 9.24 Romains 2.17 Esaïe 45.25
9 Lakini umetutupa, umetufedhehesha, Wala hutoki na majeshi yetu.
Psaumes 60.10 Psaumes 74.1 Psaumes 60.1 Psaumes 108.11 Psaumes 43.2
10 Waturudisha nyuma tukampa mtesi kisogo, Na watuchukiao wanajipatia mateka.
Lévitique 26.17 Josué 7.8 Psaumes 89.41 Josué 7.12 Deutéronome 28.25
11 Umetutoa kama kondoo tuwe chakula, Na kututawanya kati ya mataifa.
Deutéronome 28.64 Romains 8.36 Deutéronome 4.27 Psaumes 60.1 Esaïe 11.11-11.12
12 Wawauza watu wako bila kupata mali, Wala hukupata faida kwa thamani yao.
Jérémie 15.13 Deutéronome 32.30 Esaïe 52.3-52.4 Apocalypse 18.13 Juges 2.14
13 Umetufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.
Psaumes 80.6 Psaumes 79.4 Psaumes 89.41 Psaumes 123.3-123.4 Psaumes 89.51
14 Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa, Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi.
Jérémie 24.9 Job 16.4 2 Rois 19.21 2 Chroniques 7.20 Esaïe 37.22
15 Mchana kutwa fedheha yangu i mbele yangu, Na haya ya uso wangu imenifunika,
Psaumes 69.7 Esdras 9.6 Josué 7.7-7.9 Jérémie 51.51 Psaumes 89.45
16 Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru, Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi.
Psaumes 8.2 Esaïe 37.3-37.4 Psaumes 74.22-74.23 Esaïe 37.17 Psaumes 79.12
17 Haya yote yametupata, bali hatukukusahau, Wala hatukulihalifu agano lako.
Daniel 9.13 Deutéronome 6.12 Psaumes 78.57 Esaïe 17.10 Psaumes 44.20
18 Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma, Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Psaumes 119.157 Psaumes 119.51 Psaumes 78.57 Sophonie 1.6 1 Corinthiens 15.58
19 Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu, Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.
Job 3.5 Psaumes 23.4 Psaumes 51.8 Matthieu 4.16 Job 30.29
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu;
Job 11.13 Psaumes 81.9 Psaumes 68.31 Psaumes 7.3-7.5 1 Rois 8.22
21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.
Jérémie 17.10 Hébreux 4.12-4.13 Psaumes 139.1-139.24 Job 31.4 Romains 2.16
22 Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa.
Romains 8.36 Jean 15.21 Psaumes 79.2-79.3 1 Corinthiens 15.30-15.31 Psaumes 44.11
23 Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe kabisa.
Psaumes 7.6 Psaumes 78.65 Psaumes 35.23 Psaumes 77.7 Psaumes 59.4-59.5
24 Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu?
Job 13.24 Psaumes 42.9 Psaumes 74.23 Psaumes 43.1-43.4 Psaumes 10.11
25 Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi.
Psaumes 119.25 Psaumes 66.11-66.12 Lamentations 4.5 Esaïe 51.23
26 Uondoke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
Psaumes 25.22 Psaumes 26.11 Psaumes 130.7-130.8 Psaumes 35.2

Cette Bible est dans le domaine public.