1 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu Baba zetu wametuambia, Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale.
Psaumes 42.1 Exode 13.14-13.15 Psaumes 78.3-78.6 Psaumes 77.5 Nombres 21.27-21.30
2 Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa, Ukawakalisha wao. Wewe uliwatesa watu wa nchi, Ukawaeneza wao.Exode 15.17 Psaumes 78.55 Psaumes 135.10-135.12 Josué 24.12 Psaumes 80.8-80.11
3 Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi, Wala si mkono wao uliowaokoa; Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako, Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.
Josué 24.12 Deutéronome 7.7-7.8 Deutéronome 8.17-8.18 Deutéronome 4.37-4.38 Psaumes 77.15
4 Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu, Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo.
Psaumes 74.12 Psaumes 42.8 Psaumes 89.18 Esaïe 33.22 Marc 1.31
5 Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu; Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao.
Psaumes 108.13 Deutéronome 33.17 Psaumes 60.12 Daniel 8.4 Zacharie 10.5
6 Maana sitautumainia upinde wangu, Wala upanga wangu hautaniokoa.
Osée 1.7 1 Samuel 17.47 Psaumes 33.16-33.17 Psaumes 20.7
7 Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu; Na watuchukiao umewaaibisha.
Psaumes 140.7 1 Samuel 17.47 Psaumes 40.14 Josué 10.42 1 Samuel 7.8-7.12
8 Tumejisifia Mungu mchana kutwa, Na jina lako tutalishukuru milele.
Psaumes 34.2 Jérémie 9.24 1 Corinthiens 1.29-1.31 Romains 2.17 Esaïe 45.25
9 Lakini umetutupa, umetufedhehesha, Wala hutoki na majeshi yetu.
Psaumes 60.10 Psaumes 108.11 Psaumes 74.1 Psaumes 60.1 Psaumes 43.2
10 Waturudisha nyuma tukampa mtesi kisogo, Na watuchukiao wanajipatia mateka.
Lévitique 26.17 Josué 7.8 Josué 7.12 Psaumes 89.41 Deutéronome 28.25
11 Umetutoa kama kondoo tuwe chakula, Na kututawanya kati ya mataifa.
Romains 8.36 Deutéronome 4.27 Deutéronome 28.64 Jérémie 12.3 2 Rois 17.6
12 Wawauza watu wako bila kupata mali, Wala hukupata faida kwa thamani yao.
Jérémie 15.13 Deutéronome 32.30 Esaïe 52.3-52.4 Juges 3.8 Apocalypse 18.13
13 Umetufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.
Psaumes 79.4 Psaumes 80.6 Deutéronome 28.37 Psaumes 89.41 Psaumes 123.3-123.4
14 Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa, Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi.
Jérémie 24.9 2 Rois 19.21 Job 16.4 Job 17.6 Psaumes 22.7
15 Mchana kutwa fedheha yangu i mbele yangu, Na haya ya uso wangu imenifunika,
Psaumes 69.7 Psaumes 71.13 Esdras 9.6 Josué 7.7-7.9 Jérémie 51.51
16 Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru, Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi.
Psaumes 8.2 Psaumes 74.18 Esaïe 37.3-37.4 Psaumes 74.22-74.23 Esaïe 37.17
17 Haya yote yametupata, bali hatukukusahau, Wala hatukulihalifu agano lako.
Daniel 9.13 Jérémie 31.32 Psaumes 78.7 Psaumes 9.17 Ezéchiel 20.37
18 Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma, Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Psaumes 119.51 Psaumes 119.157 Psaumes 78.57 Sophonie 1.6 Job 23.11-23.12
19 Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu, Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.
Job 3.5 Psaumes 23.4 Psaumes 51.8 Apocalypse 13.2 Ezéchiel 29.3
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu;
Psaumes 68.31 Job 11.13 Psaumes 81.9 Exode 9.29 Psaumes 78.11
21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.
Jérémie 17.10 Hébreux 4.12-4.13 Jérémie 23.24 1 Corinthiens 4.5 Psaumes 139.1-139.24
22 Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa.
Romains 8.36 Jean 15.21 1 Rois 19.10 Apocalypse 11.3-11.9 Jean 16.2-16.3
23 Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe kabisa.
Psaumes 78.65 Psaumes 7.6 Psaumes 35.23 Psaumes 88.14 Psaumes 74.1
24 Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu?
Job 13.24 Psaumes 13.1 Exode 2.23-2.24 Psaumes 10.1 Psaumes 42.9
25 Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi.
Psaumes 119.25 Psaumes 66.11-66.12 Lamentations 4.5 Esaïe 51.23
26 Uondoke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
Psaumes 25.22 Psaumes 26.11 Psaumes 130.7-130.8 Psaumes 35.2