Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 132.6
Bible en Swahili de l’est


Rappel des promesses de Dieu à David

1 Bwana, umkumbukie Daudi Taabu zake zote alizotaabika.
Psaumes 121.1 Psaumes 120.1 1 Samuel 18.1-18.30 Psaumes 125.1 Psaumes 123.1
2 Ndiye aliyemwapia Bwana, Akaweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.
Genèse 49.24 Esaïe 49.26 Psaumes 146.5-146.6 Psaumes 56.12 Psaumes 116.14-116.18
3 Sitaingia hemani mwa nyumba yangu, Wala sitapanda matandiko ya kitanda changu;
Matthieu 6.33 Aggée 1.4 Ecclésiaste 9.10
4 Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi, Wala kope zangu kusinzia;
Proverbes 6.4 Ruth 3.18 Genèse 24.33
5 Hata nitakapompatia Bwana mahali, Na Shujaa wa Yakobo maskani.
1 Chroniques 22.7 Ephésiens 2.22 Actes 7.46-7.49 2 Chroniques 2.6 2 Samuel 6.17
6 Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata, Katika konde la Yearimu tuliiona.
1 Samuel 17.12 1 Samuel 7.1 Ruth 1.2 Genèse 35.19 1 Chroniques 13.5-13.6
7 Na tuingie katika maskani yake, Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake.
Psaumes 99.5 Psaumes 5.7 Psaumes 122.1 Psaumes 95.6 Psaumes 66.13-66.14
8 Ee Bwana, uinuke, uende kwenye raha yako, Wewe na sanduku la nguvu zako.
2 Chroniques 6.41-6.42 Nombres 10.35-10.36 Psaumes 78.61 Psaumes 68.1
9 Makuhani wako na wavikwe haki, Watauwa wako na washangilie.
Job 29.14 Esaïe 61.10 Psaumes 132.16 Esaïe 65.14 Psaumes 35.26-35.27
10 Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako, Usiurudishe nyuma uso wa masihi
1 Rois 11.34 Psaumes 89.38-89.39 Psaumes 84.9 1 Rois 15.4-15.5 1 Rois 11.12-11.13
11 Bwana amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalihalifu, Baadhi ya wazao wa mwili wako Nitawaweka katika kiti chako cha enzi.
2 Samuel 7.12 Actes 2.30 Psaumes 110.4 Psaumes 89.3-89.4 2 Chroniques 6.16
12 Wanao wakiyashika maagano yangu, Na shuhuda nitakazowafundisha; Watoto wao nao wataketi Katika kiti chako cha enzi milele.
Esaïe 59.21 Actes 2.30 Psaumes 115.14 Psaumes 102.28 Luc 1.32-1.33
13 Kwa kuwa Bwana ameichagua Sayuni, Ameitamani akae ndani yake.
Psaumes 68.16 Psaumes 76.1-76.2 Psaumes 78.68-78.69 Hébreux 12.22 Psaumes 48.1-48.3
14 Hapo ndipo mahali pangu pa raha milele, Hapo nitakaa kwa maana nimepatamani.
Esaïe 66.1 Psaumes 132.8 Psaumes 87.2 Apocalypse 21.23 Ephésiens 2.22
15 Hakika nitavibariki vyakula vyake Wahitaji wake nitawashibisha chakula.
Psaumes 147.14 Proverbes 3.9-3.10 Exode 23.25 Psaumes 36.8 Aggée 2.16-2.19
16 Na makuhani wake nitawavika wokovu, Na watauwa wake watashangilia.
2 Chroniques 6.41 Psaumes 132.9 Esaïe 61.10 Osée 11.12 Psaumes 140.4
17 Hapo nitamchipushia Daudi pembe, Na taa nimemtengenezea masihi wangu.
Luc 1.69 2 Chroniques 21.7 1 Rois 11.36 Ezéchiel 29.21 1 Rois 15.4
18 Adui zake nitawavika aibu, Bali juu yake taji yake itasitawi.
Job 8.22 Psaumes 109.29 Psaumes 35.26 Psaumes 21.8-21.9 Psaumes 72.8-72.11

Cette Bible est dans le domaine public.