Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 105.34
Bible en Swahili de l’est


La fidélité de Dieu envers Israël

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana,liitieni jina ,Wajulisheni watu matendo yake.
Esaïe 12.4 Psaumes 99.6 Daniel 4.1-4.3 Psaumes 145.11-145.12 Joël 2.32
2 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote.
Psaumes 119.27 Psaumes 77.12 Psaumes 98.5 Psaumes 47.6-47.7 Deutéronome 6.6-6.9
3 Jisifuni kwa jina lake takatifu, Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
Luc 11.9-11.10 Psaumes 9.10 Esaïe 45.25 Galates 6.14 Esaïe 45.19
4 Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote.
Psaumes 27.8 Psaumes 78.61 Amos 5.4-5.6 Sophonie 2.2-2.3 2 Chroniques 6.41
5 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya, Miujiza yake na hukumu za kinywa chake.
Psaumes 77.11 Psaumes 119.13 Esaïe 43.18-43.19 1 Corinthiens 11.24-11.26 Deutéronome 8.2
6 Enyi wazao wa Ibrahimu, mtumishi wake; Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Esaïe 41.14 Psaumes 105.42 Romains 9.4-9.29 Exode 3.6 Psaumes 106.5
7 Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.
Esaïe 26.9 Apocalypse 15.4 Josué 24.15-24.24 Psaumes 95.7 Psaumes 100.3
8 Analikumbuka agano lake milele; Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
Psaumes 111.5 Deutéronome 7.9 Psaumes 106.45 Psaumes 105.42 Psaumes 111.9
9 Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka.
Genèse 17.2 Genèse 26.3 Genèse 22.16-22.18 Genèse 28.13 Actes 7.8
10 Alilomthibitishia Yakobo liwe amri, Na Israeli liwe agano la milele.
Genèse 28.13-28.15 Genèse 17.7-17.8 2 Samuel 23.5 Hébreux 13.20
11 Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani, Iwe urithi wenu mliopimiwa.
Genèse 15.18 Genèse 13.15 Psaumes 78.55 Genèse 26.3-26.4 Genèse 28.13
12 Walipokuwa watu wawezao kuhesabiwa, Naam, watu wachache na wageni ndani yake,
Genèse 34.30 Hébreux 11.9 Deutéronome 7.7 Genèse 23.4 Deutéronome 26.5
13 Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa, Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
14 Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao.
Genèse 35.5 Exode 7.16-7.17 Genèse 31.24-31.29 Genèse 26.14-26.33 Genèse 20.1-20.7
15 Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
Genèse 26.11 1 Jean 2.27 Genèse 49.8-49.33 Genèse 20.7 Genèse 48.19-48.20
16 Akaiita njaa iijilie nchi, Akakiharibu chakula chote walichokitegemea.
Esaïe 3.1 Ezéchiel 4.16 Lévitique 26.26 Genèse 41.54 Psaumes 104.15
17 Alimpeleka mtu mbele yao, Yusufu aliuzwa utumwani.
Actes 7.9 Genèse 37.36 Genèse 50.20 Genèse 39.1 Genèse 37.27-37.28
18 Walimwumiza miguu yake kwa pingu, Akatiwa katika minyororo ya chuma.
Genèse 40.15 Genèse 39.20 Actes 16.24 Psaumes 107.10
19 Hata wakati wa kuwadia neno lake, Ahadi ya Bwana ilimjaribu.
Proverbes 21.1 Genèse 40.20-40.21 Actes 7.10 Psaumes 44.4 Daniel 2.30
20 Mfalme alituma watu akamfungua, Mkuu wa watu akamwachia.
Genèse 41.14
21 Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake, Na mwenye amri juu ya mali zake zote.
Genèse 41.40-41.44 Genèse 45.26 Genèse 45.8 Genèse 41.55
22 Awafunge masheki wake kama apendavyo, Na kuwafundisha wazee wake hekima.
Esaïe 19.11 Genèse 41.38 Genèse 41.44 Genèse 41.33
23 Israeli naye akaingia Misri, Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.
Psaumes 106.22 Psaumes 78.51 Actes 13.17 Genèse 47.28 Genèse 46.2-46.7
24 Akawajalia watu wake wazae sana, Akawafanya kuwa hodari kuliko watesi wao.
Deutéronome 26.5 Actes 7.17 Exode 12.37 Genèse 46.3 Hébreux 11.12
25 Akawageuza moyo wawachukie watu wake, Wakawatendea hila watumishi wake.
Actes 7.19 Exode 1.16 Exode 2.23 Exode 4.21 Exode 9.16
26 Akamtuma Musa, mtumishi wake, Na Haruni ambaye amemchagua.
Exode 3.10 Exode 28.29-28.38 Exode 29.5-29.46 Exode 28.12 Exode 28.1-28.2
27 Akaweka mambo ya ishara zake kati yao, Na miujiza katika nchi ya Hamu.
Psaumes 78.43-78.51 Psaumes 105.28 Exode 7.1-7.11 Psaumes 106.22 Psaumes 105.23
28 Alituma giza, kukafunga giza, Wala hawakuyaasi maneno yake.
Psaumes 99.7 Joël 2.2 Exode 10.21-10.23 2 Pierre 2.4 Ezéchiel 2.4-2.8
29 Aliyageuza maji yao yakawa damu, Akawafisha samaki wao.
Exode 7.20-7.21 Psaumes 78.44 Esaïe 50.2 Apocalypse 16.3 Ezéchiel 29.4-29.5
30 Nchi yao ilijaa vyura, Vyumbani mwa wafalme wao.
Apocalypse 16.13-16.14 Exode 8.3-8.14 Psaumes 78.45
31 Alisema, kukaja makundi ya mainzi, Na chawa mipakani mwao mwote.
Exode 8.16-8.18 Exode 8.21-8.24 Psaumes 78.45 Esaïe 7.18
32 Badala ya mvua aliwapa mvua ya mawe, Na moto wa miali katika nchi yao.
Psaumes 78.47-78.48 Apocalypse 11.19 Apocalypse 8.7 Apocalypse 16.21 Exode 9.18-9.28
33 Akaipiga mizabibu yao na mitini yao, Akaivunja miti ya mipaka yao.
Apocalypse 9.4 Psaumes 78.47
34 Alisema, kukaja nzige, Na tunutu wasiohesabika;
Exode 10.12-10.15 Psaumes 78.46 Joël 2.25 Joël 1.4-1.7 Apocalypse 9.3-9.10
35 Wakaila miche yote ya nchi yao, Wakayala matunda ya ardhi yao.
36 Akawapiga wazaliwa wa kwanza katika nchi, Malimbuko ya nguvu zao.
Psaumes 135.8 Psaumes 136.10 Psaumes 78.51 Genèse 49.3 Exode 12.29-12.30
37 Akawatoa hali wana fedha na dhahabu, Katika kabila zao asiwepo mwenye kukwaa.
Exode 12.35-12.36 Actes 13.17 Genèse 15.14 Exode 3.22
38 Misri ilifurahi walipoondoka, Maana kwa ajili yao hofu imewaangukia.
Exode 15.16 Exode 12.33 Genèse 35.5 Josué 2.9 Exode 10.7
39 Alitandaza wingu liwe funiko, Na moto utoe nuru usiku.
Néhémie 9.12 Esaïe 4.5 Psaumes 78.14 1 Corinthiens 10.1-10.2 Exode 13.21-13.22
40 Walipotaka akaleta kware, Akawashibisha chakula cha mbinguni.
Psaumes 78.18 Jean 6.31-6.33 Nombres 11.4-11.9 Josué 5.12 Exode 16.12-16.35
41 Akaufunua mwamba, kukabubujika maji, Yakapita pakavuni kama mto.
Exode 17.6 Nombres 20.11 1 Corinthiens 10.4 Esaïe 48.21 Psaumes 78.15-78.16
42 Maana alilikumbuka neno lake takatifu, Na Ibrahimu, mtumishi wake.
Exode 2.24 Luc 1.72-1.73 Genèse 13.14-13.17 Exode 32.13 Deutéronome 9.5
43 Akawatoa watu wake kwa shangwe, Na wateule wake kwa nyimbo za furaha.
Esaïe 63.11-63.14 Esaïe 35.10 Jérémie 31.11-31.12 Psaumes 78.52-78.53 Deutéronome 4.37-4.38
44 Akawapa nchi za mataifa, wakairithi kazi ya watu;
Psaumes 78.55 Josué 24.13 Josué 11.23 Deutéronome 6.10-6.11 Psaumes 80.8
45 Ili wazishike amri zake, na kuzitii sheria zake. Haleluya.
Deutéronome 4.40 Ezéchiel 36.24-36.28 Psaumes 106.1 Ephésiens 2.8-2.10 Tite 2.14

Cette Bible est dans le domaine public.