Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 32.17
Bible en Swahili de l’est


Intervention d’Élihu

Reproches à Job et à ses amis

1 Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwenye haki machoni pake mwenyewe.
Job 10.7 Job 33.9 Job 23.7 Job 10.2 Job 27.4-27.6
2 Ndipo zikawaka hasira za huyo Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, katika jamaa ya Ramu, juu ya Ayubu, kwa sababu alikuwa amejipa haki mwenyewe zaidi ya Mungu.
Genèse 22.21 Job 35.2 Job 40.8 Job 27.5 Psaumes 69.9
3 Tena hasira zake ziliwaka juu ya hao rafiki zake watatu kwa sababu hawakupata jawabu, lakini wamemhukumia Ayubu makosa.
Job 8.6 Job 22.5-22.30 Job 15.34 Job 32.1 Job 26.2-26.4
4 Basi huyo Elihu alikuwa anangoja ili anene na Ayubu, kwa sababu hao wengine walikuwa wazee kuliko yeye.
Job 32.11-32.12 Proverbes 18.13
5 Hata Elihu alipoona kuwa hapana jawabu katika vinywa vya watu hao watatu, hasira zake ziliwaka.
Job 32.2 Exode 32.19
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, akajibu, na kusema, Mimi ni kijana, na ninyi ni wazee sana; Kwa hiyo nilijizuia, nisithubutu kuwaonyesha nionavyo.
Job 15.10 1 Timothée 5.1 1 Pierre 5.5 Lévitique 19.32 Job 15.7
7 Nilisema, Yafaa siku ziseme, Na wingi wa miaka ufundishe hekima.
Proverbes 16.31 Job 12.12 Proverbes 1.1-1.4 Hébreux 5.12 1 Rois 12.6-12.8
8 Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.
Proverbes 2.6 Job 33.4 Jacques 1.5 Job 38.36 Ecclésiaste 2.26
9 Sio wakuu walio wenye akili, Wala sio wazee watambuao hukumu.
Matthieu 11.25 Job 12.20 Jérémie 5.5 Jean 7.48 Jacques 2.6-2.7
10 Basi nilisema, Nisikilizeni mimi; Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.
1 Corinthiens 7.25 1 Corinthiens 7.40
11 Tazama, niliyangojea maneno yenu, Nilizisikiliza nisikie hoja zenu, Hapo mlipokitafuta mtakalonena.
Ecclésiaste 12.9-12.10 Job 5.27 Job 29.23 Job 32.4 Proverbes 28.11
12 Naam, niliwasikiza ninyi, Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu, Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.
Job 32.3 1 Timothée 1.7
13 Jitunzeni msiseme, Sisi tumepata hekima; Mungu yumkini akamshinda, si mtu;
Jérémie 9.23 1 Corinthiens 1.19-1.21 Ezéchiel 28.3 Job 19.6 Jean 19.11
14 Kwa kuwa yeye hajayaelekeza maneno yake kwangu; Wala sitamjibu mimi kwa maneno yenu.
15 Wameshangaa, hawajibu tena; Hawana neno la kusema.
Matthieu 7.23 Job 29.22 Matthieu 22.46 Job 6.24-6.25 Matthieu 22.34
16 Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni, Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;
Jacques 1.19 Job 13.5 Proverbes 17.28 Amos 5.13
17 Mimi nami nitajibu sehemu yangu, Mimi nami nitaonyesha nionavyo.
Job 32.10 Job 33.12 Job 35.3-35.4
18 Kwa kuwa nimejaa maneno; Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.
Psaumes 39.3 Ezéchiel 3.14-3.27 Actes 4.20 2 Corinthiens 5.13-5.14 Jérémie 20.9
19 Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa; Kama viriba vipya li karibu na kupasuka.
Matthieu 9.17
20 Nitanena, ili nipate kutulia; Nitafunua midomo yangu na kujibu.
Job 21.3 Job 13.19 Job 20.2 Job 13.13 Proverbes 8.6-8.7
21 Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu; Wala sitajipendekeza kwa mtu ye yote.
Lévitique 19.15 Job 13.8 Job 34.19 Matthieu 22.16 Deutéronome 1.17
22 Kwani mimi sijui kujipendekeza; Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.
Psaumes 12.2-12.3 Proverbes 29.5 Galates 1.10 1 Thessaloniciens 2.5 Job 17.5

Cette Bible est dans le domaine public.