Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 24.4
Bible en Swahili de l’est


1 Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?
Actes 1.7 2 Pierre 3.7-3.8 Ecclésiaste 8.6-8.7 Ecclésiaste 3.17 Esaïe 2.12
2 Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
Deutéronome 19.14 Deutéronome 27.17 Proverbes 23.10 Proverbes 22.28 Job 1.15
3 Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
Deutéronome 24.6 Job 31.16-31.17 1 Samuel 12.3 Deutéronome 24.10-24.13 Job 22.6-22.9
4 Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.
Proverbes 28.28 Job 24.14 Amos 2.7 Esaïe 10.2 Psaumes 41.1
5 Tazama, kama punda-mwitu jangwani Wao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii; Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
Psaumes 104.23 Job 39.5-39.7 Job 24.14 Proverbes 4.16 Sophonie 3.3
6 Hukata nafaka zao mashambani; Na kuokota zabibu za waovu.
Deutéronome 28.33 Juges 6.3-6.6 Deutéronome 28.51 Michée 6.15
7 Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo, Wala hawana cha kujifunika baridi.
Exode 22.26-22.27 Job 22.6 Deutéronome 24.11-24.13 Actes 9.31 Job 31.19-31.20
8 Hutota kwa manyunyo ya milimani, Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
Lamentations 4.5 Hébreux 11.38 Cantique 5.2
9 Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba, Na kutwaa rehani kwa maskini;
Néhémie 5.5 2 Rois 4.1
10 Hata wazunguke uchi pasipo mavazi, Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
Amos 2.7-2.8 Amos 5.11-5.12 Deutéronome 24.19
11 Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao; Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
Jacques 5.4 Jérémie 22.13 Deutéronome 25.4
12 Watu huugua toka mji ulio na watu wengi, Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele; Wala Mungu hauangalii upumbavu.
Ecclésiaste 4.1 Malachie 3.15 Ecclésiaste 8.11-8.12 Esaïe 52.5 Psaumes 69.26
13 Hawa ni katika hao waliouasi mwanga; Hawazijui njia zake, Wala hawakai katika mapito yake.
Jean 3.19-3.20 Jude 1.6 Jacques 4.17 Jean 12.40 Jean 8.44
14 Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji; Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.
1 Thessaloniciens 5.2 Ephésiens 5.7-5.11 2 Samuel 11.14-11.17 Apocalypse 3.3 Psaumes 10.8-10.10
15 Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza, Akisema, Hapana jicho litakaloniona; Naye huuficha uso wake.
Psaumes 10.11 Proverbes 7.9-7.10 Psaumes 50.18 Job 22.13-22.14 Psaumes 73.11
16 Wao hutoboa nyumba gizani; Hujifungia ndani wakati wa mchana; Hawaujui mwanga.
Jean 3.20 Matthieu 24.43 Exode 22.2-22.3 Job 38.12-38.13 Ezéchiel 12.5-12.7
17 Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu; Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.
Job 3.5 Apocalypse 6.16-6.17 2 Corinthiens 5.10-5.11 Psaumes 73.18-73.19 Jérémie 2.26
18 Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika; Sehemu yao inalaaniwa duniani; Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.
Psaumes 69.22 Malachie 2.2 Job 22.16 Psaumes 73.18-73.20 Esaïe 23.10
19 Chaka na hari hukausha maji ya theluji; Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.
Psaumes 49.14 Job 21.13 Psaumes 58.8-58.9 Ecclésiaste 9.4-9.6 Luc 12.20
20 Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.
Daniel 4.14 Proverbes 10.7 Job 18.16-18.17 Esaïe 26.14 Ecclésiaste 8.10
21 Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa; Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
Job 29.13 Job 24.3 Job 31.16-31.18 1 Samuel 1.6-1.7 Job 22.9
22 Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake; Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.
Daniel 6.4-6.9 Esther 3.8-3.10 Apocalypse 16.13-16.14 Apocalypse 17.2 Jean 19.12-19.16
23 Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo; Na macho yake ya juu ya njia zao.
Apocalypse 2.23 Proverbes 15.3 Habakuk 1.13 Psaumes 73.3-73.12 Jérémie 12.1-12.3
24 Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka; Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote, Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.
Psaumes 37.10 Psaumes 92.7 Jacques 5.1-5.3 Psaumes 73.19 Jacques 1.11
25 Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo, Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?
Job 9.24 Job 15.2 Job 6.28 Job 27.4 Job 11.2-11.3

Cette Bible est dans le domaine public.