Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 24.18
Bible en Swahili de l’est


1 Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?
Actes 1.7 Ecclésiaste 8.6-8.7 Ecclésiaste 3.17 2 Pierre 3.7-3.8 Romains 2.5
2 Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
Deutéronome 19.14 Deutéronome 27.17 Proverbes 23.10 Proverbes 22.28 Job 1.15
3 Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
Deutéronome 24.6 Job 31.16-31.17 1 Samuel 12.3 Deutéronome 24.10-24.13 Job 22.6-22.9
4 Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.
Proverbes 28.28 Amos 2.7 Job 24.14 Job 30.25 Job 29.12
5 Tazama, kama punda-mwitu jangwani Wao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii; Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
Psaumes 104.23 Job 39.5-39.7 Proverbes 4.16 Sophonie 3.3 Genèse 27.40
6 Hukata nafaka zao mashambani; Na kuokota zabibu za waovu.
Deutéronome 28.33 Juges 6.3-6.6 Deutéronome 28.51 Michée 6.15
7 Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo, Wala hawana cha kujifunika baridi.
Exode 22.26-22.27 Job 22.6 Deutéronome 24.11-24.13 Actes 9.31 Job 31.19-31.20
8 Hutota kwa manyunyo ya milimani, Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
Lamentations 4.5 Hébreux 11.38 Cantique 5.2
9 Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba, Na kutwaa rehani kwa maskini;
Néhémie 5.5 2 Rois 4.1
10 Hata wazunguke uchi pasipo mavazi, Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
Amos 2.7-2.8 Amos 5.11-5.12 Deutéronome 24.19
11 Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao; Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
Jacques 5.4 Jérémie 22.13 Deutéronome 25.4
12 Watu huugua toka mji ulio na watu wengi, Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele; Wala Mungu hauangalii upumbavu.
Ecclésiaste 4.1 Psaumes 69.26 Exode 1.13-1.14 Juges 10.16 Exode 2.23-2.24
13 Hawa ni katika hao waliouasi mwanga; Hawazijui njia zake, Wala hawakai katika mapito yake.
Jean 3.19-3.20 Jean 8.44 Jean 8.31 1 Jean 2.19 Luc 12.47-12.48
14 Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji; Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.
1 Thessaloniciens 5.2 Ephésiens 5.7-5.11 2 Samuel 11.14-11.17 Apocalypse 3.3 Psaumes 10.8-10.10
15 Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza, Akisema, Hapana jicho litakaloniona; Naye huuficha uso wake.
Psaumes 10.11 Proverbes 7.9-7.10 2 Samuel 11.4-11.13 Exode 20.14 Ezéchiel 8.12
16 Wao hutoboa nyumba gizani; Hujifungia ndani wakati wa mchana; Hawaujui mwanga.
Jean 3.20 Exode 22.2-22.3 Job 38.12-38.13 Ezéchiel 12.5-12.7 Job 24.13
17 Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu; Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.
Job 3.5 Apocalypse 6.16-6.17 2 Corinthiens 5.10-5.11 Psaumes 73.18-73.19 Jérémie 2.26
18 Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika; Sehemu yao inalaaniwa duniani; Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.
Malachie 2.2 Job 22.16 Psaumes 73.18-73.20 Esaïe 23.10 Psaumes 58.7
19 Chaka na hari hukausha maji ya theluji; Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.
Job 21.13 Psaumes 49.14 Luc 12.20 Job 21.23 Job 6.15-6.17
20 Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.
Daniel 4.14 Proverbes 10.7 Job 18.16-18.17 Ecclésiaste 8.10 Job 14.7-14.10
21 Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa; Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
Job 29.13 Job 24.3 Job 31.16-31.18 1 Samuel 1.6-1.7 Job 22.9
22 Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake; Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.
Daniel 6.4-6.9 Esther 3.8-3.10 Apocalypse 16.13-16.14 Apocalypse 17.2 Jean 19.12-19.16
23 Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo; Na macho yake ya juu ya njia zao.
Apocalypse 2.23 Proverbes 15.3 Psaumes 10.13-10.14 Psaumes 11.4-11.5 Ecclésiaste 8.11
24 Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka; Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote, Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.
Psaumes 37.10 Jacques 1.11 Job 20.5 Psaumes 37.35-37.36 Job 8.22
25 Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo, Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?
Job 9.24 Job 15.2 Job 6.28 Job 27.4 Job 11.2-11.3

Cette Bible est dans le domaine public.