Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 21.8
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 7 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Yasikizeni sana maneno yangu; Jambo hili na liwe faraja yenu.
Job 33.31-33.33 Job 18.2 Hébreux 2.1 Esaïe 55.2 Job 13.3-13.4
3 Niacheni, nami pia nitanena; Tena nikiisha nena, zidini kudhihaki.
Job 17.2 Job 16.10 Job 16.20 Job 12.4-12.5 Job 13.9
4 Mimi, je! Mashitaka yangu yamhusu mwanadamu? Nami kwa nini nisikose kusubiri?
Psaumes 42.11 Psaumes 102.1 Matthieu 26.38 Psaumes 77.3-77.9 Job 7.11-7.21
5 Niangalieni, mkastaajabu, Mkaweke mkono kinywani.
Juges 18.19 Job 29.9 Job 40.4 Proverbes 30.32 Psaumes 39.9
6 Hata nikumbukapo nahuzunika, Na utisho wanishika mwilini mwangu.
Psaumes 119.120 Psaumes 88.15 Psaumes 77.3 Habakuk 3.16 Lamentations 3.19-3.20
7 Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?
Job 12.6 Psaumes 73.3-73.12 Jérémie 12.1-12.3 Psaumes 37.35 Habakuk 1.13
8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.
Job 5.3-5.4 Job 20.10 Job 20.28 Job 18.19 Proverbes 17.6
9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.
Psaumes 73.5 Job 9.34 Esaïe 57.19-57.21 Job 15.21 Job 18.11
10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.
Exode 23.26 Psaumes 144.13-144.14 Deutéronome 28.11 Luc 16.19 Ecclésiaste 9.1-9.2
11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.
Psaumes 127.3-127.5 Psaumes 107.41
12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.
Amos 6.4-6.6 Esaïe 5.12 Genèse 4.21 Genèse 31.27 Esaïe 22.13
13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
Job 36.11 Luc 12.19-12.20 Matthieu 24.38-24.39 Psaumes 73.4 Luc 17.28-17.29
14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
Job 22.17 Proverbes 1.29 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Luc 8.28 Psaumes 10.11
15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
Exode 5.2 Job 34.9 Malachie 1.13-1.14 Job 35.3 Matthieu 7.7
16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
Job 22.18 Psaumes 1.1 Luc 16.2 Psaumes 49.6-49.7 Psaumes 52.5-52.7
17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?
Job 18.5-18.6 Job 18.18 Proverbes 20.20 Psaumes 90.7-90.9 Matthieu 25.8
18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?
Psaumes 1.4 Job 13.25 Psaumes 83.13 Psaumes 35.5 Esaïe 17.13
19 Mwasema, Mungu huwawekea watoto wa mtu huo uovu wake. Na amlipe mwenyewe, ili apate kuujua.
Exode 20.5 Jérémie 31.29 Deutéronome 32.41 Esaïe 14.21 Ezéchiel 18.14
20 Macho yake mwenyewe na yaone uharibifu wake, Akanywe ghadhabu zake Mwenyezi.
Esaïe 51.17 Apocalypse 14.10 Psaumes 75.8 Jérémie 51.7 Jérémie 25.15-25.16
21 Kwani ana furaha gani katika mbari yake baada yake, Hesabu ya miezi yake itakapokwisha katwa katikati?
Job 14.5 Job 14.21 Luc 16.27-16.28 Ecclésiaste 2.18-2.19 Psaumes 55.23
22 Je! Mtu awaye yote atamfundisha Mungu maarifa? Naye ndiye awahukumuye walioko juu.
Romains 11.34 Esaïe 40.13-40.14 1 Corinthiens 2.16 Ecclésiaste 5.8 Job 40.2
23 Mmoja hufa katika nguvu zake kamili, Mwenye kukaa salama na kustarehe;
Job 20.22-20.23 Psaumes 73.4-73.5 Luc 12.19-12.21 Psaumes 49.17
24 Vyombo vyake vimejaa maziwa, Na mafuta ya mifupani mwake ni laini.
Proverbes 3.8 Job 15.27 Psaumes 17.10
25 Mwingine hufa katika uchungu wa roho, Asionje mema kamwe.
Job 7.11 Proverbes 14.10 Ezéchiel 4.16-4.17 Job 3.20 Job 10.1
26 Wao hulala mavumbini sawasawa, Mabuu huwafunika.
Esaïe 14.11 Ecclésiaste 9.2 Job 20.11 Job 3.18-3.19 Job 24.20
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.
Psaumes 119.86 1 Pierre 2.19 Job 32.3 Luc 5.22 Job 5.3-5.5
28 Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi? Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?
Job 20.7 Job 8.22 Job 31.37 Zacharie 5.4 Psaumes 52.5-52.6
29 Je! Hamkuwauliza wapitao njiani? Na maonyo yao hamyajui?
Psaumes 129.8
30 Kwamba mwovu huachiliwa katika siku ya msiba? Na kuongozwa nje katika siku ya ghadhabu?
Proverbes 16.4 Job 20.28 Psaumes 110.5 Nahum 1.2 Sophonie 1.15
31 Ni nani atakayetangaza njia yake usoni pake? Tena ni nani atakayemlipa kwa hayo aliyofanya?
Deutéronome 7.10 Galates 2.11 1 Rois 21.19-21.24 Job 41.11 Actes 24.25
32 Pamoja na hayo atachukuliwa kaburini, Nao watalinda zamu juu ya ziara lake.
Luc 16.22 Ezéchiel 32.21-32.32 Psaumes 49.14
33 Udongo wa bondeni utakuwa tamu kwake, Na watu wote watafuata nyuma yake, Kama vile walivyomtangulia watu wasiohesabika.
Hébreux 9.27 Job 30.23 Ecclésiaste 1.4 Ecclésiaste 8.8 Ecclésiaste 12.7
34 Basi imekuwaje ninyi kunituza moyo bure, Kwa kuwa katika jawabu zenu unasalia uongo tu.
Job 16.2 Job 42.7 Job 13.4 Job 32.3

Cette Bible est dans le domaine public.