Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 21.27
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 7 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Yasikizeni sana maneno yangu; Jambo hili na liwe faraja yenu.
Job 15.11 Job 33.1 Job 34.2 Job 33.31-33.33 Job 18.2
3 Niacheni, nami pia nitanena; Tena nikiisha nena, zidini kudhihaki.
Job 16.10 Job 17.2 Job 16.20 Job 13.13 Job 12.4-12.5
4 Mimi, je! Mashitaka yangu yamhusu mwanadamu? Nami kwa nini nisikose kusubiri?
2 Rois 6.26-6.27 Psaumes 142.2-142.3 1 Samuel 1.16 Psaumes 42.11 Psaumes 102.1
5 Niangalieni, mkastaajabu, Mkaweke mkono kinywani.
Job 40.4 Juges 18.19 Job 29.9 Proverbes 30.32 Romains 11.33
6 Hata nikumbukapo nahuzunika, Na utisho wanishika mwilini mwangu.
Psaumes 77.3 Habakuk 3.16 Lamentations 3.19-3.20 Psaumes 119.120 Psaumes 88.15
7 Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?
Job 12.6 Habakuk 1.13 Psaumes 73.3-73.12 Jérémie 12.1-12.3 Psaumes 37.35
8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.
Job 18.19 Proverbes 17.6 Psaumes 17.14 Job 5.3-5.4 Job 20.10
9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.
Job 9.34 Psaumes 73.5 Job 18.11 Psaumes 73.19 Esaïe 57.19-57.21
10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.
Exode 23.26 Luc 12.16-12.21 Deutéronome 7.13-7.14 Psaumes 144.13-144.14 Deutéronome 28.11
11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.
Psaumes 127.3-127.5 Psaumes 107.41
12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.
Esaïe 5.12 Genèse 4.21 Amos 6.4-6.6 Esaïe 22.13 Genèse 31.27
13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
Job 36.11 Psaumes 73.4 Luc 17.28-17.29 Luc 12.19-12.20 Matthieu 24.38-24.39
14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
Job 22.17 Proverbes 1.29 Jean 3.19-3.20 Jean 8.45-8.47 Romains 1.28
15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
Exode 5.2 Job 34.9 Malachie 1.13-1.14 Osée 13.6 Psaumes 12.4
16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
Job 22.18 Psaumes 1.1 Luc 16.25 Job 12.9-12.10 Luc 16.2
17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?
Job 18.5-18.6 Proverbes 24.20 Proverbes 13.9 Job 18.18 Proverbes 20.20
18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?
Psaumes 1.4 Psaumes 35.5 Job 13.25 Psaumes 83.13 Esaïe 17.13
19 Mwasema, Mungu huwawekea watoto wa mtu huo uovu wake. Na amlipe mwenyewe, ili apate kuujua.
Exode 20.5 Jérémie 31.29 Job 22.24 2 Corinthiens 5.21 Esaïe 53.4-53.6
20 Macho yake mwenyewe na yaone uharibifu wake, Akanywe ghadhabu zake Mwenyezi.
Esaïe 51.17 Apocalypse 14.10 Psaumes 75.8 Psaumes 60.3 Luc 16.23
21 Kwani ana furaha gani katika mbari yake baada yake, Hesabu ya miezi yake itakapokwisha katwa katikati?
Job 14.5 Psaumes 55.23 Psaumes 102.24 Job 14.21 Luc 16.27-16.28
22 Je! Mtu awaye yote atamfundisha Mungu maarifa? Naye ndiye awahukumuye walioko juu.
Romains 11.34 1 Corinthiens 2.16 Esaïe 40.13-40.14 Jude 1.6 Esaïe 45.9
23 Mmoja hufa katika nguvu zake kamili, Mwenye kukaa salama na kustarehe;
Psaumes 73.4-73.5 Luc 12.19-12.21 Psaumes 49.17 Job 20.22-20.23
24 Vyombo vyake vimejaa maziwa, Na mafuta ya mifupani mwake ni laini.
Proverbes 3.8 Job 15.27 Psaumes 17.10
25 Mwingine hufa katika uchungu wa roho, Asionje mema kamwe.
Job 7.11 Job 20.23 Ecclésiaste 6.2 Proverbes 14.10 Ezéchiel 4.16-4.17
26 Wao hulala mavumbini sawasawa, Mabuu huwafunika.
Ecclésiaste 9.2 Esaïe 14.11 Job 20.11 Job 3.18-3.19 Job 19.26
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.
Job 20.5 Job 15.20-15.35 Job 4.8-4.11 Psaumes 119.86 1 Pierre 2.19
28 Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi? Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?
Job 8.22 Job 20.7 Job 1.3 Psaumes 37.36 Job 31.37
29 Je! Hamkuwauliza wapitao njiani? Na maonyo yao hamyajui?
Psaumes 129.8
30 Kwamba mwovu huachiliwa katika siku ya msiba? Na kuongozwa nje katika siku ya ghadhabu?
Proverbes 16.4 Job 20.28 Apocalypse 6.17 Romains 2.5 2 Pierre 3.7
31 Ni nani atakayetangaza njia yake usoni pake? Tena ni nani atakayemlipa kwa hayo aliyofanya?
Deutéronome 7.10 Galates 2.11 Esaïe 59.13 Psaumes 50.21 2 Samuel 12.7-12.12
32 Pamoja na hayo atachukuliwa kaburini, Nao watalinda zamu juu ya ziara lake.
Luc 16.22 Ezéchiel 32.21-32.32 Psaumes 49.14
33 Udongo wa bondeni utakuwa tamu kwake, Na watu wote watafuata nyuma yake, Kama vile walivyomtangulia watu wasiohesabika.
Job 30.23 Hébreux 9.27 Genèse 3.19 Job 24.24 Ecclésiaste 1.4
34 Basi imekuwaje ninyi kunituza moyo bure, Kwa kuwa katika jawabu zenu unasalia uongo tu.
Job 16.2 Job 13.4 Job 32.3 Job 42.7

Cette Bible est dans le domaine public.