Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 31.13
Bible en Swahili de l’est


Fonctions des prêtres et des Lévites

1 Basi hayo yote yalipokwisha, wakatoka Israeli wote waliokuwako waende miji ya Yuda, wakazivunja-vunja nguzo, wakayakata-kata maashera, wakabomoa mahali pa juu na madhabahu katika Yuda yote na Benyamini, katika Efraimu pia na Manase, hata walipokwisha kuviharibu vyote. Ndipo wana wa Israeli wote wakarudi, kila mtu kwa milki yake, mijini kwao.
2 Rois 18.4 2 Chroniques 32.12 2 Chroniques 23.17 2 Rois 23.2-23.20 2 Chroniques 30.1-30.27
2 Hezekia akaziweka zamu za makuhani na Walawi kwa zamu zao, kila mtu kwa kadiri ya huduma yake, makuhani na Walawi pia, kwa sadaka za kuteketezwa na kwa sadaka za amani, kutumika, na kushukuru, na kusifu, malangoni mwa matuo ya Bwana.
1 Chroniques 24.1 Luc 1.5 2 Chroniques 29.24-29.26 1 Chroniques 16.4-16.6 Jérémie 33.11
3 Tena akaweka sehemu ya mfalme ya mali zake kwa sadaka za kuteketezwa, yaani, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na sadaka za kuteketezwa za sabato, na za mwezi mpya, na sikukuu, kama ilivyoandikwa katika torati ya Bwana.
Ezéchiel 45.17 2 Chroniques 35.7 Lévitique 23.2-23.44 Nombres 28.1-29.40 Psaumes 81.1-81.4
4 Tena akawaamuru watu waliokaa Yerusalemu, watoe sehemu ya makuhani na Walawi, ili hao wajibidiishe katika torati ya Bwana.
Malachie 2.7 Nombres 18.8-18.21 Galates 6.6 Néhémie 13.10-13.13 Lévitique 27.30-27.33
5 Mara ilipotangaa amri, wana wa Israeli wakatoa kwa wingi malimbuko ya nafaka, na divai, na mafuta, na asali, na mazao yote ya mashamba; na zaka za vitu vyote wakazileta nyingi.
Néhémie 13.12 Nombres 18.12 Exode 36.5-36.6 Jacques 1.18 1 Corinthiens 15.20
6 Nao wana wa Israeli na Yuda, waliokaa mijini mwa Yuda, wakaleta pia zaka za ng’ombe na kondoo, na zaka za vitu vilivyowekwa wakfu, alivyowekewa Bwana, Mungu wao, wakaviweka chungu chungu.
Lévitique 27.30 Deutéronome 14.28 2 Chroniques 11.16-11.17
7 Katika mwezi wa tatu wakaanza kuweka misingi ya hizo chungu, wakazimaliza katika mwezi wa saba.
Lévitique 23.16-23.24
8 Hata walipokuja Hezekia na wakuu, na kuziona zile chungu, wakamhimidi Bwana, na watu wake Israeli.
Genèse 14.19-14.20 Psaumes 144.15 Ephésiens 1.3 Philippiens 4.10 1 Chroniques 29.10-29.20
9 Ndipo Hezekia akaulizana na makuhani na Walawi katika habari ya hizo chungu.
10 Azaria kuhani mkuu, wa nyumba ya Sadoki, akamjibu, akasema, Tangu watu walipoanza kuleta matoleo nyumbani kwa Bwana, tumekula na kushiba, na kusaza tele; kwa kuwa Bwana amewabariki watu wake; na kilichosalia ndiyo akiba hii kubwa.
Malachie 3.10 1 Chroniques 6.8 Proverbes 10.22 Genèse 39.5 Genèse 30.27-30.30
11 Ndipo Hezekia akaamuru kutengeneza vyumba nyumbani mwa Bwana; wakavitengeneza.
Néhémie 10.38-10.39 Néhémie 13.12-13.13 Néhémie 13.5
12 Wakayaingiza matoleo na zaka na vitu vilivyowekwa wakfu, kwa uaminifu; na juu yake Konania Mlawi alikuwa mkuu, na wa pili ni Shimei nduguye.
2 Chroniques 35.9 2 Rois 12.15 1 Chroniques 26.20-26.26
13 Na Yehieli, na Azaria, na Nahathi, na Asaheli, na Yerimothi, na Yozabadi, na Elieli, na Ismakia, na Mahathi, na Benaya, walikuwa wasimamizi chini ya mkono wa Konania na Shimei nduguye, kwa amri ya Hezekia mfalme, na Azaria mkuu wa nyumba ya Mungu.
2 Chroniques 31.4 2 Chroniques 31.10-31.11 1 Chroniques 24.5 Néhémie 11.11 2 Chroniques 30.12
14 Na Kore, mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa mlango wa mashariki, alizisimamia sadaka za hiari za Mungu; ili kugawa matoleo ya Bwana, navyo vitu vilivyokuwa vitakatifu sana.
Lévitique 6.16-6.17 Esdras 3.5 Lévitique 10.12-10.13 1 Chroniques 26.17 Lévitique 23.38
15 Na chini yake walikuwa Edeni, na Minyamini, na Yeshua, na Shemaya, na Amaria, na Shekania, mijini mwa makuhani, kwa walivyoaminiwa, ili kuwagawia ndugu zao kwa zamu, wakuu na wadogo sawasawa;
Josué 21.9-21.19 1 Chroniques 25.8 1 Chroniques 9.22 2 Chroniques 29.12 2 Chroniques 31.13
16 zaidi ya wale waliohesabiwa kwa nasaba ya wanaume, wenye miaka mitatu na zaidi, kila mmoja aliyeingia nyumbani mwa Bwana, kama ilivyopasa kazi ya kila siku, kwa huduma zao katika malinzi yao, kwa kadiri ya zamu zao;
Esdras 3.4 1 Chroniques 23.3 Lévitique 21.22-21.23
17 na wale waliohesabiwa kwa nasaba ya makuhani kufuata nyumba za baba zao, na Walawi, wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, katika malinzi yao, kwa kadiri ya zamu zao;
1 Chroniques 23.24 1 Chroniques 23.27 Nombres 3.15 Nombres 4.3 1 Chroniques 24.20-25.26
18 na wale waliohesabiwa kwa nasaba ya wadogo wao wote, wake zao, na wana wao, na binti zao, katika kusanyiko lote; kwani kwa vile walivyoaminiwa, wakajitakasa katika utakatifu;
1 Chroniques 9.22 Romains 15.16 2 Chroniques 31.15 Esaïe 5.16
19 tena kwa ajili ya wana wa Haruni makuhani, waliokuwamo mashambani mwa malisho ya miji yao, mji kwa mji, kulikuwa na watu waliotajwa majina yao, ili kuwagawia sehemu wanaume wote miongoni mwa makuhani, na wote waliohesabiwa kwa nasaba miongoni mwa Walawi.
2 Chroniques 31.12-31.15 Nombres 35.2-35.5 Lévitique 25.34 2 Chroniques 28.15 1 Chroniques 6.60
20 Na hivyo ndivyo alivyofanya Hezekia katika Yuda yote; akatenda yaliyo mema, na ya adili, na uaminifu, mbele za Bwana, Mungu wake.
2 Rois 20.3 2 Rois 22.2 Actes 24.16 1 Thessaloniciens 2.10 3 Jean 1.5
21 Na katika kila kazi aliyoanza kwa utumishi wa nyumba ya Mungu, na kwa torati, na kwa amri, ili kumtafuta Mungu wake, aliifanya kwa moyo wake wote, akafanikiwa.
Deutéronome 29.9 Deutéronome 10.12 Jérémie 29.13 Psaumes 1.2-1.3 1 Chroniques 22.13

Cette Bible est dans le domaine public.