Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 20.22
Bible en Swahili de l’est


Victoires de Josaphat

1 Ikawa baadaye, wana wa Moabu, na wana wa Amoni, na pamoja nao baadhi ya Wameuni, wakaja juu ya Yehoshafati vitani.
2 Chroniques 19.11 Esaïe 8.9-8.10 Jérémie 10.24 Esaïe 16.6 Apocalypse 3.19
2 Wakaja watu waliomwambia Yehoshafati, wakisema, Wanakuja jamii kubwa juu yako watokao Shamu toka ng’ambo ya bahari; na tazama, wako katika Hasason-tamari (ndio En-gedi).
Genèse 14.7 1 Samuel 23.29 Josué 3.16 Cantique 1.14 Genèse 14.3
3 Yehoshafati akaogopa, akauelekeza uso wake amtafute Bwana; akatangaza mbiu ya watu kufunga katika Yuda yote.
2 Chroniques 19.3 Jérémie 36.9 1 Samuel 7.6 Joël 1.14 Jonas 3.5-3.9
4 Yuda wakakusanyika pamoja ili wamtafute Bwana; hata kutoka miji yote ya Yuda wakaja kumtafuta Bwana.
Psaumes 50.15 Psaumes 34.5-34.6 2 Chroniques 19.5 Psaumes 69.35 Psaumes 60.10-60.12
5 Yehoshafati akasimama kati ya kusanyiko la Yuda na Yerusalemu, nyumbani mwa Bwana, mbele ya ua mpya;
2 Chroniques 34.31 2 Rois 19.15-19.19 2 Chroniques 6.12-6.13
6 akasema, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe uliye Mungu mbinguni? Tena si wewe utawalaye falme zote za mataifa? Na mkononi mwako mna uweza na nguvu, asiweze mtu ye yote kusimama kinyume chako.
1 Chroniques 29.11-29.12 Deutéronome 4.39 Daniel 4.25 Daniel 4.17 Matthieu 6.9
7 Si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Ibrahimu rafiki yako hata milele?
Esaïe 41.8 Jacques 2.23 Psaumes 44.2 Genèse 13.15 Exode 6.7
8 Nao walikaa humo, wamekujengea patakatifu pa jina lako humo, wakisema,
2 Chroniques 6.10 2 Chroniques 2.4
9 Yakitujia mabaya, upanga, hukumu, au tauni, au njaa, tutasimama mbele ya nyumba hii, na mbele zako, (maana jina lako limo katika nyumba hii), na kukulilia katika shida yetu, nawe utasikia na kuokoa.
2 Chroniques 6.20 2 Chroniques 6.28-6.30 1 Rois 8.33 1 Rois 8.37 Exode 20.24
10 Na sasa, tazama, wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, ambao hukuwaacha Israeli waingie katika nchi yao, walipotoka nchi ya Misri; lakini wakawageukia mbali, wasiwaharibu;
Nombres 20.17-20.21 Deutéronome 2.9 Deutéronome 2.4-2.5 Deutéronome 2.19 Juges 11.15-11.18
11 tazama, jinsi wanavyotulipa, wakija kututupa toka milki yako, uliyoturithisha.
Psaumes 83.3-83.12 Proverbes 17.13 Juges 11.23-11.24 Psaumes 35.12 Jérémie 18.20
12 Ee Mungu wetu, je! Hutawahukumu? Maana sisi hatuna uwezo juu ya jamii kubwa hii, wanaotujia juu yetu; wala hatujui tufanyeje; lakini macho yetu yatazama kwako.
Psaumes 25.15 Psaumes 121.1-121.2 Psaumes 123.1-123.2 Juges 11.27 1 Samuel 3.13
13 Wakasimama Yuda wote mbele za Bwana, pamoja na wadogo wao, na wake zao, na watoto wao.
Actes 21.5 Esdras 10.1 Jonas 3.5 Deutéronome 29.10
14 Ndipo Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu, akajiliwa na roho ya Bwana, katikati ya kusanyiko;
2 Chroniques 15.1 2 Chroniques 24.20 Nombres 11.25-11.26 Esaïe 65.24 Actes 10.4
15 akasema, Sikieni, Yuda wote, nanyi mkaao Yerusalemu, na wewe mfalme Yehoshafati; Bwana awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani vita si yenu bali ni ya Mungu.
2 Chroniques 32.7-32.8 1 Samuel 17.47 Deutéronome 20.1 Deutéronome 1.29-1.30 Esaïe 43.1-43.2
16 Kesho shukeni juu yao; tazameni, wanakwea kwa kupandia Sisi; nanyi mtawapata penye mwisho wa bonde, mbele ya jangwa la Yerueli.
17 Hamtahitaji kupigana vita, jipangeni, simameni, mkauone wokovu wa Bwana ulio pamoja nanyi, enyi Yuda na Yerusalemu; msiogope, wala msifadhaike; kesho tokeni juu yao; kwa kuwa Bwana yu pamoja nanyi.
Exode 14.13-14.14 2 Chroniques 15.2 Matthieu 28.20 Esaïe 41.10 Nombres 14.9
18 Yehoshafati akainama kichwa, kifulifuli; wakaanguka mbele za Bwana Yuda wote na wakaao Yerusalemu, wakimsujudia Bwana.
Exode 4.31 2 Chroniques 7.3 Psaumes 95.6 Job 1.20 Genèse 24.26
19 Na Walawi, wa wana wa Wakohathi na wa wana wa Wakorahi, wakasimama ili wamsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
1 Chroniques 15.16-15.22 Néhémie 12.42-12.43 Psaumes 49.1 Esdras 3.12-3.13 1 Chroniques 25.1-25.7
20 Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwaminini Bwana, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa.
Jean 11.40 Esaïe 7.9 Hébreux 11.6 Romains 8.31 Jean 5.46-5.47
21 Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia Bwana, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu, wakitoka mbele ya jeshi, na kusema, Mshukuruni Bwana; kwa maana fadhili zake ni za milele.
1 Chroniques 16.34 2 Chroniques 5.13 Psaumes 107.1 Psaumes 29.2 1 Chroniques 16.29
22 Nao walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.
Juges 7.22 2 Chroniques 13.13 Esaïe 19.2 2 Chroniques 20.10 2 Rois 6.17
23 Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.
1 Samuel 14.20 Juges 7.22 Ezéchiel 35.2-35.3 Josué 24.4 Deutéronome 2.5
24 Hata Yuda walipofika mnara wa kulindia wa jangwani, wakalitazama hilo jeshi; nao, angalia, walikuwa maiti walioanguka nchi, wala hapana aliyeokoka.
Exode 14.30 Jérémie 33.5 1 Chroniques 5.22 Psaumes 110.6 Esaïe 37.36
25 Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana.
Psaumes 68.12 2 Rois 7.9-7.16 Nombres 31.15 Proverbes 3.15 1 Samuel 30.19-30.20
26 Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia Bwana; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.
Luc 1.68 Psaumes 107.21-107.22 Esaïe 62.4 2 Chroniques 5.9 Psaumes 103.1-103.2
27 Kisha wakarudi, kila mtu wa Yuda na Yerusalemu, na Yehoshafati mbele yao, ili kuurudia Yerusalemu kwa furaha; kwa kuwa Bwana amewafurahisha juu ya adui zao.
Néhémie 12.43 2 Samuel 6.14-6.15 Hébreux 6.20 Michée 2.13 Psaumes 30.1
28 Wakafika Yerusalemu wenye vinanda vinubi na mapanda kwenda nyumbani kwa Bwana.
Psaumes 150.3-150.5 Apocalypse 14.2-14.3 Psaumes 92.3 2 Samuel 6.5 Psaumes 57.8
29 Ikawa hofu ya Mungu juu ya falme zote za nchi, waliposikia ya kuwa Bwana amepigana juu ya adui za Israeli.
2 Chroniques 17.10 2 Chroniques 14.14 Genèse 35.5 2 Rois 7.6 Josué 5.1
30 Basi ukatulia ufalme wake Yehoshafati; kwa sababu Mungu wake alimstarehesha pande zote.
2 Chroniques 14.6-14.7 2 Chroniques 15.15 Job 34.29 Jean 14.27 Proverbes 16.7

Résumé du règne de Josaphat

31 Yehoshafati akatawala juu ya Yuda; alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Azuba binti Shilhi.
1 Rois 22.41-22.44
32 Akaiendea njia ya Asa babaye, wala hakuiacha, akifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
Psaumes 36.3 2 Chroniques 17.3-17.6 1 Rois 15.11 2 Chroniques 14.11-14.13 2 Chroniques 16.7-16.12
33 Lakini mahali pa juu hapakuondolewa; wala mioyo ya watu bado haijakazwa kwa Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 17.6 2 Chroniques 19.3 2 Chroniques 12.14 Deutéronome 29.4 2 Chroniques 14.3
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
1 Rois 16.1 2 Chroniques 19.2 1 Rois 16.7 2 Chroniques 13.22 2 Chroniques 16.11
35 Baada ya hayo Yehoshafati mfalme wa Yuda akapatana na Ahazia mfalme wa Israeli; naye huyo ndiye aliyefanya mabaya mno;
1 Rois 22.48-22.49 2 Rois 1.2-1.16
36 akapatana naye kufanya merikebu za kuendea Tarshishi; wakazifanya merikebu zile huko Esion-geberi.
1 Rois 9.26 1 Rois 10.22 2 Chroniques 9.21
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii juu ya Yehoshafati, akasema, Kwa sababu umepatana na Ahazia, Bwana amezivunja-vunja kazi zako. Zikavunjika merikebu, zisiweze kufika Tarshishi.
Proverbes 13.20 2 Chroniques 9.21 2 Chroniques 19.2 Josué 7.11-7.12 1 Rois 22.48

Cette Bible est dans le domaine public.