Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 4.6
Bible en Swahili de l’est


Autres descendants de Juda

1 Wana wa Yuda; Peresi, na Hesroni, na Karmi, na Huri, na Shobali.
Genèse 46.12 Genèse 38.29 1 Chroniques 2.3 1 Chroniques 2.9 Ruth 4.18
2 Na Reaya, mwana wa Shobali, akamzaa Yahathi; na Yahathi akawazaa Ahumai, na Lahadi. Hizo ndizo jamaa za Wasorathi.
Josué 15.33 Juges 13.25 1 Chroniques 2.52-2.54
3 Na hawa ndio wana wa babaye Etamu; Yezreeli, na Ishma, na Idbashi; na umbu lao aliitwa jina lake Haselelponi;
2 Chroniques 11.6 Juges 15.11
4 na Penueli, babaye Gedori, na Ezeri, babaye Husha. Hao ndio wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi, babaye Bethlehemu.
1 Chroniques 2.50 1 Chroniques 4.18 1 Chroniques 4.39 1 Chroniques 2.19 Josué 15.36
5 Naye Ashuri, babaye Tekoa, alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.
1 Chroniques 2.24
6 Naye Naara akamzalia Ahuzamu, na Heferi, na Temeni, na Ahashtari. Hao ndio wana wa Naara.
7 Na wana wa Hela walikuwa Serethi, na Ishari, na Ethnani.
8 Na Hakosi akawazaa Anubu, na Sobeba, na jamaa za Aharheli, mwana wa Harumu.
9 Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze; na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa huzuni.
Genèse 34.19 Genèse 3.16 Esaïe 43.4 Genèse 35.18 1 Chroniques 7.23
10 Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.
Matthieu 7.7-7.11 Psaumes 116.1-116.4 Jean 10.28 2 Timothée 4.18 Psaumes 119.173
11 Naye Kelubu, nduguye Shuha, akamzaa Mehiri, aliyekuwa babaye Eshtoni.
12 Na Eshtoni akamzaa Beth-Rafa, na Pasea, na Tehina, babaye Ir-nahashi. Hao ni watu wa Reka.
13 Na wana wa Kenazi; Othnieli, na Seraya; na wana wa Othnieli; Hathathi.
Josué 15.17 Juges 1.13 Juges 3.9-3.11
14 Na Meonothai akamzaa Ofra; na Seraya akamzaa Yoabu, babaye bonde la Wakarashi; kwani hao walikuwa mafundi.
2 Rois 24.14 Néhémie 11.35
15 Na wana wa Kalebu, mwana wa Yefune; Iru, na Ela, na Naamu; na wana wa Ela; na Kenazi.
Nombres 13.6 Nombres 14.6-14.10 Juges 1.12-1.14 Nombres 14.30 Josué 14.6-14.14
16 Na wana wa Yehaleleli; Zifu, na Zifa, na Tiria, na Asareli.
17 Na wana wa Ezrahi; Yetheri, na Meredi, na Eferi, na Yaloni; na Miriamu akamzalia na Shamai, na Ishba, babaye Eshtemoa.
Josué 15.50 1 Chroniques 21.24 1 Chroniques 6.57 1 Chroniques 4.19 1 Samuel 30.28
18 Na mkewe Myahudi akawazaa Yeredi, babaye Gedori, na Heberi, babaye Soko, na Yekuthieli, babaye Zanoa. Na hawa ndio wana wa Bithia, binti Farao, ambaye Meredi alimwoa.
1 Chroniques 4.4 Josué 15.58 1 Chroniques 4.39 1 Chroniques 2.42 Josué 15.48
19 Na wana wa mkewe Hodia, umbu lake Nahamu, walikuwa babaye Keila, Mgarmi, na Eshtemoa, Mmaaka.
Josué 15.44 1 Samuel 23.1-23.13
20 Na wana wa Shimoni; Amnoni, na Rina, na Ben-hanani, na Tiloni. Na wana wa Ishi; Zohethi, na Ben-zohethi.
21 Wana wa Shela, mwana wa Yuda; Eri, babaye Leka, na Laada, babaye Maresha, na jamaa zao wa mbari ya wafuma nguo za kitani safi, wa mbari ya Ashbea;
Genèse 38.5 Genèse 46.12 1 Chroniques 2.3 Nombres 26.20 1 Chroniques 9.5
22 na Yokimu, na watu wa Kozeba, na Yoashi, na Sarafi waliokuwa na mamlaka katika Moabu, na Yashubi-lehemu. Na taarifa hizi ni za zamani sana.
23 Hao ndio waliokuwa wafinyanzi, na wenyeji wa Netaimu na Gedera; ndipo walipokaa pamoja na mfalme ili kufanya kazi yake.
1 Chroniques 4.14 Psaumes 81.6

Descendance de Siméon

24 Wana wa Simeoni; Yemueli, na Yamini, na Yakini, na Sohari, na Shauli;
Genèse 46.10 Exode 6.15 Nombres 26.12-26.14
25 na mwanawe huyo ni Shalumu, na mwanawe huyo ni Mibsamu, na mwanawe huyo ni Mishma.
26 Na wana wa Mishma; mwanawe huyo ni Hamueli, na mwanawe huyo ni Zakuri, na mwanawe huyo ni Shimei.
27 Naye Shimei alikuwa na wana wa kiume kumi na sita, na wana wa kike sita; walakini nduguze walikuwa hawana watoto wengi, tena jamaa yao yote haikuongezeka sana kwa mfano wa wana wa Yuda.
Nombres 2.4 Nombres 2.13 Nombres 26.22 Nombres 26.14
28 Nao wakakaa huko Beer-sheba, na Molada, na Hasar-shuali;
Josué 19.2-19.3 Josué 19.9 Josué 15.28-15.29
29 na huko Bilha, na Esemu, na Toladi;
Josué 19.3-19.4
30 na huko Bethueli, na Horma, na Siklagi;
Josué 15.31 1 Chroniques 12.1 1 Samuel 27.6 Néhémie 11.28 Josué 19.4-19.5
31 na huko, Beth-markabothi, na Hasar-susimu, na Bethbiri, na Shaaraimu. Hiyo ndiyo miji yao hata wakati wa kumiliki Daudi.
Josué 19.5-19.6
32 Na vijiji vyao vilikuwa Etamu, na Aini, na Rimoni, na Tokeni, na Ashani, miji mitano,
Josué 19.7
33 na vijiji vyao vyote vilivyoizunguka miji iyo hiyo, mpaka Baali. Hayo ndiyo makao yao, na hati ya nasaba yao wanayo.
Josué 19.8
34 Naye Meshobabu, na Yamleki, na Yosha, mwana wa Amazia;
35 na Yoeli, na Yehu, mwana wa Yoshibia, mwana wa Seraya, mwana wa Asieli;
36 na Elioenai, na Yaakoba, na Yeshohava, na Asaya, na Adieli, na Yesimieli, na Benaya;
37 na Ziza, mwana wa Shifi, mwana wa Aloni, mwana wa Yedaya mwana wa Shimri, mwana wa Shemaya;
38 hao waliotajwa majina yao ndio waliokuwa wakuu katika jamaa zao; na mbari za baba zao zikaongezeka sana.
Genèse 6.4 1 Chroniques 5.24
39 Basi wakaenda mpaka maingilio ya Gedori, naam, mpaka upande wa mashariki wa bonde hilo, ili kuwatafutia kondoo zao malisho.
1 Chroniques 4.18 Josué 15.58 1 Chroniques 4.4 Josué 12.13
40 Wakaona malisho ya unono, mazuri, na nchi yenyewe ilikuwa na nafasi, tena imetulia, na kuwa na amani; kwani waliokaa huko zamani walikuwa watu wa Hamu.
Juges 18.7-18.10 Genèse 10.6 Genèse 9.22-9.29 Psaumes 78.51 Psaumes 105.23
41 Na hao walioandikwa majina yao waliingia huko katika siku za Hezekia, mfalme wa Yuda, na kuzipiga hema zao, pamoja na hao Wameuni walioonekana huko, wakawaangamiza kabisa, hata siku hii ya leo, nao wakakaa huko badala yao; kwa sababu huko kulikuwa na malisho kwa kondoo zao.
Esaïe 14.28-14.32 Juges 10.12 Nombres 32.1-32.4 2 Rois 18.8-18.12 Actes 17.26
42 Na baadhi yao, maana ya hao wana wa Simeoni, watu mia tano, wakaenda mpaka mlima Seiri, na majemadari wao walikuwa Pelatia, na Nearia, na Refaya, na Uzieli, wana wa Ishi.
Genèse 36.8-36.9 Deutéronome 1.2
43 Nao wakawapiga mabaki ya Waamaleki waliookoka, wakakaa huko, hata siku hii ya leo.
1 Samuel 30.17 2 Samuel 8.12 1 Samuel 15.7-15.8 Deutéronome 34.6 Matthieu 27.8

Cette Bible est dans le domaine public.