Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 14.4
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Amatsia sur Juda

1 Katika mwaka wa pili wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Rois 13.10 2 Chroniques 25.1-25.4 1 Chroniques 3.12 2 Rois 14.15
2 Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Yehoadani wa Yerusalemu.
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi.
2 Chroniques 24.17 1 Rois 15.3 2 Rois 12.2 2 Chroniques 25.14-25.16 2 Chroniques 25.2-25.3
4 Walakini mahali pa juu hapakuondolewa; watu wakaendelea kutoa dhabihu na kufukiza uvumba katika mahali pa juu.
2 Rois 12.3 2 Rois 16.4 2 Rois 15.4 2 Rois 15.35
5 Ikawa, mara ufalme ulipokuwa imara mkononi mwake, aliwaua watumishi wale waliomwua mfalme baba yake;
Genèse 9.6 Exode 21.12-21.14 Nombres 35.33 2 Rois 12.20-12.21 2 Chroniques 25.3-25.4
6 ila hakuwaua watoto wa hao wauaji; kama ilivyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, kama alivyoamuru Bwana, akisema, Mababa wasife kwa makosa ya wana, wala wana wasife kwa makosa ya mababa; lakini kila mtu atakufa kwa kosa lake mwenyewe.
Ezéchiel 18.4 Ezéchiel 18.20 Deutéronome 24.16 Jérémie 31.30
7 Akawaua Waedomi katika Bonde la Chumvi watu elfu kumi; akautwaa Sela vitani, akauita jina lake Yoktheeli hata leo.
2 Samuel 8.13 Josué 15.38 1 Chroniques 18.12 Psaumes 60.1 Esaïe 16.1
8 Ndipo Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, Njoo, tutazamane uso kwa uso.
2 Chroniques 25.17-25.24 2 Rois 14.11 2 Samuel 2.14-2.17 Proverbes 18.6 Proverbes 20.18
9 Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma kwa Amazia mfalme wa Yuda, akisema, Mbaruti uliokuwako Lebanoni ulituma kwa mwerezi uliokuwako Lebanoni, kusema, Umwoze mwanangu binti yako; kukapita hayawani aliyekuwako Lebanoni, akaukanyaga ule mbaruti.
Juges 9.8-9.15 1 Rois 4.33 Osée 9.6 2 Samuel 12.1-12.4 2 Chroniques 25.10-25.13
10 Kweli umepiga Edomu, na moyo wako umekutukuza; ujisifu basi, ukae nyumbani mwako. Mbona unataka kujitia bure katika madhara, hata uanguke, wewe na Yuda pamoja nawe?
2 Chroniques 26.16 Deutéronome 8.14 2 Chroniques 32.25 Proverbes 20.3 Proverbes 16.18
11 Lakini Amazia hakutaka kusikia. Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea; wakatazamana uso kwa uso, yeye na Amazia mfalme wa Yuda, huko Beth-shemeshi ulio wa Yuda.
Josué 19.38 2 Chroniques 25.20 2 Chroniques 25.16 1 Samuel 6.9-6.19 Josué 21.16
12 Yuda wakashindwa mbele ya Israeli; wakakimbia kila mtu hemani kwake.
2 Samuel 18.17 1 Samuel 4.10 1 Rois 22.36
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamtwaa Amazia mfalme wa Yuda, mwanawe Yoashi mwana wa Ahazia, huko Beth-shemeshi, akaja Yerusalemu, akauvunja ukuta wa Yerusalemu toka lango la Efraimu hata lango la pembeni, mikono mia nne.
Néhémie 12.39 Néhémie 8.16 Jérémie 31.38 Zacharie 14.10 2 Chroniques 36.6
14 Akaitwaa dhahabu yote na fedha, na vyombo vyote vilivyoonekana katika nyumba ya Bwana, na katika hazina za nyumba ya mfalme, tena watu, kuwa amana; akarudi Samaria.
1 Rois 14.26 1 Rois 7.51 1 Rois 15.18 2 Rois 24.13 2 Rois 25.15
15 Basi mambo yote ya Yehoashi yaliyosalia, aliyoyafanya, na ushujaa wake, na jinsi alivyopigana na Amazia mfalme wa Yuda, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 14.19-14.20 2 Rois 10.34-10.35 2 Rois 13.12-13.13
16 Yehoashi akalala na baba zake, akazikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli; na Yeroboamu mwanawe akatawala mahali pake.
Amos 7.10-7.11 Osée 1.1 2 Samuel 7.12 Amos 1.1 2 Rois 13.13
17 Naye Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda akaishi baada ya kufa kwake Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli miaka kumi na mitano.
2 Chroniques 25.25-25.28 2 Rois 14.1-14.2 2 Rois 14.23 2 Rois 13.10
18 Basi mambo yote ya Amazia yaliyosalia, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
2 Rois 13.8 2 Rois 13.12 1 Rois 14.29 1 Rois 11.41
19 Wakafanya fitina juu yake katika Yerusalemu, naye akakimbia mpaka Lakishi, lakini wakatuma watu kumfuata mpaka Lakishi, wakamwua huko.
Josué 10.31 2 Rois 15.25 2 Rois 18.14 2 Rois 15.14 2 Rois 21.23
20 Wakamleta juu ya farasi; naye akazikwa huko Yerusalemu pamoja na babaze katika mji wa Daudi.
2 Rois 9.28 2 Rois 8.24 2 Rois 12.21 1 Rois 11.43 2 Chroniques 26.23
21 Na watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia aliyekuwa mwenye umri wa miaka kumi na sita,wakamfanya awe mfalme mahali pa baba yake Amazia.
2 Rois 21.24 Matthieu 1.8-1.9 2 Rois 15.13 1 Chroniques 3.12 2 Chroniques 26.1
22 Huyo akajenga Elathi, akaurudisha kwa Yuda, baada ya kulala mfalme pamoja na babaze.
2 Rois 16.6 1 Rois 9.26 Deutéronome 2.8 2 Chroniques 26.2 2 Chroniques 8.17

Règne de Jéroboam II sur Israël

23 Katika mwaka wa kumi na tano wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala katika Samaria; akatawala miaka arobaini na mmoja.
Amos 1.1 2 Rois 14.27 Amos 7.9-7.11 Osée 1.1
24 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana; wala hakuyaacha makosa yote ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli.
Psaumes 106.20 Deutéronome 9.18 2 Rois 13.6 Genèse 38.7 1 Rois 12.28-12.31
25 Yeye akaurudisha mpaka wa Israeli toka kuingia kwa Hamathi hata bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, alilolinena kwa mkono wa mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii, aliyekuwa wa Gath-heferi.
Deutéronome 3.17 Josué 19.13 Jonas 1.1 Matthieu 12.39-12.40 1 Rois 8.65
26 Kwani Bwana akayaona mateso ya Israeli, kwamba yalikuwa machungu sana; maana hakukuwa na mfungwa wala asiyefungwa, wala msaidizi kwa ajili ya Israeli.
Deutéronome 32.36 2 Rois 13.4 Exode 3.7 Exode 3.9 Psaumes 106.43-106.45
27 Wala Bwana hakusema ya kwamba atalifuta jina la Israeli litoke chini ya mbingu; lakini akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
2 Rois 13.23 2 Rois 13.5 Apocalypse 3.5 Psaumes 69.28 Deutéronome 9.14
28 Basi mambo yote ya Yeroboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, na jinsi aliyvopigana, akawapatia tena Israeli Dameski na Hamathi, iliyokuwa kwanza ya Yuda, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 11.24 1 Chroniques 18.5-18.6 2 Samuel 8.6 2 Chroniques 8.3-8.4
29 Yeroboamu akalala na babaze, yaani, na wafalme wa Israeli. Na Zekaria mwanawe akatawala mahali pake.
2 Rois 15.8

Cette Bible est dans le domaine public.