Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 11.18
Bible en Swahili de l’est


Idolâtrie de Salomon

1 Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,
Deutéronome 17.17 Néhémie 13.23-13.27 Proverbes 2.16 Lévitique 18.18 Proverbes 5.8-5.20
2 na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.
Exode 34.16 Deutéronome 7.3-7.4 Exode 23.32-23.33 Nombres 25.1-25.3 Josué 23.12-23.13
3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
2 Samuel 5.13-5.16 2 Samuel 3.2-3.5 Juges 9.5 Ecclésiaste 7.28 2 Chroniques 11.21
4 Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.
1 Rois 9.4 1 Rois 8.61 1 Rois 11.42 1 Rois 14.21 2 Chroniques 34.2
5 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni.
1 Rois 11.7 Juges 2.13 1 Rois 11.33 2 Rois 23.13 Juges 10.6
6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.
Nombres 14.24 Josué 14.8 Josué 14.14
7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.
Nombres 21.29 Juges 11.24 Actes 7.43 Deutéronome 17.3-17.4 2 Rois 23.13-23.14
8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu.
1 Corinthiens 10.11-10.12 Ezéchiel 16.22-16.29 1 Corinthiens 10.20-10.22 Osée 4.11-4.12 1 Rois 11.1
9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili,
1 Rois 9.2 1 Rois 3.5 Esaïe 29.13-29.14 Psaumes 78.58-78.60 Deutéronome 3.26
10 akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana.
2 Chroniques 7.17-7.22 1 Rois 9.4-9.7 1 Rois 6.12-6.13
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako.
1 Rois 11.31 1 Rois 12.15-12.16 1 Rois 12.20 2 Rois 17.21 2 Samuel 12.9-12.12
12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako.
2 Rois 22.19-22.20 2 Rois 20.19 Exode 20.5 Genèse 12.2 Genèse 19.29
13 Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.
1 Rois 12.20 1 Rois 11.32 Deutéronome 12.11 Deutéronome 12.5 1 Rois 11.39

Ennemis de Salomon

14 Ndipo Bwana akamwondokeshea Sulemani adui, Hadadi Mwedomi; yeye alikuwa wa wazao wake mfalme wa Edomu.
1 Rois 12.15 2 Samuel 24.1 Esaïe 10.26 Esaïe 13.17 1 Chroniques 5.26
15 Kwa maana ikawa, Daudi alipokuwako Edomu, naye Yoabu, mkuu wa jeshi, amepanda awazike waliouawa, akiisha kumpiga kila mwanamume wa Edomu,
2 Samuel 8.14 1 Chroniques 18.12-18.13 Deutéronome 20.13 Genèse 25.23 Nombres 31.17
16 (kwa kuwa Yoabu alikaa huko miezi sita pamoja na Israeli wote, hata alipompoteza kila mwanamume wa Edomu);
17 yule Hadadi alikimbia, yeye na Waedomi wengine, watumishi wa baba yake, pamoja naye, waende Misri; yule Hadadi akali ni mtoto mdogo.
2 Samuel 4.4 Exode 2.1-2.10 Matthieu 2.13-2.14 2 Rois 11.2
18 Wakaondoka katika Midiani, wakafika Parani; wakachukua pamoja nao watu toka Parani, wakafika Misri, kwa Farao mfalme wa Misri; aliyempa nyumba, akamwamria vyakula, akampa mashamba.
Nombres 10.12 Deutéronome 1.1 Deutéronome 33.2 Genèse 21.21 Nombres 25.18
19 Hadadi akapendeza sana machoni pa Farao, hata akamwoza umbu la mkewe, umbu la Tapenesi aliyekuwa malkia.
Actes 7.10 Actes 7.21 Genèse 39.21 Genèse 41.45 Jérémie 43.7-43.9
20 Naye huyo umbu la Tapenesi akamzalia Genubathi mwanawe, ambaye Tapenesi alimlea nyumbani mwa Farao; naye Genubathi akawako nyumbani mwa Farao pamoja na wana wa Farao.
Genèse 21.7 1 Samuel 1.24
21 Naye Hadadi aliposikia huko Misri ya kuwa Daudi amelala na babaze, na Yoabu, jemadari wa jeshi, amekufa, Hadadi akamwambia Farao, Unipe ruhusa, niende mpaka nchi yangu.
1 Rois 2.10 2 Samuel 3.21 1 Samuel 9.26 Exode 4.19 Josué 2.21
22 Farao akamwambia, Umekosa nini kwangu, hata, tazama, unatafuta kuirudia nchi yako? Akajibu, Hakuna, lakini unipe ruhusa tu.
Marc 14.31 Psaumes 37.8 Jérémie 2.31 2 Samuel 18.22-18.23 Luc 22.35
23 Tena, Mungu akamwondokeshea adui mwingine, Rezoni mwana wa Eliada, aliyemkimbia bwana wake Hadadezeri mfalme wa Soba,
1 Rois 11.14 2 Samuel 8.3 2 Samuel 10.8 Psaumes 60.1 1 Chroniques 19.16-19.19
24 naye akakusanya watu, akawa mkuu wa jeshi, hapo Daudi alipowaua hao watu wa Soba; wakaenda Dameski, wakakaa humo, na kumiliki huko Dameski.
2 Samuel 10.18 2 Samuel 10.8 1 Rois 19.15 Genèse 14.15 1 Rois 20.34
25 Naye akawa adui wa Israeli siku zote za Sulemani, zaidi ya madhara yake Hadadi; naye akawachukia Israeli, akamiliki juu ya Shamu.
Deutéronome 23.7 2 Chroniques 15.2 Zacharie 11.8 2 Samuel 16.21 1 Rois 5.4
26 Na Yeroboamu wa Nebati, Mwefraimu wa Sereda, mtumwa wake Sulemani; ambaye jina lake mamaye aliitwa Serua, mwanamke aliyefiwa na mumewe; yeye naye akainua mkono wake juu ya mfalme.
2 Chroniques 13.6 1 Rois 12.2 2 Samuel 20.21 1 Rois 11.28 1 Rois 11.11
27 Na hii ndiyo sababu ya yeye kumwinulia mfalme mkono. Sulemani aliijenga Milo, akapafunga palipobomoka pa mji wa baba yake Daudi.
1 Rois 9.24 1 Rois 9.15 Ezéchiel 13.5 2 Samuel 20.21 Esaïe 22.9
28 Na huyo Yeroboamu alikuwa mtu hodari, shujaa; Sulemani akaona ya kuwa kijana huyo ni mtu mwenye bidii, akamweka juu ya kazi yote ya nyumba ya Yusufu.
Proverbes 22.29 Esaïe 14.25 Zacharie 10.6 2 Samuel 19.20 Amos 5.6
29 Ikawa zamani zile Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya, Mshiloni, alikutana naye njiani; naye Ahiya amevaa vazi jipya, na hao wawili walikuwa peke yao mashambani.
1 Rois 14.2 2 Chroniques 9.29 1 Rois 12.15 Josué 18.1 2 Samuel 14.6
30 Ahiya akalishika lile vazi jipya alilokuwa amelivaa, akalirarua vipande kumi na viwili.
1 Samuel 15.27-15.28 1 Samuel 24.4-24.5
31 Akamwambia Yeroboamu, Twaa wewe vipande kumi, maana Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nitaurarua ufalme, na kuuondoa katika mkono wa Sulemani, nami nitakupa wewe kabila kumi,
1 Rois 11.11-11.12
32 (lakini yeye atakuwa na kabila moja kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalemu mji ule niliouchagua katika miji yote ya kabila za Israeli);
1 Rois 11.13 1 Rois 12.20-12.21 1 Rois 14.21
33 kwa sababu wameniacha mimi wakaabudu Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu wa Wamoabi, na Milkomu, mungu wa wana wa Amoni wala hawakuenda katika njia zangu, kutenda mema machoni pangu, kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, kama Daudi baba yake.
1 Rois 11.9 1 Rois 11.5-11.7 1 Chroniques 28.9 Jérémie 2.13 1 Rois 3.14
34 Walakini sitauondoa ufalme wote katika mkono wake; lakini nitamfanya awe mkuu siku zote za maisha yake, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi niliyemchagua kwa maana alizishika amri zangu na sheria zangu,
Job 11.6 Habakuk 3.2 Psaumes 103.10 1 Rois 11.12-11.13 Esaïe 55.3
35 lakini nitauondoa ufalme katika mkono wa mwanawe, nami nitakupa wewe kabila kumi.
Exode 20.5-20.6 1 Rois 11.12 1 Rois 12.20 2 Chroniques 10.15-10.17 1 Rois 12.15-12.17
36 Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili Daudi, mtumishi wangu, apate kuwa na taa siku zote mbele zangu katika Yerusalemu, mji ule niliouchagua niweke jina langu huko.
2 Rois 8.19 1 Rois 15.4 1 Rois 11.13 2 Samuel 21.17 2 Chroniques 21.7
37 Nami nitakutwaa wewe, nawe utatawala kama roho yako inavyotamani, nawe utakuwa mfalme juu ya Israeli.
2 Samuel 3.21 1 Rois 11.26 Deutéronome 14.26
38 Tena itakuwa, ukiyasikia yote nitakayokuamuru, na kuenda katika njia zangu, na kutenda yaliyo mema machoni pangu, ili kuzishika amri zangu na hukumu zangu kama Daudi mtumishi wangu alivyotenda, basi, nitakuwa pamoja nawe, nitakujengea nyumba iliyo imara, kama nilivyomjengea Daudi, nami nitakupa wewe Israeli.
2 Samuel 7.11 Josué 1.5 Deutéronome 31.8 2 Samuel 7.26-7.29 1 Rois 9.4-9.5
39 Tena nitawatesa wazao wa Daudi kwa sababu hii, lakini si daima.
1 Rois 11.36 Jérémie 23.5-23.6 1 Rois 12.16 Luc 1.32-1.33 Luc 2.11
40 Basi Sulemani akataka kumwua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akaondoka, akakimbilia Misri, kwa Shishaki, mfalme wa Misri, akakaa katika Misri hata wakati wa kufa kwake Sulemani.
2 Chroniques 12.2-12.9 Esaïe 14.24-14.27 1 Rois 14.25-14.26 Proverbes 21.30 Esaïe 46.10

Mort de Salomon

41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani?
2 Chroniques 9.29-9.31
42 Na siku alizotawala Sulemani katika Yerusalemu juu ya Israeli wote zilikuwa miaka arobaini.
1 Rois 2.11
43 Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi baba yake; na Rehoboamu mwanawe akatawala mahali pake.
1 Rois 2.10 2 Rois 21.18 Matthieu 1.7 2 Chroniques 9.31 Jérémie 22.19

Cette Bible est dans le domaine public.