Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 1.8
Bible en Swahili de l’est


Règne de Salomon

Vieillesse de David et prétentions d’Adonija

1 Mfalme Daudi alikuwa mzee, mkongwe katika siku zake, nao wakamfunika nguo, lakini asipate moto.
Josué 23.1-23.2 1 Chroniques 29.27-29.28 Luc 1.7 Genèse 24.1 Psaumes 90.10
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, Bwana wangu mfalme na atafutiwe kijana mwanamwali; naye asimame mbele ya mfalme, amtunze; alale kifuani mwako, ili bwana wangu mfalme apate moto.
Ecclésiaste 4.11 Deutéronome 13.6 Deutéronome 10.8 2 Chroniques 29.11 Michée 7.5
3 Basi wakatafuta kijana mzuri mipakani mwote mwa Israeli, wakamwona Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
Josué 19.18 1 Samuel 28.4 Esther 2.2 Esther 2.4 2 Rois 4.25
4 Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua.
Matthieu 1.25
5 Ndipo Adonia mwana wa Hagithi akatakabari, akasema, Mimi nitakuwa mfalme. Akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, na watu hamsini wapige mbio mbele yake.
2 Samuel 15.1 2 Samuel 3.4 1 Chroniques 28.5 Exode 9.17 Luc 18.14
6 Tena baba yake hakumchukiza wakati wo wote kwa kusema, Mbona umefanya hivi? Kisha, alikuwa mtu mzuri sana; naye alizaliwa baada ya Absalomu.
2 Samuel 3.3-3.4 1 Chroniques 3.2 1 Samuel 3.13 1 Samuel 10.23 Hébreux 12.5-12.6
7 Akashauriana na Yoabu, mwana wa Seruya, na Abiathari, kuhani; nao wakamsaidia Adonia, wakamfuata.
2 Samuel 20.25 1 Rois 2.22 2 Samuel 20.23 1 Samuel 22.20-22.23 1 Rois 2.26-2.35
8 Ila Sadoki, kuhani, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Nathani, nabii, na Shimei, na Rei, na mashujaa wa Daudi, hao hawakuwa pamoja na Adonia.
1 Rois 4.18 2 Samuel 20.25 2 Samuel 23.8-23.39 Ezéchiel 44.15 1 Rois 2.35
9 Adonia akachinja kondoo, na ng’ombe, na vinono, karibu na jiwe la Zohelethi, lililo karibu na chemchemi Rogeli; akawaita ndugu zake wote, wana wa mfalme, na watu wote wa Yuda, watumishi wa mfalme;
2 Samuel 17.17 2 Samuel 13.23-13.27 Proverbes 15.8 2 Samuel 15.11-15.12 Josué 15.7
10 ila Nathani, nabii, na Benaya, na mashujaa, na Sulemani nduguye, hakuwaita hao.
2 Samuel 12.24 1 Rois 1.8 2 Samuel 12.1-12.15 1 Rois 1.19

Désignation de Salomon comme roi

11 Ndipo Nathani akamwambia Bath-sheba, mamaye Sulemani, akasema, Je! Hukusikia ya kuwa Adonia, mwana wa Hagithi, anamiliki, na bwana wetu Daudi hana habari?
2 Samuel 3.4 1 Chroniques 28.4-28.5 2 Samuel 12.24-12.25 1 Chroniques 22.9-22.10 2 Samuel 7.12-7.17
12 Haya basi, nikupe shauri, tafadhali, upate kuiokoa roho yako, na roho ya mwanao Sulemani.
Jérémie 38.15 Actes 27.31 Proverbes 27.9 Proverbes 11.14 Genèse 19.17
13 Enenda uingie ndani kwa mfalme Daudi, ukamwambie, Je! Hukuniapia mimi mjakazi wako, Ee mfalme, bwana wangu, kusema, Hakika yake Sulemani mwana wako atamiliki baada yangu, na kuketi katika kiti changu cha enzi? Mbona basi anamiliki Adonia?
1 Rois 1.30 1 Rois 1.17 1 Rois 1.35 Jérémie 33.21 1 Rois 2.12
14 Tazama, wakati ule utakapokuwa katika kusema na mfalme, mimi nami nitaingia nyuma yako, na kuyahakikisha maneno yako.
1 Rois 1.17-1.27 2 Corinthiens 13.1
15 Basi Bath-sheba akaingia ndani kwa mfalme, ndani ya chumba chake; naye mfalme alikuwa mzee sana; na Abishagi, Mshunami, alikuwa akimtumikia mfalme.
1 Rois 1.1
16 Bath-sheba akainama, akamsujudia mfalme. Naye mfalme akamwuliza, Wataka nini?
1 Rois 2.20 1 Samuel 20.41 1 Samuel 24.8 Matthieu 20.32 Esther 7.2
17 Akamwambia, Bwana wangu, uliniapia mimi mjakazi wako kwa Bwana, Mungu wako, ya kwamba, bila shaka Sulemani mwanao atamiliki baada yangu, yeye ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi.
1 Rois 1.13 1 Rois 1.30 Genèse 18.12 1 Pierre 3.6
18 Na sasa, angalia, Adonia anamiliki; na wewe, bwana wangu mfalme, huna habari.
1 Rois 1.24 1 Rois 1.11 Actes 3.17 1 Rois 1.5 2 Samuel 15.10
19 Tena amechinja ng’ombe, na vinono, na kondoo tele, na kuwaita wana wa mfalme wote pia, na Abiathari, kuhani, na Yoabu, jemadari wa jeshi. Ila Sulemani, mtumishi wako, huyu hakumwita.
1 Rois 1.25 1 Rois 1.7-1.10
20 Ee mfalme, bwana wangu, macho ya Israeli wote yanakuelekea wewe, kwamba uwaambie ni nani atakayeketi katika kiti chako cha enzi baada yako, Ee mfalme, bwana wangu.
2 Samuel 23.2 1 Chroniques 29.1 Psaumes 25.15 1 Chroniques 28.10 Psaumes 123.2
21 Ama sivyo itakuwa, bwana wangu mfalme atakapolala pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Sulemani tutahesabiwa kuwa wahalifu.
1 Rois 2.10 Deutéronome 31.16 Genèse 15.15 1 Rois 2.15 1 Rois 2.22-2.24
22 Basi tazama, alipokuwa katika kusema na mfalme, Nathani, nabii, aliingia.
Job 1.16-1.18 Genèse 24.15 Daniel 9.20
23 Wakamwambia mfalme wakasema, Tazama, Nathani, nabii. Naye alipoingia ndani mbele ya mfalme, akamsujudia kifudifudi.
Romains 13.7 1 Pierre 2.17 1 Rois 1.16
24 Nathani akasema, Ee mfalme, bwana wangu, je! Wewe umesema ya kwamba, Adonia atamiliki baada yangu, ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi?
1 Rois 1.17-1.18 1 Rois 1.5 1 Rois 1.13-1.14
25 Maana leo ameshuka, na kuchinja ng’ombe, na vinono, na kondoo tele, naye amewaita wana wote wa mfalme, na majemadari wa jeshi, na Abiathari, kuhani; na tazama, wanakula na kunywa mbele yake, wakisema, Na aishi mfalme Adonia!
1 Samuel 10.24 1 Rois 1.19 1 Rois 1.9 2 Samuel 16.16 Marc 11.9-11.10
26 Walakini mimi, mimi mtumishi wako, na Sadoki, kuhani, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Sulemani, mtumishi wako, hakutuita sisi.
1 Rois 1.8 1 Rois 1.10 1 Rois 1.19 2 Samuel 7.2 2 Samuel 12.25
27 Je! Bwana wangu mfalme ndiye aliyelitenda jambo hili, bila kutujulisha sisi watumishi wako ni nani atakayeketi katika kiti cha enzi cha bwana wangu mfalme baada yake?
Jean 15.15 2 Rois 4.27 1 Rois 1.24
28 Ndipo mfalme Daudi akajibu, akasema, Niitieni Bath-sheba. Basi akaingia ndani kwa mfalme, akasimama mbele ya mfalme.
29 Naye mfalme akaapa, akasema, Bwana aishivyo, aliyenikomboa roho yangu katika shida zote,
2 Samuel 4.9 2 Samuel 12.5 2 Rois 4.30 2 Rois 5.20 2 Rois 5.16
30 hakika yake nitafanya leo kama vile nilivyokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, nikasema, Kwa yakini Sulemani mwanao atamiliki baada yangu, naye ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi badala yangu.
1 Rois 1.17 1 Rois 1.13
31 Ndipo Bath-sheba akainama kifudifudi, akamsujudia mfalme, akasema, Bwana wangu mfalme Daudi na aishi milele.
Daniel 2.4 Daniel 3.9 Daniel 6.6 Daniel 6.21 Néhémie 2.3
32 Naye mfalme Daudi akasema, Niitie Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada. Nao wakaingia ndani mbele ya mfalme.
1 Rois 1.8 1 Rois 1.26 1 Rois 1.38
33 Naye mfalme akawaambia, Twaeni pamoja nanyi watumishi wa bwana wenu, mkampandishe Sulemani mwanangu juu ya nyumbu wangu mimi mkamtelemshe mpaka Gihoni;
2 Chroniques 32.30 1 Rois 1.38 2 Chroniques 33.14 Genèse 41.43 Esther 6.6-6.11
34 kisha Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na wamtie mafuta huko, awe mfalme juu ya Israeli; kapigeni panda, mkaseme, Mfalme Sulemani na aishi!
2 Samuel 15.10 1 Samuel 10.1 1 Rois 1.25 1 Rois 19.16 2 Rois 9.13
35 Kisha pandeni juu nyuma yake, naye atakuja ili aketi katika kiti changu cha enzi; kwa maana atakuwa mfalme badala yangu; ndiye niliyemweka awamiliki Israeli na Yuda.
1 Rois 1.13 1 Rois 1.17 1 Chroniques 28.4-28.5 1 Chroniques 23.1 1 Rois 2.15
36 Basi Benaya, mwana wa Yehoyada, akamjibu mfalme, akasema, Amina; Bwana, Mungu na bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
Deutéronome 27.15-27.26 1 Chroniques 17.27 Jérémie 28.6 1 Samuel 25.29 1 Corinthiens 14.16
37 Kama vile Bwana alivyokuwa pamoja na bwana wangu mfalme, kadhalika na awe pamoja na Sulemani, na kufanya kiti chake cha enzi kuwa kitukufu kuliko kiti cha enzi cha bwana wangu mfalme Daudi.
1 Rois 1.47 1 Samuel 20.13 Josué 1.17 Josué 1.5 Psaumes 46.7
38 Basi wakashuka Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Wakerethi, na Wapelethi, wakampandisha Sulemani juu ya nyumbu wa mfalme Daudi, wakampeleka mpaka Gihoni.
2 Samuel 8.18 1 Rois 1.8 1 Rois 1.33 1 Chroniques 18.17 2 Samuel 20.20-20.23
39 Na Sadoki, kuhani, akatwaa ile pembe ya mafuta katika Hema, akamtia Sulemani mafuta. Nao wakapiga panda; na watu wote wakasema, Mfalme Sulemani na aishi!
Psaumes 89.20 1 Samuel 10.24 1 Rois 1.34 1 Chroniques 29.22 2 Rois 11.12
40 Kisha watu wote wakapanda juu nyuma yake, watu wakapiga mazomari, wakafurahi furaha kubwa mno, hata nchi ikapasuka kwa sauti zao.
1 Chroniques 12.38-12.40 Daniel 3.5 Zacharie 9.9 Luc 19.37 Apocalypse 11.15-11.18
41 Basi Adonia, na wageni wote waliokuwa pamoja naye, wakasikia hayo walipokuwa wamekwisha kula. Naye Yoabu aliposikia sauti ya panda alisema, Za nini kelele hizi za mji uliotaharuki?
Ecclésiaste 7.4-7.6 Job 20.5 Matthieu 24.38-24.39 Proverbes 14.13 Exode 32.17
42 Naye alipokuwa katika kunena, tazama Yonathani, mwana wa Abiathari kuhani, akafika. Naye Adonia akasema, Karibu; maana wewe u mtu mwema, unaleta habari njema.
2 Samuel 15.36 2 Samuel 17.17 2 Samuel 18.27 2 Samuel 15.27 1 Thessaloniciens 5.2-5.3
43 Naye Yonathani akajibu, akamwambia Adonia, Hakika bwana wetu mfalme Daudi amemtawaza Sulemani.
44 Tena mfalme alipeleka pamoja naye Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Wakerethi, na Wapelethi, wakampandisha juu ya nyumbu wa mfalme.
45 Kisha Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, wakamtia mafuta huko Gihoni, ili awe mfalme. Nao wamepanda juu kutoka huko wakifurahi, hata mji ukavuma. Ndizo kelele zile mlizozisikia.
1 Rois 1.40 Esdras 3.13 Daniel 5.26-5.28 1 Samuel 28.14 1 Samuel 4.5
46 Na tena, Sulemani ameketi katika kiti cha enzi cha ufalme.
1 Chroniques 29.23 Psaumes 132.11 Aggée 2.22 1 Rois 1.13
47 Na tena, watumishi wa mfalme walifika, ili wambariki bwana wetu mfalme Daudi, wakisema, Mungu wako na alikuze jina la Sulemani kuliko jina lako, na kukifanya kiti chake cha enzi kuwa kitukufu kuliko kiti chako. Naye mfalme akainama chini juu ya kitanda chake.
1 Rois 1.37 Genèse 47.31 2 Samuel 21.3 Esdras 6.10 Psaumes 20.1-20.4
48 Na tena, mfalme akasema hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenipa leo hivi mtu wa kuketi katika kiti changu cha enzi, nayo macho yangu yakiwa yanaona hayo.
1 Rois 3.6 Psaumes 132.11-132.12 Daniel 4.34 Psaumes 145.2 Psaumes 41.13
49 Ndipo wageni wote waliokuwa pamoja na Adonia wakaogopa, wakaondoka, wakaenda zao kila mtu njia yake.
Esaïe 21.4-21.5 Proverbes 28.1 Daniel 5.4-5.6
50 Adonia naye akaogopa mbele ya Sulemani; akaondoka, akaenda, akazishika pembe za madhabahu.
1 Rois 2.28 Exode 27.2 Psaumes 118.27 Exode 38.2 Exode 21.14
51 Akaambiwa Sulemani, kusema, Tazama, Adonia amwogopa mfalme Sulemani; kwani, tazama, amezishika pembe za madhabahu, akisema, Mfalme Sulemani na aniapie leo kwamba hataniua mimi mtumwa wake kwa upanga.
52 Akasema Sulemani, Akionekana kuwa mtu wa kweli, hata unywele mmoja wake hautaanguka chini; lakini uovu ukionekana ndani yake, atakufa.
1 Samuel 14.45 2 Samuel 14.11 Actes 27.34 Job 15.22 Luc 21.18
53 Basi mfalme Sulemani akatuma watu, wakamtelemsha toka madhabahuni. Naye akaja, akamwinamia mfalme Sulemani; naye Sulemani akamwambia, Enenda nyumbani kwako.
1 Rois 1.16 2 Samuel 14.24 1 Rois 2.36 2 Samuel 1.2 2 Samuel 14.28

Cette Bible est dans le domaine public.