Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 49.10
Bible en Swahili de l’est


Bénédiction et mort de Jacob

1 Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho.
Nombres 24.14 Daniel 10.14 Jérémie 23.20 Deutéronome 4.30 Esaïe 2.2
2 Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu.
Psaumes 34.11 Proverbes 4.1-4.4 Proverbes 7.1 Proverbes 1.8-1.9 Proverbes 7.24
3 Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu.
Deutéronome 21.17 Psaumes 78.51 Genèse 29.32 Psaumes 105.36 Nombres 1.20
4 Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako, Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda changu.
Genèse 35.22 1 Chroniques 5.1 Deutéronome 27.20 Nombres 32.1-32.42 Genèse 46.8
5 Simeoni na Lawi ni ndugu; Panga zao ni silaha za jeuri.
Genèse 34.25-34.31 Genèse 29.33-29.34 Proverbes 18.9 Genèse 46.10-46.11
6 Nafsi yangu, usiingie katika siri yao, Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao, Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu, Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng’ombe;
Psaumes 26.9 Genèse 34.30 Psaumes 57.8 Psaumes 16.9 Psaumes 64.2
7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali, Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma. Nitawagawa katika Yakobo, Nitawatawanya katika Israeli.
Josué 19.1-19.9 1 Chroniques 4.24-4.31 Josué 21.1-21.45 Proverbes 27.3 1 Chroniques 4.39-4.40
8 Yuda, ndugu zako watakusifu, Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia.
1 Chroniques 5.2 Hébreux 7.14 Genèse 27.29 Genèse 29.35 Deutéronome 33.7
9 Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?
Nombres 24.9 Nombres 23.24 Apocalypse 5.5 Osée 5.14 Michée 5.8
10 Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.
Psaumes 60.7 Nombres 24.17 Luc 1.32-1.33 Esaïe 42.1 Esaïe 33.22
11 Atafunga punda wake katika mzabibu, Na mwana-punda wake katika mzabibu mzuri. Amefua nguo zake kwa mvinyo, Na mavazi yake kwa damu ya zabibu.
2 Rois 18.32 1 Rois 4.25 Joël 3.18 Esaïe 63.1-63.3 Michée 4.4
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo, Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
13 Zabuloni atakaa pwani ya bahari, Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu, Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.
Deutéronome 33.18-33.19 Genèse 30.20 Josué 19.10-19.16
14 Isakari ni punda hodari, Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo;
1 Chroniques 12.32 Genèse 30.18 Juges 10.1 Josué 19.17-19.23 Juges 5.15-5.16
15 Akaona mahali pa raha, kuwa pema, Na nchi, ya kuwa ni nzuri, Akainama bega lake lichukue mizigo, Akawa mtumishi kwa kazi ngumu.
Ezéchiel 29.18 2 Samuel 7.1 Juges 3.11 Psaumes 81.6 Josué 14.15
16 Dani atahukumu watu wake, Kama moja ya makabila ya Israeli;
Deutéronome 33.22 Genèse 30.6 Nombres 10.25 Juges 15.20 Juges 18.26-18.27
17 Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katika njia, Aumaye visigino vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali.
1 Chroniques 12.35 Juges 18.22-18.31 Juges 16.22-16.30 Juges 14.1-14.15
18 Wokovu wako nimeungoja, Ee Bwana.
Psaumes 119.174 Psaumes 119.166 Esaïe 25.9 Michée 7.7 Luc 2.25
19 Gadi, jeshi litamsonga, Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
Genèse 30.11 Nombres 32.1-32.42 1 Chroniques 5.11-5.22 1 Chroniques 3.18-3.22 Juges 10.1-10.11
20 Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.
Deutéronome 33.24-33.25 Genèse 30.13 Josué 19.24-19.31 Genèse 46.17
21 Naftali ni ayala aliyefunguliwa; Anatoa maneno mazuri.
Deutéronome 33.23 Genèse 30.8 Juges 5.18 Genèse 46.24 Josué 19.32-19.39
22 Yusufu ni mti mchanga wenye kuzaa, Mti mchanga wenye kuzaa karibu na chemchemi, Matwi yake yametanda ukutani.
Genèse 41.52 Genèse 48.1 Psaumes 128.1 Ezéchiel 19.11 Genèse 46.27
23 Wapiga mishale walimtenda machungu, Wakamtupia, wakamwudhi,
Genèse 37.24 Genèse 37.28 Psaumes 64.3 Genèse 37.18 Psaumes 118.13
24 Lakini upinde wake ukakaa imara, Mikono yake ikapata nguvu, Kwa mikono ya Mwenye Enzi wa Yakobo; Kwa jina la mchungaji, yeye jiwe la Israeli,
Esaïe 28.16 Psaumes 132.5 Psaumes 132.2 Psaumes 18.30 Job 29.20
25 Naam, kwa Mungu wa baba yako atakaye kusaidia; Kwa mibaraka ya mbinguni juu. Mibaraka ya vilindi vilivyo chini, Mibaraka ya maziwa, na ya mimba.
Genèse 28.13 Genèse 35.11 Genèse 35.3 Philippiens 4.19 Genèse 17.1
26 Mibaraka ya baba yako Imepita mibaraka ya milima ya kale, Vitu vinavyotamanika vya vilima vya milele; Na vikae juu ya kichwa cha Yusufu, Juu ya utosi wa kichwa chake aliye mkuu kati ya ndugu zake.
Deutéronome 33.15-33.16 Habakuk 3.6 Ephésiens 1.3 Psaumes 89.36 Esaïe 66.5
27 Benyamini ni mbwa-mwitu mwenye kurarua-rarua Asubuhi atakula mawindo, Na jioni atagawanya mateka.
Ezéchiel 22.27 Juges 20.25 Juges 20.21 Genèse 35.18 1 Samuel 11.4-11.11
28 Hizo zote ndizo kabila za Israeli kumi na mbili. Na hayo ndiyo aliyowaambia baba yao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa mbaraka wake aliwabariki.
1 Rois 18.31 Actes 26.7 Esther 8.9 Ezéchiel 39.8-39.10 Esther 8.11
29 Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;
Genèse 47.30 Genèse 50.13 Genèse 15.15 Genèse 25.8-25.17 Hébreux 12.23
30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.
Genèse 23.8-23.9 Genèse 23.16-23.18 Genèse 23.20
31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;
Genèse 25.9 Genèse 35.29 Genèse 47.30 Actes 7.16 Genèse 23.3
32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi.
Genèse 23.17-23.20
33 Basi Yakobo alipokwisha kuwaagiza wanawe, akakunja miguu yake kitandani, akafa, akakusanywa pamoja na watu wake.
Genèse 49.29 Genèse 25.8 Job 30.23 Luc 2.29 Genèse 25.17

Cette Bible est dans le domaine public.